Sunday, December 6, 2015

Mkapa awataka wananchi wa Kusini kujikita katika elimu.




Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamn William Mkapa, akihutubia katika Mahafali ya Nne ya Chuo kikuu Kishiriki cha Stella Maris Mtwara, yaliyofanyika jana chuoni hapo. Jumla ya wanafunzi 524 wamehitimu




Baadhi ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Stella Maris Mtwara, wakiwa katika sherehe ya Mahafali ya Nne ya chuo hicho yaliyofanyika jana mkoani Mtwara na kuhudhuriwa na Rais mstahafu wa awamu ya tatu Mhe. Benjamin William Mkapa



Na Juma Mohamed, Mtwara.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa, amewataka wazazi wa mikoa ya Kusini kutoa msukumo kwa watoto wao waweze kujali umuhimu wa elimu, ili wanufaike na uwekezaji unaoendelea katika mikoa hiyo unaotokana na rasilimali za gesi na mafuta.
Akizungumza mkoani hapa katika Mahafali ya Nne ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Maris, Mtwara, alisema kumekuwa na msukumo mdogo sana kwa wazazi katika kusisitiza umuhimu wa elimu kwa vijana wa mikoa hiyo, jambo amabalo linapelekea kuwa na uhaba wa vijana wanaopta elimu ya juu katika vyuo vilivyopo
Alisema, chuo cha Stella Maris kina uwezo wa kupokea wanafunzi 3,000 lakini wanafunzi wanaojiunga hawafikii idadi hiyo, na kwamba hiyo ni changamoto kwa wazazi.

Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin W. Mkapa

“Nafahamu kuwa zilikuwepo changamoto nyingi kwenye mikoa yetu ya Kusini. Lakini nyingi ya hizi changamoto zimebaki ni historia..ni vema sasa tukajiandaa vema kitaaluma ili tuweze kunufaika na uchumi wa gesi ambao unatujia kwenye kanda hii, bila elimu bora tutabaki kuwa waangaliaji tu huku wengine wakija kunufaika na rasilimali hizi hapa nyumbani kwetu..” alisema.
Alisema, anasikitishwa na takwimu za matokeo ya mitihani kwa shule za sekondari za miaka ya karibuni kwa mikoa ya Kusini na pwani, kutokana na shule kutofanya vizuri kwenye mitihani yao na kuhathiri hata udahili wa wanafunzi katika taasisi mbalimbalii ikiwa ni pamoja na Stella Maris.
“Nikiwa mzaliwa wa Kusini, nimekuwa nikisikitishwa sana na hali ya elimu kwenye eneo hili hususani uchache wa shule na taasisi nyingine za elimu kama hizi..juhudi kadhaa zimefanywa na serikali za awamu zote katika kujaribu kutatua tatizo hili, lakini sekta binafsi na wadau mbalimbali wa elimu kama Kanisa Katoliki wametoa mchango mkubwa sana kwenye kusaidia kutatua tatizo la mgawanyiko sawia wa taasisi za elimu kwenye kanda mbalimbali.” Aliongeza.

Wahitimu

Awali, mkuu wa chuo hicho, Slaus Mwisomba, aliwasihi wahitimu hao ambao jumla yao ni 514, kwenda kutumia vizuri taaluma zao walizopata katika kipindi chote walichokuwa chuoni hapo ili jamii iweze kunufaika nao na kwamba waachane na hanasa mbalimbali ambazo zinaweza kuwachafua na kuwashushia hadhi yao kama wasomi wa elimu ya juu.
Aidha, alieleza changamoto ambazo chuo inakabiliana nazo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maabara kwa ajili ya masomo ya Sayansi ambayo ni Phizikia, Kemia na Baiolojia.
“Stemmuco inalengo la kuanzisha Maabala ya Sayansi hali inayoweza kwa chuo kutoa fursa ya kudahili wanafunzi wa masomo ya Sayansi...hii itaongeza nguvukazi, itaongeza utaalamu na mambo mengine kwa kujua hapa tulipo kuna rasilimali gani amabzo zinahitaji sayansi kwa ajili ya kuendelezwa..” alisema.
Kwa upande wao, baadhi ya wahitimu, walieleza kufurahishwa na hotuba ya Mhe. Mkapa hasa aliposisitiza juu ya wao kwenda kukabiliana na hali ya kimaisha huko waendako na kuto kata tama pale wanapoona wanakosa fursa za ajira na kwamba wajaribu kutumia elimu zao kwa kutafuta namna ya kujiajiri ili waweze kufanikiwa, na kusema kuwa wameipokea hotuba hiyo kama chachu ya wao kwenda kufanikiwa kimaisha.
Gladness Paul, ambaye amepata elimu ya biashara, alisema atatumia elimu hiyo kwa kufanya shughuli mbalimbali za ujasiliamli ambazo anaamini jamii kwa kiasi kikubwa itanufaika na elimu yake kupitia shughuli hizo.




No comments: