Monday, May 23, 2016

Yanga watavuna kiasi hiki cha fedha iwapo watatwaa ubingwa wa Shirikisho..

 

Yanga imekuwa na mafanikio makubwa chini ya Hans van der Pluijm baada ya kutwaa taji la Ligi Kuu na kutinga hatua ya makundi lakini ili isonge ni sharti ivuke vikwazo vyote

Bingwa wa kombe la shirikisho Afrika anavuna dola 625,000(billion 1.3), mshindi wa pili dola 432,000 (milioni 907.2), mshindi wa tau dola 239,000(milioni 501.9) na mshindi wa mwisho anapata dola 150,000(milioni 315)

Mwaka 1998 Yanga walifuzu hatua ya nane bora chini ya Tito Mwavalunda aliyekuwa kocha kipindi hicho akishirikiana na Felix minziro. Baada ya miaka takribani 18 Yanga inafuzu hatua ya nane bora chini ya Mholanzi Hans Van Pluijim.

Yanga wamefanikiwa kuiondoa Sagrada Esperanca ya Angola kwa jumla ya magoli mawili kwa moja, baada ya awali kushinda Tanzania kwa magoli mawili kwa sifuri na kwenda kufungwa moja bila na Waangola hao.

Wiki hii ratiba ya makundi itapangwa kwa timu 8 zilizosalia ambazo ni TP Mazembe (Congo) , Etoile du Dahel (Tunisia) , Mo Bejaia (Algeria) , Kawkab Marrakech (Morocco) , Ahli Tripoli (Libya) ,  Medeame (Ghana) ,na Yanga yenyewe.

Goal inakuletea baadhi ya timu zitazokuwa kikwazo kwa Yanga endapo watapangwa kundi moja

TP Mazembe

Mabingwa wa mara 5 wa klabu bingwa Afrika (1967,1968, 2009, 2010, 2015) inamilikiwa na tajiri wa Congo Moise Katumbi, licha ya kutoanza vizuri msimu huu na kupelekea kutolewa kwenye klabu bingwa, bado TP Mazembe inasimama kama moja ya timu bora Afrika, aina ya wachezaji wao wenye uzoefu kwenye michuano mikubwa na uwekezaji mkubwa, inaweza kuwa kikwazo kwa Yanga kama wakiwa kundi moja, haitakuwa rahisi kwa Yanga kupata matokeo kirahisi kwa Tp Mazembe.

Mo Bejaia

Timu kutoka Algeria, iliyoanzishwa mwaka 1954, haina rekodi  kubwa katika michuano ya Afrika, lakini si timu ya kubeza sana sababu wamefanikiwa kuiondoa moja ya timu bora Afrika, Esperanca ya Tunisia, baada ya mechi ya kwanza kutoka bila bila na marudiano kule Tunisia mchezo kuisha kwa goli moja moja hivyo Mo Bejaia kufuzu kwa goli la ugenini, kutokana na ubora wa nchi ya Algeria katika soka Mo Bejaia itakuwa moja ya timu itakayo leta upinzani mkubwa katika hatua hio ya makundi.

Fus Rabat

Mabingwa wa zamani wa kombe la shirikisho mwaka 2010, Fus Rabat kutoka Morocco, imefanikiwa kuingia hatua ya makundi baada ya kuiondoa Stade Maliene ya Mali kwa idadi ya magoli 4 kwa bila, moja ya timu bora kati ya timu zilizomo kwenye 8 bora shirikisho, wanashika nafasi ya pili kwenye ligi kuu nchini Morocco ambayo ni miongoni mwa ligi bora za Afrika, Fus Rabat ,Yanga haina budi kuzihofu changamoto za klabu hii ya Morocco sababu ya uwekezaji wao waliofanya katika klabu kwa nia ya kufanya vizuri Afrika.

Etoile Du Sahel

Huyu ndo bingwa mtetezi wa kombe la shirikisho, kutokana na Yanga kutokuwa na matokeo mazuri kwa timu za kiarabu, kwa miaka ya hivi karibuni si timu sahihi ya kuiombea kupangwa nayo kundi moja, aina ya wachezaji wenye uzoefu wa michuano mikubwa, ukubwa wa la benchi la ufundi na ubora wa ligi yao, ambao wanongoza ligi mpaka sasa, Etoile itakuwa kikwazo kwa Yanga kama wakitupwa kundi moja, itakuwa ngumu kupata matokeo ugenini kwa Yanga endapo watapangwa katika kundi moja.

CHANZO: GOAL

No comments: