Sunday, July 24, 2016

Mtwara Tech waibuka vinara mbele ya Ndalichako, maonyesho ya Young Scientists Tanzania.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prf. Joyce Ndalichako akiinua tuzo kwa pamoja na washindi wa kwanza katika maonyesho ya Young Scientists Tanzania mkoa wa Mtwara, wanafunzi kutoka shule ya sekondari ya Mtwara Ufundi.


Ushindi rahaaaaaa


Twapongezana baada ya ushindi


Tuzo zikisubiri washindi katika maonyesho ya Young Scientists Tanzania mkoa wa Mtwara.

Picha ya pamoja washindi wa nafasi mbalimbali katika maonyesho ya Young Scientists Tanzania mkoa wa Mtwara na waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prf. Joyce Ndalichako


Mshindi mwenza katika nafasi ya kwanza katika maonyesho ya Young Scientists Tanzania mkoa wa Mtwara, Jacqueline Munisi kutoka shule ya sekondari ya Mtwara Ufundi. (Mtwara Technical)


Mshindi mwenza katika nafasi ya pili kwenye maonyesho ya Young Scientists Tanzania mkoa wa Mtwara, Diana Sosoka kutoka shule ya sekondari ya Wasichana Mtwara. (Mtwara Girls)



Juma Mohamed, Mtwara

Serikali imewataka wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi na sekondari nchini kujikita zaidi katika kusoma masomo ya Sayansi ili kuliongezea Taifa wataalamu hasa katika kuunga mkono sera ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli inayohitaji kuwa na Tanzania yenye viwanda.
Akizungumza katika kilele cha maonyesho ya Teknolojia na Wanasayansi Vijana kutoka shule mbalimbali za sekondari mkoani Mtwara, waziri wa elimu, sayansi na teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, amesema wizara yake itaongeza fursa nyingi katika masuala ya sayansi na teknolojia kwa kutambua mahitaji yaliyopo.

Mkurugenzi na mwanzilishi mwenza wa maonyesho hayo Dokta Gosbert Kamugisha, amesema vijana hao ambao walitumia muda wa miezi sita kuandaa maonyesho hayo wako tayari kufanya masuala ya sayansi ta teknolojia kwa masilahi ya Taifa, huku washindi wa kwanza na wapili katika maonyesho hayo kutoka shule za Mtwara Ufundi na Mtwara Wasichana wakielezea furaha zao baada ya kutangazwa washindi.
Tazama Video hapa chini >>>



Washindi waliopatikana kupitia maonyesho hayo ambayo yalihusisha shule Arobaini mkoani Mtwara watauwakilisha mkoa huo katika maonyesho yakitaifa yatakayofanyika mwezi huu jijini Dar es Salaam.

No comments: