Washindi wa maonyesho ya Young Scientists & Technology kutoka Mtwara Girls, Diana Sosoka (kulia) na Nadhra Mresa wakiondoka eneo la uwanja wa ndege Mtwara kuelekea shuleni kwao. |
Wanafunzi wa Mtwara Girls wakifurahia ushindi wa wenzao |
Na Juma Mohamed, Mtwara
Kwa mara
nyingine, mkoa Mtwara umeendelea kufanya vizuri katika elimu baada ya shule ya
sekondari ya wasichana Mtwara kufanikiwa kuwa washindi wa kwanza Kitaifa katika
maonyesho ya wanasayansi na wanateknolojia wachanga (Young Scientists &
Technology) yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, na kutunukiwa zawadi
mbalimbali.
Wanafunzi
Diana Sosoka na Nadhra Mresa wa kidato cha sita, waliopata ushindi huo ambao
ulihusisha shule 150 wamesema kupitia mashine ambayo wameibuni ya kutotolesha
vifaranga vya kuku na kupelekea ushindi huo, inaweza kuwakomboa wanawake kuondokana
na umasikini.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Wasichana Mtwara, wakiwa nje ya uwanja wa ndege wa Mtwara kuwasubiri wenzao washindi wa maonyesho ya Young Scientists & Technology. |
“Hatujapata ‘sapoti’
kubwa sana ya kuweza kutengeneza ‘incubator’ ambayo ni mzuri, matarajio yetu
tungeomba ushirikiano na ‘sapoti’ maana ni biashara hii tunaifanya na pia
tunataka kutoa elimu kwa wanawake..sio wanawake tu, na wanaume pia, kwahiyo
elimu itolewe kwa Watanzania wote ili kuondoa huu umasikini..” alisema Diana.
Mwalimu wa
sayansi alioambatana nao katika maonyesho hayo Rashidi Ally alieleza siri ya
ushindi huo, ambao ulipelekea kupewa zawadi mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha
sh. Milioni 1.7, kusomeshwa bure katika chuo kikuu nje ya nchi baada ya
kumaliza mtihani wa kidato cha sita na kupelekwa nchini Thailand.
Afisa elimu
wa mkoa wa Mtwara Fatuma Kilimia, aliwahusia wanafunzi hao kutokubali
kudanganywa na wanaume na kuharibu malengo yao, na kuwataka kujifunza kusema
hapana.
Washindi wa maonyesho ya Young Scientists & Technology Kitaifa, Diana Sosoka (kulia) na Nadhra Mresa. |
Mkuu wa mkoa
wa Mtwara Halima Dendego, aliahidi kuwaunganisha na shirika la Kuhudumia
viwanda vidogogo SIDO pamoja na chuo cha VETA Mtwara kwa ajili ya kuendeleza
ujuzi wao, pamoja na kuchapisha majina yao katika mashine nyingine za
kutotolesha kuku zitakazotengezwa.
“Hiki
walichofanya watoto wetu mimi niahidi tutawaunganisha wapo wenzetu wa SIDO wapo
wenzetu wa VETA, ili sasa kuuhisha kile walichofanya na waone katika macho yao
kuna wanawake wamewakomboa kwa kutumia akili zao..kwahiyo sisi tutafanya hayo
ili hilo walilotengeneza liwe kwa wingi na ubora Zaidi ili waweze kusonga
mbele..na kwakweli nitawaomba SIDO na VETA waweke nembo kwa kutumia majina zile
mashine zipewe majina kwa kumbukumbu thabiti ya kuukomboa mkoa wa Mtwara.” Alisema
Dendego
Ushindi huo
kwa Mtwara unakuwa ni mafanikio mengine baada ya hivi karibuni kuingia katika
mikoa kumi bora iliyofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita
kutokana na matokeo ya shule ya sekondari ya Tandahimba
No comments:
Post a Comment