MICHEZO NA BURUDANI


Ndanda FC waiduwaza Azam Nangwanda Mtwara


Heka heka langoni mwa Azam, wakati Ndanda waliposawazisha bao kupitia kwa mshambuliaji Omary Mponda katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Ndanda walishinda 2-1.


Nahodha wa Ndanda, Kigi Makasy akiwatambulisha wachezaji wenzake kwa katibu tawala wa mkoa wa Mtwara-Alfred Luanda.


Kikosi cha Ndanda FC kilichoanza katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda magoli 2-1.


Kikosi cha Azam FC kilichoanza katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya NdandaFC katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda magoli 2-1


Kiungo wa Azam FC Jean Mugiraneza akiwania mpira wa juu mbele ya kiungo wa Ndanda Nassoro Kapama katika mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda 2-1.


JUMA MOHAMED, MTWARA.

Ndanda FC leo hii wameiduwaza Azam katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kufunga magoli 2-1
Azam walianza kupata bao la kuongoza katika dakika ya saba likifungwa na Francisco Zekumbawira, kabla ya Omary Mponda kuisawazishia Ndanda dakika ya 41 na baadae Riphat Khamisi kufunga bao la ushindi kwa shuti kali dakika ya 84.

Mshambuliaji wa Ndanda FC, Omary Mponda akijaribu kumtoka mlinzi wa Azam FC David Mwantika ktika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara Nangwanda Sijaona Mtwara. Ndanda walishinda 2-1

 
Manaodha wa timu zote mbili wamezungumza baada ya mchezo huo ambapo Nahodha wa Azam John Bocco anasema wamekubali matokeo na sasa wanajipanga kwa michezo inayofuata, huku nahodha wa Ndanda Kigi Makasy, akiwataka mashabiki kuzidi kuwaunga mkono katika michezo yao.
Huo ni mchezo wa pili kwa Ndanda kupata ushindi, baada ya wiki iliyopita kuwafunga majimaji ushindi kama huo wa mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika mjini Songea.

Katibu tawala wa mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda, akisalimiana na nahodha wa Ndanda FC-Kigi Makasy kabla ya kuanza kwa mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam. Ndanda walishinda 2-1.

 

No comments: