![]() |
Wilbert Mweta, akiwa na baadhi ya wachezaji wenzake wa Ndanda Fc katika moja ya michezo ya Ligi kuu msimu uliopita. |
![]() |
Wilbert Mweta, (mwenye fulana jeupe) katika bonanza la michezo siku ya uzinduzi wa Taasisi yake ya Mweta Sports Center ya jijini Mwanza. |
Na Juma
Mohamed.
NAODHA wa
timu ya soka ya Ndanda Fc ya mkoani Mtwara na mkurugenzi wa Taasisi ya michezo ya Mweta Sports Center ya jijini Mwanza, Wilbert Mweta, amesema ili Tanzania
ifanikiwe katika soka ni lazima kuwe na mipango thabiti katika kukuza vipaji
vya vijana.
Alisema,
Watanzania wamekuwa watu wakupenda kuona mafanikio siku zote bila kuwa na
mipango kwanzia ngazi za chini kwa ajili ya kuandaa mikakati ya kufikia
mafanikio, jambo ambalo linakwamisha hasa timu ya Taifa ambayo mara nyingi
imekuwa ikishiriki michuano mbalimbali ya Kimataifa bila mafanikio yoyote.
Alisema,
iwapo wachezaji wengine wa Tanzania watakuwa na malengo kama yakwake ya kuamua
kuanzisha vituo vya michezo kwa ajili ya kukuza soka la vijana, basi utakuwa ni
mchango mkubwa kwa Taifa na kwao wenyewe kwasababu itakuwa ni fursa nyingine ya
kujiajiri.
![]() |
Nembo ya Kituo cha Michezo cha Mweta Sports Center (MSC) kinachomilikiwa na Nahodha wa timu ya soka ya Ndanda Fc, Wilbert Mweta, cha jijini Mwanza. |
Mweta ambaye
kituo chake kilipata usajili rasmi mwezi January mwaka huu na kuwa na jumla ya
vijana 86 wenye umri kuanzia U-17 ambao wapo 36, U-14 walio 24 na U-12 ambao
wapo 26, alisema iwapo atapata nafasi ya kukutana na Rais wa Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, atakuwa na mambo manne ya kumshauri.
Jambo la
kwanza alisema ni kuja na mpango wa muda mrefu wa kuwaandaa vijana ambao baada
ya miaka mitano hadi kumi watalifanya Taifa kuwa na timu imara yenye kuweza
kushindana katika mashindano makubwa.
“Mambo
mengine ambayo nitamshauri Rias Jamal Malinzi ni kwamba waamuzi wa mpira wafanye
kazi yao, wachezaji tufanye kazi yetu na vyama husika vya mpira ngazi zote
kwanzia chini mpaka juu vifanye kazi zao kama kanuni na sheria zinavyosema na
mwisho wa siku tutapata bingwa ambaye ni bingwa kweli..” alisema.
Kuhusu kuchezea
timu ya Taifa, alisema kwasasa hafikirii kabisa suala hilo na hana ndoto hizo
kwasababu anaamini kuwa Watanzania bado wanahitaji ushindani na kwenda katika
michuano mikubwa kama Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) huku jitihada
zilizoonyeshwa na wachezaji waliopo kwasasa zinaonekana kutofanikia na hata
yeye anaona kiwango chake hakina tofauti na wachezaji waliopo katika timu hiyo,
hivyo kuwepo kwake hakutoongeza kitu.
![]() |
Wilbert Mweta akiwa mazoezini kujiandaa na moja ya michezo ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara |
“Nikiitwa
timu ya Taifa nitauliza maswali mawili kwamba wameniita kwasababu gani, kwenda
kucheza mpira nadhani jibu la kwanza litakuwa ni hilo..sasa nitauliza kwamba
nakwenda kushindana au nakwenda kushiriki, wakiniambia kwenda kushiriki
nitakwenda lakini kama kwenda kushindana sitoweza kwenda..” alisema Mweta
ambaye wiki mbili zilizopita aliandaa bonanza lililohusisha wachezaji wenzake
wanaocheza Ligi Kuu na kuambatana na uzinduzi wa kituo chake cha michezo.
