Saturday, July 9, 2016

Moto wateketeza vyumba 9 vya madarasa Lindi Sekondari.



 


Na Juma Mohamed.

JUMLA ya vyumba Tisa vya madarasa vimeteketea katika shule ya sekondari ya Lindi, kufuatia kuzuka kwa moto mkubwa ulioanza kuwaka majira ya saa Saba za usiku kutokana na hitirafu ya umeme.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi Renata Mzinga, ameiambia Juma News kwa njia ya simu kuwa, mbali na vyumba hivyo, athari zingine zilizotokana na moto huo ni kuteketeza matundu 26 ya vyoo, ofisi 4 za walimu pamoja na vyumba viwili vya maabara za Phizikia na Kemia.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi, Renata Mzinga. (PICHA: MTANDAO)

“Ulianzia kwenye ‘Main switch’..chumba ambacho kina ‘Main Switch’ kwamujibu wa mtoa taarifa za awali ambaye ni mwalimu wa shule hiyo na kwasababu moto huo pale hakuna namna ya kuingiza zima moto yale madarasa ya nyuma miundombinu ilizuia kuingiza gari la zima moto kwahiyo wananchi wakawa wanajitahidi kuuzima kwa kuchota maji hiyo ikapelekea moto kusambaa..”alisema Kamanda.
Aidha, alisema hakuna madhara mengine yoyote yaliyojitokeza dhidi ya binaadam na kwamba bado wanafunzi walikuwa hajaanza kuwasili shuleni hapo kutoka makwao walikokuwa kwa likizo.

No comments: