Friday, July 22, 2016

Shule mbili manispaa ya Mtwara Mikindani zatumia choo kimoja.


Wanafunzi wa shule za msingi Maendeleo na Rahaleo wakisubiri zamu ya kuingia Msalani.



Vyoo ambavyo vilikuwa vikitumiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Maendeleo..kwasasa vimefungwa kutokana na kuwa vibovu.


Choo kinachotumiwa na walimu wa shule mbili za msingi, Maendeleo na Rahaleo za manispaa ya Mtwara Mikindani.







Na Juma Mohamed, Mtwara.

Wakati mkoa wa Mtwara ukisimama kifua mbele kutokana na kufanikiwa kumaliza tatizo la madawati kwa shule za msingi na sekondari kwa Zaidi ya asilimia miamoja, bado unakabiliwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya majengo katika shule mbalimbali.
Shule ya msingi Maendeleo iliyopo manispaa ya Mtwara Mikindani, ni miongoni mwa shule zinazokabiliwa na changamoto hiyo kutokana na wanafunzi wake kulazimika kupanga foleni kusubiri zamu ya kuingia chooni kujisaidia hali ambayo inawafanya wapitwe na sehemu ya vipindi vya darasani, kwasababu shule hiyo haina vyoo na kujikuta wanadoea vyoo vya shule ya Rahaleo.
“Tunapata shida ya usafi kwasababu, kama sisi tuliokua huku kule choo kikichafuka kidogo tunalaumiwa sisi kuwa ndio tuliochafua kwasababu kule chooni kunatupiwa makopo kwamfano watoto wa Awali wakitupa makopo tunachukuliwa darasa la Saba kwenda kudeki, kwahiyo huku ndani tunakosa vipindi na mwalimu anakuwa ameshafundisha..” alisema Mashaka Fadhili.

Thabiti Hussein-mwanafunzi wa shule ya msingi Maendeleo, manispaa ya Mtwara Mikindani



Thabiti Hussein, mwanafunzi wa Maendeleo aliiomba serikali kufanya jitihada za kuwajengea vyoo ili waondokane na adha wanayoipata kutokana na kutumia muda wa masomo kufanya usafi vyooni.
Changamoto hiyo haijaishia kwa wanafunzi pekee, bali hata kwa walimu ambao ni Zaidi ya Arobaini kwa shule zote mbili za Rahaleo na Maendeleo, wanalazimika kutumia matundu mawili ya vyoo na kujikuta wanapanga foleni kusubiri zamu.

Choo cha shule ya msingi Maendeleo



“Sisi walimu choo chetu tunatumia matundu mawili wanaume na wanawake, kwahiyo choo kipo lakini tuna ‘share’ na Rahaleo hichohicho kimoja..kwahiyo hua tunapanga foleni kwakweli hata vyoo vya walimu havitoshelezi kwahiyo nilikuwa naomba serikali inaposikia jambo hili itupie macho kwa ujumla kwamba sisi shule ya msingi Maendeleo tunachangamoto nyingi..” alisema Fabiola Haule, mwalimu mkuu wa shule ya Maendeleo.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Maendeleo, manispaa ya Mtwara Mikindani-Fabiola Haule.



Naibu Meya wa manispaa hiyo, Erick Mkapa ambaye ni diwani wa kata ya Rahaleo, alikiri kuwapo kwa changamoto hiyo na kueleza kuwa anafanya juhudi za kuwashirikisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha wanatatua tatizo hilo.
Choo cha shule ya msingi Maendeleo ambayo ilianzishwa mwaka 2007 ilipogawanywa kutoka shule ya Rahaleo, kimefungwa kwa takribani miaka mine sasa kutokana na kutokidhi kwa matumizi ya wanafunzi.

'Toka nije mimi'




No comments: