Wednesday, September 7, 2016

Ndanda FC ‘Waikomalia’ tena Yanga Nangwanda Mtwara.


Heka heka langoni mwa timu ya Ndanda.


Kikosi cha Ndanda kilianza katika mechi dhidi ya Yanga Nangwanda Mtwara. Timu hizo zilitoka suluhu ya 0-0



Juma Mohamed, Mtwara.

Klabu ya soka ya Ndanda FC ya mkoani Mtwara imeendelea kuwabania Yanga kuweza kuapata ushindi katika uwanja wa Nangwanda Sijaona ambapo katika mchezo wa leo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara wamelazimishwa suluhu ya bila kufungana.
Mchezo huo ulioamriwa na mwamuzi Hance Mabena kutoka jijini Tanga akisaidiwa na Nicholous Makaranga na Haji Mwalukuta, ulikuwa ni wa kushambuliana zamu kwa zamu huku timu zote zikijaribu kufanya madiliko kadhaa ambayo hata hivyo hayakuzaa matunda.

Kikosi cha Yanga kilianza katika mechi dhidi ya Ndanda. Mechi hiyo iliisha kwa suluhu ya 0-0



Yanga walimbadilisha Deus Kaseke ambaye alionyeshwa kadi ya njano na nafasi yake kuchukuliwa na Juma Maadhi, huku Ndanda wakimtoa kiungo Salum Minelly ambaye pia alionywa kwa kadi ya Njano na nafasi yake kuchukuliwa na Nassoro Kapama.
Baada ya mchezo huo makocha wa timu zote mbili Juma Mwambusi ambaye ni msaidizi wa Hans Van Pluijm wa Yanga na Hamimu Mawazo wa Ndanda wameeleza maoni yao.
“Hii ni mara ya pili tunacheza na mara ya kwanza tulifungwa hii tumetoka sare, kwahiyo siwezi kusema hatuwezi kushinda uwanja wa Nangwanda..lakini kikubwa ni hali ya hewa na hali ya uwanja kwa tulitegea kutocheza mpira nzuri..” alisema Juma Mwambusi kocha msaidizi wa Yanga.
Naye Hamimu Mawazo wa Ndanda FC alisema kutokana na alikitazama kikosi chake katika mchezo huo amegundua kuwa wameanza kujirekebisha makosa yaliyokuwa yakiwatatiza mwanzo na kwamba kadiri muda unavyokwenda watazidi kuwa sawa.
Kwa upande wa mashabiki, Ndanda wameonekana kuyapokea vizui matokeo hayo na kuahidi kufanya vizuri katika mchezo ujao na Kagera, huku wale wa Yanga wakielekeza lawama zao kwa mwamuzi.

Hii ni mara ya pili kwa Yanga kushindwa kupata matokeo ya ushindi katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara ambapo misimu miwili iliyopita mabingwa hao watetezi wa VPL waliwahi kupoteza mchezo kwa kufungwa mabao 2-1 katika mchezo wa mwisho wa ligi


Wachezaji wa timu za Ndanda na Yanga wakisalimia mashabiki muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wao.

No comments: