Vijana kutoka vyuo mbalimbali mkoani Mtwara walioudhuria semina ya siku moja ya kuwajengea uwezo juu ya masuala ya uwekezaji katika sekta ya rasilimali za Mafuta na Gesi yanayoendelea mkoani hapa. |
Vijana wakifuatilia somo kutoka kwa mwezeshaji Justin Lusasi, Mhadhiri wa chuo cha Stella Maris-Mtwara |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
ZAIDI ya vijana
30 kutoka katika vyuo mbalimbali mkoani hapa wamepatiwa elimu juu ya masuala ya
uwekeza katika rasilimali za Mafuta na Gesi asilia, katika semina ya siku moja
iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la MRENGO kwa lengo la kuwajengea
uwezo wa uelewa katika masuala mbalimbali yanayohusu sekta hiyo.
Wakizungumza
mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo, baadhi ya wanafunzi hao walisema
imewasaidia kuweza kufahamu mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na namna rasilimali
hizo zitakavyoanza kuwanufaisha wananchi ambao wengi wao wanatarajia kuona
mafanikio kwa siku za karibuni.
Mshamu Nayopa,
muhitimu wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) tawi la Mtwara, alisema awali
alikuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitarajia kuona faida ya rasilimali
hizo zikianza kuonekana mapema, lakini baada ya kupata elimu kupitia semina
hiyo amepata ufahamu kuwa itachukua muda mrefu mpaka wananchi kuanza kuziona
faida zake.
“Mtaani
kulikua na mitazamo mingi kwa vijana, lakini baada ya kuja kupata mafunzo
tumegundua mambo yapo tofauti sana, vijana wengi wanatarajia mambo mengi sana
wanavyosikia ‘Issue’ ya gesi, kwamba gesi itawezesha maisha yao na kufanya kila
kitu, kitu ambacho sidhani kama ni kweli..kwamujibu wa elimu ambayo tumeipata
hapa ni sawa gesi italeta mafanikio kwa wananchi lakini itachukua muda mrefu
sana tofauti na watu wanavyotarajia..” alisema.
Aliwataka vijana
ambao wako mitaani, kuacha kuishi kwa kutojishughulisha na kutegemea gesi
itawasaidia kwasasa, na baadala yake wajishughulishe na mambo mbalimbali ambayo
yatawawezesha kupiga hatua kimaisha.
Kwa upande
wake, mratibu wa mradi wa Mafuta na Gesi unaotekelezwa na shirika hilo kwa
kufadhiliwa na shirika la Utunzaji wa Mazingira Duniani (WWF), Mustafa
Kwiyunga, alisema lengo la kuwajengea uwezo vijana hao ni kutaka kuendeleza
majadiliano mbalimbali hasa katika vyuo na pia waende kuwa mabalozi wazuri wa
kutoa elimu juu ya rasilimali hizo kwa wananchi.
Vijana wakifuatilia somo kutoka kwa mwezeshaji Justin Lusasi, Mhadhiri wa chuo cha Stella Maris-Mtwara |
“Wamalizapo
wawe mabalozi wazuri kule chini kuwza kuwaelimisha wananchi waweze kuwahamasisha
watoto wao kupenda masomo ya sayansi ili waweze kupata ajira katika maeneo ya
uchimbaji wa mafuta na gesi..lakini pia jukwaa hili tunalitengeneza kwa ajili
ya kwenda kukutana katika vyuo na pia tutakua na ratiba ya kukutana kila baada
ya miezi mitatu ili kujua kinachoendelea na kupashana habari mbalimbali kuhusu
mafuta na gesi..” alisema.
Naye,
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Maris (STEMMUCO) mkoani Mtwara,
Justin Lusasi, aliwataka wazizi na walezi kuhamasika katika kuwapeleka shule
watoto wao kwa ajili kuwatengenezea misingi bora ya maisha ambayo wataipata
kupitia rasilimali hizo, na waache kupoteza muda katika masuala ya Jando na
Unyago.
No comments:
Post a Comment