![]() |
Bi Modesta Makaidi, akiwa na aliyekuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Dekrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiungwa mkono na UKAWA, Mhe, Edwatd Lowassa. wakati wa moja ya mkutano wa kampeni wilayani Masasi.(PICHA-MTANDAO) |
Na Juma
Mohamed.
Mgombea
Ubunge wa chama cha National League for Democracy (NLD) katika jimbo la
Lulindi, wilayani Masasi, mkoani hapa, Modesta Makaidi, amewataka makada wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutorudia vitendo vya kugawa kanga na unga kwa
wananchi ili kuwashawishi kumchagua mgombea wao katika uchaguzi ujao jimboni
humo.
Akizungumza
na wilayani humo, amesema siku moja kabla ya kupiga kura katika uchaguzi wa
ubunge ambao bado haujapangwa, atapita kila kijiji kwa ajiji ili kuwabaini
watakofanya hivyo ambao ameahidi kuwashushia kipigo kwa kutumia vijana wake.
Alisema,
makada hao walifanya hivyo awali katika kipindi cha kampeni kabla ya tume
kuahirisha uchaguzi wa ubunge katika jimbo hilo kutokana na dosari katika
karatasi ya mgombea mmoja, na kwamba alishindwa kuwachukulia hatua kutokana na
kukubwa na msiba wa mume wake, Dkt. Emmanuel Makaidi, ambaye alikuwa mwenyekiti
mwenza wa vyama vinavyounda UKAWA.
Modesta Makaidi (PICHA-MTANDAO) |
“Siku moja
kabla ya kupiga kura nitapita kila kijiji..sisi hatutakua na uwezo wa
kuwakamata na kuwapeleka TAKUKURU (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa)
katikati tutashindwa, nitaalika vijana ‘wakung’utwe’ wote wanaopokea na
wanaotoa, kwasababu CCM haitaki amani na haitaki kuingia madarakani kwa mapenzi
ya wananchi.” Alisema.
Aliongeza
kuwa, wananchi wa jimboni humo wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha na kipato
chao ni hali ya chini, hivyo ni rahisi kurubuniwa kwa kupewa hongo ili
kuwabadilisha kisiasa.
Aidha, aliitaka
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutangaza mapema tarehe rasmi ya kufanyika
uchaguzi huo ili wananchi ambao ndio wapiga kura waweze kujiandaa na kupanga
vizuri ratiba zao kutokana na wengi wao kuwa na majukumu mengine hasa ya
kilimo.
Alisema,
awali wananchi walitangaziwa kuwa wangepiga kura Oktoba 28 lakini ilishindikana
na kwamba msimamizi alilazimika kutangaza tarehe hiyo ili kutuliza morali ya
wananchi ambao walikuwa na kiu ya kutaka kupiga kura ya kuchagua wabunge wao.
“wananchi
wametaharuki, waliambiwa tarehe 28 na wasimamizi na wasimamizi walisema vile
kwa kutaka kujinusuru na wasinge sema vile wangefanyiwa vurugu siku ile..sasa
wanataka tarehe maalumu ili wajiandae kwasababu sasaivi ni kipindi cha kulima
watu wako mashambani..” aliongeza.
Alimtaka msimamizi
wa uchaguzi kutenda haki kwa kumtangaza mgombea atakeshinda kihalali baada ya
uchaguzi, ili kuhepusha shari kwasababu wananchi watamjua mshindi kupitia
matokeo yakayobandikwa katika vituo vyao vya kupigia kura.
No comments:
Post a Comment