Na Juma
Mohamed-Mtwara.
JUMLA ya
Tani 4,000 za korosho zimekusanywa na Chama Kikuu cha Ushirika cha MAMCU kutoka
kwa wanunuzi holela wa zao hilo (Kangomba), kufuatia jitihada zinazofanywa na
Bodi ya Korosho Tanzania za kudhibiti ununuzi huo katika maeneo mbalimbali
yanayolima korosho.
Akizungumza mkoani hapa, kaimu meneja mkuu wa chama hicho, Kalvin Rajabu, alisema, kumekuwa
na jitihada za dhati zinazofanywa na bodi kuhakikisha wanatokomeza ulanguzi huo
ambao umekithiri katika maeneo ya vijijini na kwamba jitihada hizo zinaonesha
kufanikiwa.
“Pale katikati
kulikuwa na changamoto, vyama vya msingi vilikuwa vinakosa korosho kutokana na
wanunuzi hawa holela, lakini tunashukuru jitihada zilizofanywa na bodi ya
korosho wameza kusimamia na kuhakikisha wale waliokuwa wakinunua kwa Kangomba
wanawadhibiti na korosho kurudishwa kwenye vyama vya msingi..kwahiyo ukija
kuangalia wastani wa Tani 4,000 tumeweza kuzipata baada ya bodi ya korosho
kufanya kazi yao vizuri..” alisema.
Alisema,
hali ya mauzo kwanzia mwezi septemba ulivyozinduliwa na bodi, inaenda vizuri na
kwamba mpaka kufikia Novemba 27 mwaka huu chama hicho tayari kimeshafanya
minada saba ambapo jumla ya Tani 30,588 ziliingizwa sokoni na kuuzwa.
Aidha,
alisema, chama kilifanikiwa kusambaza fedha katika halmashauri za Mtwara
manispaa, Mtwara vijijini, Masasi, Masasi mjini na Nanyumbu kiasi cha zaidi ya
sh. Bilioni 99 ambazo anaamini zimeshawafikia wakulima kutokana na mauzo ya korosho
zao.
Alisema,
halmashauri za wilaya za Mtwara manispaa na Nanyamba zilisambazwa jumla ya sh.
Bilioni 12.9, wakati upande wa halmashauri ya Masasi ni bilioni 23.5 huku
Masasi mjini wakipatiwa kiasi cha bilioni 2 na bilioni 10.5 zikienda katika halmashauri
ya Nanyumbu.
“Hali ya
biashara katika minada mbalimbali ilikua nzuri, tulianza na bei ya sh. 2,407
mpaka kufikia bei ya sh. 2,700..hali imeonekana sio mbaya sana kwamba soko
linakua na mwelekeo nzuri, lakini mpaka kufikia mnada wa mwisho, jumla ya
makusanyo katika maeneo yote ya MAMCU ambao tunafanya kazi katika wilaya tatu
za Mtwara, Masasi na Nanyumbu, jumla ya tani 33,933 tumeweza kukusanya na
kuuza.” Aliongeza.
No comments:
Post a Comment