Waendesha Pikipiki waliopata mafunzo ya usalama barabarani katika Tarafa ya Mahuta wilayani Tandahimba, wakiwa katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo. |
Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki wa Tarafa ya Mahuta, wilayani Tandahimba akiwaimbisha wanafunzi wake. |
Juma Mohamed, Tandahimba.
Waendesha
Pikipiki za kubeba abiria maarufu Bodaboda wilayani Tandahimba mkoani Mtwara,
wameliomba jeshi la Polisi wilayani humo kuwachukulia hatua kali za kisheria
wanaoendesha vyombo hivyo bila kuvaa kofia ngumu (Helmet) ili kuokoa maisha ya
Watanzania wanaokufa kwa uzembe.
Akizungumza
wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku saba ya usalama barabarani kwa waendesha
pikipiki hao katika Tarafa ya Mahuta wilayani humo, katibu wa mafunzo hayo
Latifu Komba, alisema wengine wanafikia hatua ya kuendesha wakiwa wamevaa
kandambili hali ambayo inashusha hadhi ya kazi hiyo.
“Na kwakua
tulishakaa vikao mbalimbali na kukubaliana kwamba madereva Bodaboda wote
wafuate sheria za usalama barabarani, tunaomba kwanzia leo dereva bodaboda
yeyote ambaye hana kofia ngumu yani Helmet au aliovaa ndala wakati akiendesha
pikipiki na akabeba abiria na hasievaa kofia wote kwa pamoja wachukuliwe hatua
tena hatua kali za kisheria ili kulinda hadhi ya kazi yetu na kuokoa maisha ya
Watanzania wanaokufa kwa uzembe unaoweza kuhepukika..” alisema Komba.
Naye,
kamnada wa polisi wilaya ya Tandahimba, Mrakibu wa Polisi, Fraterine Tesha,
alisema mafunzo hayo yatasaidia kupunguza ugomvi uliokuwapo baina ya waendesha
pikipiki hao na jeshi la polisi na kwamba kwakua wamekiri wenyewe kutii sheria
za usalama barabarani, watakiuka kwa makusudi watachukuliwa hatua.
Mkuu wa
wilaya ya Tandahimba, Sebastian Waryuba, amewasisitiza waendesha pikipiki hao
kwenda kuitumia vizuri elimu waliyoipata ili kuhepuka kupata ajali zisizo za lazima
na kuhatarisha maisha yao.
Mkuu wa wilaya ya Tandahimba, Sebastian Waryuba, akiwahutubia waendesha pikipiki wa Tarafa ya Mahuta, wilayani Tandahimba waliohitimu mafunzo ya usalama Barabarani. |
“Vilema ni
wengi, sikuhizi jamani hakuna ‘spare’ ya kichwa..kwahiyo nduguzangu elimu hii
muitumie vizuri kuhepuka kupata ajai, vaa ‘helmet’ mwingine anaona akivaa ‘helmet’
sura yake itakuwa imefichwa hataonekana, hapana sura yako itabaki ileile ila
ukitembea na helmet ni kinga tosha..” alisema.
Mbunge wa
Tandahimba, Katani Ahmad, aliwataka waliohitimu mafunzo hayo kwenda
kuwahamasisha wengine ambao walikataa kwa makusudi kuudhuria mafunzo hayo ili
awamu nyingine waweze kujifunza sheria hizo na kudai kuwa wanampa wakati mgumu
kuwatetea pindi wanapokamatwa kwa makosa ya kizembe.
Kwa upande
wake mkurugenzi mtendaji wa shirika la Kupunguza Umasikini na Kutunza Mazingira
(APEC) linalotoa mafunzo hayo, Respicius Timanywa alieleza matarajio ya shirika
hilo baada ya mafunzo hayo.
“Tunatarajia
wahitimu hawa wakimaliza mafunzo haya hatutamwona dereva wa pikipiki akiendesha
bila ‘helmet’..tunatarajia baada ya kumaliza mafunzo haya hatutaona ‘site’
mirror zinang’olewa kwenye pikipiki na kuachwa nyumbani..” alisema.
Katika mafunzo
hayo yaliyofanyika katika vituo vinne tofauti wilayani humo, jumla ya vijana 76
wamehitimu na wanatarajia kupatiwa leseni za udereva.
Picha ya pamoja, mkuu wa wilaya ya Tandahimba, Sebastian Waryuba, viongozi mbalimbali na waendesha pikipiki wa Mahuta. |
No comments:
Post a Comment