Sunday, July 17, 2016

Majaliwa azitaka halmashauri Mtwara kuwa na benki ya ardhi.


Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza na watendaji wa serikali mkoani Mtwara jana.



Waziri mkuu Kassim Majaliwa akiwapungia mikono makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati akiwasili katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kuzungumza na watendaji wa serikali.


Na Juma Mohamed, Mtwara.

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amewataka wakurugenzi wa halmashauri nchini kuhakikisha wanamaliza migogoro yote iliyopo baina ya wananchi na halmasahuri zao kwa ajili ya kufanikisha maendeleo ya pamoja.
Akizizungumza mkoani Mtwara katika kikao cha pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali jana, alisisitiza kuacha tabia ya kupuuza hoja zinazotolewa na madiwani kuhusu matatizo yaliyopo kwenye kata zao huku akiwataka kuacha tabia ya kushinda ofisini na baadala yake kwenda kusikiliza hoja za wananchi.
“Na tulisema wakurugenzi piteni kwenye maeneo yenu, msikae ofisini, nyie kama watendaji wakuu mjiridhishe kwamba yale yanayozungumzwa na Madiwani kwamba kuna tatizo moja, mbili, tatu nne kweli yapo? Kama lipo je lina ukubwa gani wa tatizo na linatakiwa kupata uharaka wa kiasi gani..kwahyowakurugenzi mnao wajibu mkubwa wa kuhakikisha kwamba migogoro ya wananchi na halmashauri inakwisha..” alisema.
Aidha, alizitaka halmashauri zote mkoani Mtwara kuhakikisha zinakuwa na benki ya ardhi kwa ajili ya kutenga maeneo maalumu kwa shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwekezaji.

Waziri mkuu Kassim Majaliwa akiwapungia mikono makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati akiwasili katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kuzungumza na watendaji wa serikali.



Awali akitoa taarifa ya mkoa, mkuu wa mkoa Mtwara,Halima Dendego alisema kuwa mkoa unaendelea na ukusanyaji wa mapato ya ndani na kwaamba wamefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi Bilioni 16.6 katika halmashauri zote mpaka sasa huku wakitaraji kufikia lengo.
“Lakini kwa halmashauri mapato ya ndani tulipaswa kukusanya Bilioni 20 na mpaka leo tumekusanya Bilioni 16.6 ni sawa na asilimia 82.2 na ninaamini kabisa bado tunaendelea kukusanya na hasa tozo za ardhi ambazo tunatakiwa turudishiwe kutoka wizara.” Alisema Dendego.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wa Mkoa wa Mtwara na mbunge wa Newala mjini, George Mkuchika, alisema kuwa wananchi wa mkoa wa Mtwara ni wapenda maendeleo lakini wanayumbishwa na viongozi wao huku akidai kuwa sababu za mkoa huo kuchelewa kupata maendeleo ni kwasababu ya kupigana vita na Msumbiji mwaka 1964-1974.
“Sisi tulikuwa vitani, kule vita vikichafuka tulikuwa tunalala kwenye maandaki..kwahiyo wakati wenzetu wanajenga sekondari sisi tulikuwa kwenye maandaki tukachelewa, sasa ile mnayosikia Mtwara kuchelemaana yake katika lugha za mkoa huu zote maana yake Mtwara kumekucha..” alisema.
Waziri mkuu alitumia kikao hicho ambacho kilihudhuriwa na baadhi ya wabunge  kuzisisitiza halmashauri kusimamia utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020.


No comments: