Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Mtwara vijijini, Tamimu Kambona. |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
KUFUATIA
baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kutoa taarifa za uchakavu na uhaba wa
nyuma za walimu katika shule za msingi za Mkubiru na Msangamkuu katika halmashauri
ya wilaya ya Mtwara vijijini, kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Tamimu
Kambona, amekuja juu na kuwataka waandishi wa habari kuacha kufanya kazi na
halmashauri hiyo.
Akizungumza
katika sherehe za kumuaga mwalimu mstaafu wa shule ya msingi Mkubiru, Ally
Mpomo, zilizofanyika shuleni hapo, Kambona alisema kitendo hicho kilichofanywa
na waandishi wa habari ni “Ujinga na Ulofa,” akinukuu maneno ya Rais mstaafu wa
awamu ya tatu Mhe. Benjamin W. Mkapa aliyoyasema wakati wa uzinduzi wa kampeni
za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Salaam.
Alisema,
waandishi wa habari wamekuwa mstari wa mbele zaidi kuandika mabaya yanayotokea
kuliko mazuri yanayofanywa, huku akikiri kuwa yale mabaya yanayoandikwa ni kero
kwa wahusika hivyo yanahitaji kupatiwa msaada kwa kuyatatua.
“Lakini
tatizo tu la nyumba ya mwalimu kuwa mbovu ndio walioliona wao lakuongea,
nawaomba waandishi wa habari, kama mtapenda kuandika habari zetu andikeni, kama
msipopenda hachaneni na sisi..lakini lazima eti kwasababu amesema tutumbue
majipu, mimi nasema na ninasema hili waandishi wa habari kote waliko kuanzia
wale wa Chanel Ten na wengine waliokuwa wanapenda kuongea hayo, ukipenda
kuongea mabaya kumuka na yale mazuri tunayoyafanya kwanini baya letu moja mulizungumze
lakini mema yetu elfu mbili hamzungumzi?..” alihoji Kambona ambaye pia ni afisa
elimu ya Msingi katika halmashauri hiyo.
Kaimu mwalimu mkuu wa shule ya msingi Msangamkuu, Zaitun Mkamumba, akiwa mbele ya moja ya nyumba za walimu zilizopo katika shule yake. |
Alisema,
taarifa hizo zilirushwa kwenye vyombo vya habari mbalimbali karibu wiki nzima
kwa mfululizo na kwamba alipigiwa simu na kuambiwa aangalie chaneli moja mabayo
ilikuwa ikirusha taarifa hiyo.
“Nawaambia
waandishi wa habari mliokuwepo hapa na wasiokuwepo mkawaambie, na ikiwezekana
mimi sitokuwa tayari kutoa ushirikiano na wao kama wataendelea na tabia
hii..naomba niishie hapo, lakini itakuwa vibaya au ni vizuri nikisema kama
alivyosema Rais wa awamu ya tatu alivyosema mzee Benjamin William Mkapa, wakati
wa uzinduzi wa kampeni, ni ujinga naa....mshamalizia..” aliongeza.
Wiki mbili
zilizopita, walimu wa shule hiyo walipaza sauti zao kulalamikia ugumu wa maisha
wanaoupata kutokana na kushindwa kumudu gharama za maisha ambazo haziendani na
kipato wanachokipata kwa mwezi, na kujikuta wanakabiliwa na madeni.
Wakizungumza
na Nipashe, walisema kuna mambo mengi ambayo yamekuwa ni changamoto katika
mazingira yao ya kazi, ikiwa ni pamoja na miundombinu mibovu katika shule yao
kiasi cha kuzidi kuyafanya maisha yao kuwa magumu.
Moja ya
changamoto ambazo walizieleza ni kukosekana kwa nyumba za walimu shuleni hapo
na kusababisha walimu wengi kuishi maeneo ya kijijini ambako wanalazimika
kupanga na kulipa kodi kila mwezi huku wakikabiliwa na changamoto nyingine ya
usafiri wa kutoka huko wanakoishi mpaka kufika shuleni kiasi cha kulazimika
kutumia pesa kwa ajili ya nauli ya pikipiki za kubeba abiria (Bodaboda).
“Hali ya
mshahara na maisha yalivyopanda haviendani, na hii ndio maana inasababisha
baadhi ya walimu kujihusisha na biashara labda zingewza kuwakwamua..mshahara
nalipwa sh. 350,000 na matumizi yangu kwa mwezi yanafika sh. 520,000, kwahiyo mwisho
wa mwezi najikuta nakabiliwa na madeni sana mpaka inafikia wakati tunagombana
na wenye nyumba maana kama majengo unavyoyaona hakuna nyumba za waalimu sisi
tuliokuwa wengi tunaishi mitaani kwa kupanga..” alisema mwalimu mmoja ambaye
jina lake limehifadhiwa.
Alisema,
kuna mahitaji ambayo analazimika kuyapata kila siku na yanahitaji pesa ikiwa ni
pamoja na kununua samaki wanaopatikana kwa sh. 5,000 ambao ndio mboga kubwa
kutokana na kijiji hicho kuwa katika mazingira karibu na bahari na mchele ambao
wananunua sh. 2,200.
“Mahitaji
mengine ambayo nalazimika kutumia pesa kila siku ni vocha kwa ajili ya
mawasiliano (Hakutaja anatumia kiasi gani) pamoja na viungo kama nyanya,
vitunguu na vingine, kwasababu samaki siwezi kupika bila viungo..” aliongeza.
Alisema,
kutokana na kubanwa katika majukumu yao ya kufundisha, wanajikuta wanakosa hata
muda wa kufanya shughuli nyingine ambazo labda zingeweza kuwapatia kipato
mbadala tofauti na mshahara wao, huku akisema kuwa mpaka sasa anakabiliwa na
deni la sh. 126,000.
Moja ya nyumba za walimu katika shule ya msingi Mkubiru, halmashauri ya Mtwara vijijini ambayo hata hivyo mwalimu aliyekuwa akiishi amehamishwa kutokana na kuhofia usalama wake kutokana na ubovu wa nyumba. |
Kwa upande
wake, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Hazzam Nambunga, alikiri kukumbwa na
changamoto hizo na kusema kuwa nyumba za walimu zilizopo ni mbili ambazo moja
anaishi mwalimu mkuu na nyingine anaishi mwalimu mwingine mmoja.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mkubiru, halmashauri ya Mtwara vijijini, Hazam Nambunga, akielezea changamoto alizonazo shuleni kwake. |
Aidha,
alisema, shule hiyo nakabiliwa pia ukosefu wa ofisi ya waalimu ambapo ambayo
ilikuwa ikitumika jingo lake lipo katika hali mbaya na halifai kutumika tena
kiasi cha kulazimika kutumia darasa moja kama ofisi ya waalimu na kwamba
wanafunzi wa darasa la awali ambao walikuwa wakisomea katika chumba hicho
kusomea chini ya miti.
“Tunamwomba
Mhe. Rais wa awamu ya tano, pamoja na mambo mengine, aangalie sana na kuboresha
masilahi ya walimu zaidi kuboresha miundombinu kwa kutujengea nyumba bora za
walimu” alisema.
No comments:
Post a Comment