Alisema,
katika bonanza hilo lililohudhuriwa na baadhi ya wachezaji hao waliweza
kuungana na kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya polisi na watu walijitokeza
kwenda kuwashuhudia huku wakichangia kiingilio ambacho baadaye kilisaidia kutunisha
mfuko wa kituo hicho ambacho bado kichanga na kimeweza kuajiri watu kadhaa
ambao wanafanikisha maendeleo ya vijana.
![]() |
Wilbert Mweta, (mwenye fulana jeupe) katika bonanza la michezo siku ya uzinduzi wa Taasisi yake ya Mweta Sports Center ya jijini Mwanza. |
“Nawashukuru
wale waliokuja kuhudhuria, ila wale walioshindwa naamini ni kutokana na sababu
mbalimbali za kiuchumi na umbali waliokuwepo, lakini waliokuja tulicheza
bonanza lile na vijana walicheza na sisi tulicheza mechi yetu na timu ya polisi
na tulipata kiingilio pale ‘getini’..pesa iliyopatikana tuliweza kununua vifaa
vya michezo, kwahiyo walichangia kwa nanma moja au nyingine, napenda wawe na
moyo wa aina hiyo nikiwahitaji waje watoe ‘sapoti’ kituo sio cha Mweta bali ni
cha Watanzania wote pengine itafika siku hata watoto wao watakuja pale
tukawalea..” alisema.
Mweta
alisema, kabla ya kuwa na kituo hicho, alikuwa anaendesha Klabu ambayo ilikuwa
na wachezaji kadhaa ambayo alianza nayo toka mwaka 2013 lakini baadaye mawazo
yake yakapanuka zaidi na kuamua kuanzisha kituo hicho ambacho kimepata usajili
wake mwezi Januari mwaka huu.
![]() |
Moja ya vikosi vinavyozalishwa katika kituo cha Mweta Sports Center (MSC) cha jijini Mwanza kinachomilikiwa na Golikipa na Nahodha wa timu ya soka ya Ndanda Fc ya mkoani Mtwara, Wilbert Mweta. |
Alisema,
katika Klabu hiyo, kulikuwa na wachezaji watano ambao walifanikiwa kusajiliwa
katika timu za Kurugenzi ya Iringa inayoshiriki ligi ya Daraja la Kwanza ambao
walisajili vijana wawili, huku wengine wakielekea kusajiliwa na timu ya
Bulyanhulu Fc.
Alisema,
Taaisi yake kwasasa inauongozi ambao unaaminika kiasi cha kumfanya asipatwe na
wasiwasi wowote kwa kipindi ambacho anakuwa mbali nacho kwasababu ameajiri watu
katika idara kadhaa ikiwa ni pamoja na Meneja Mkuu, Meneja Masoko, katibu pamoja
walimu watatu ambao wanashirikiana kuhakikisha mambo yanaenda sawa.
Katika watumishi
aliyonao, wapo ambao amewaajiri kabisa na wapo ambao wanajitolea kwa moyo wa
dhati, na kwamba wale walioajiriwa ni jukumu lake mwenyewe kuweza kuhakikisha
anawalipa huku akisema mpaka sasa bado hajaanza kuingiza faida ya kipato
kutokana na Taasisi hiyo na kumfanya atumie ghalama zake zaidi kuweza kuiendesha.
Alisema,
wapo baadhi ya wadau ambao wameonesha nia ya kutaka kumsaidia katika baadhi ya
maeneo katika taasisi yake, huku akitoa wito kwa wadau wengine wa soka na
wapenda maendeleo kwa ujumla kuweza kufika kituoni hapo kuona kile
kinachofanyika na hatimae waweze kushawishika kwa kumuunga mkono jitihada zake
kwa kumfadhili ili kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu hapa nchini.
Lengo lake
ni kuwa miongoni mwa wanamichezo wanaomiliki vituo bora vya michezo barani
Afrika hapo baadaye, ili kutoa mianya kwa wanamichezo wengine kuweza kufanya
kama yeye na kulitoa Taifa hapa lilipo na kulisogeza katika hatua nyingine
zaidi kimichezo.
No comments:
Post a Comment