Friday, July 1, 2016

MBUNGE KENYA KUWAKILISHA NCHI KATIKA MASHINDANO YA OLYMPIC BRAZIL.


Mbunge wa Cherengany, Wesley Korir. (PICHA: MTANDAO)



Na Mack Kemoli, Nairobi.

ALIYEKUWA bingwa wa boston marathon Wesley Korir ambaye ni mbunge wa eneo bunge la Cherengany, magharibi mwa kenya ameteuliwa katika timu ya marathon ya Kenya itakayowakilisha nchi hiyo katika mashindano ya Olympic huko Rio De Janeiro nchini Brazil, baadae mwaka huu.
Akiongea baada ya uteuzi huo, Korir mwenye umri wa miaka 32 alisema,
Lengo lango ni kufanya mazoezi kwa juhudi zangu zote, niombe niwe mzima ili nitwae medali kwenye mashindano hayo”.
Aliongezea kwamba yeye na wenzake watafanya bidii watwae nafasi za kwanza tatu katika mashindano hayo.
nina furaha kuwa mbunge wa kwanza popote duniani kushiriki katika mashindano ya Olympic kama mwanariadha na sio mwana siasa”, aliongeza Korir. Akiongea na waandishi wa habari, Korir alisema,
 “sikuamini ningewakilisha nchi yangu kwenye mashindano ya Rio, lakini licha ya majukumu ya kisiasa, nimeendelea kufanya mazoezi na kushiriki mashindano mbalimbali, nawaahidi ushindi, mimi na wenzangu tutakaowakilisha kenya kwenye  mashindano ya Olympic

Wesley Korir

Wengine watakaowakilisha Kenya kwenye mashindano hayo ya Rio kwa mbio za marathon ni pamoja na bingwa wa marathon duniani msimu huu Eliud Kipchoge ambaye alishinda mashindano ya London marathon mwaka huu  pamoja na Stanley Biwott aliyemaliza katika nafasi ya pili na ambaye pia alikuwa mshindi wa new York marathon mwaka jana.
Katika hatua nyingine,timu ya wanawake kwenye kitengo hicho inajumuisha washindi wa mashindano ya riadha ya Dunia (IAAF) yaliyofanyika Beijing mwaka jana, ambao ni Helah Kiprop, Jemima Sumgong na Visiline Jepkesho .
Waliokosa kupata nafasi katika timu hiyo ni pamoja na bingwa wa dunia wa  mbio za marathon, Dennis Kimetto na mshindi wa tatu wa mbio za marathon za Olympic huko London Wilson Kipsang .
Uteuzi wa timu ya Kenya ya olympic unafanyika katika uwanja Kipchoge Keino mjini eldoret. Uteuzi huo ulianza jana na unaendelea leo huku nafasi zikishindaniwa kwenye vitengo mbalimbali.
Timu hiyo itapiga kambi hapo hapo kabla ya mashindano hayo  ya Rio.
Eneo hilo la Eldoret ni zuri kwani ni ukanda wa juu zaidi na hutoa fursa kwa wanariadaha kujinoa kabla ya mashindano.  Zaidi ya wanariadha 1,000 kutoka nchi mbalimbali wamepiga kambi mjini Eldoret kwa maandalizi hayo.

No comments: