Na Juma
Mohamed, Mtwara.
SERIKALI
imetakiwa kuungalia kwa jicho la huruma mkoa wa Mtwara ili kuhakikisha unapiga
hatua kimichezo kutokana na uhaba wa wachezaji wanaowakilisha mkoa katika timu
za taifa.
Wito huo ulitolewa
wiki iliyopita mkoni hapa na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC),
Filbert Bayi, alipozungumza na NEWS ROOM baada ya kumalizika kwa kozi ya utawala
wa kimichezo kwa walimu na viongozi wa michezo wa wilaya za Tandahimba, Mtwara
vijijini na Mtwara manispaa.
Alisema mkoa
huo unamchango mkubwa sana katika michezo hapa nchini hasa katika mchezo wa
mpira wa miguu, kutokana na kuwa na wanamichezo mahiri miaka ya nyuma ambao
walikua ni tegemeo kubwa kwa taifa.
“Kuna akina
mzee Chuma, Mahadhi wote wametokea hapahapa..vijana wa karibuni kama akina
Mmachinga (Mohamed Husein) wote hao, mi nafikiri mkoa wa Mtwara viongozi wa
serikali wauangalie kwa jicho la huruma kuweza kurudisha michezo, mkoa huu una
dhamana sana kwa michezo na tuna wanamichezo wengi tub ado tuwafuatilie.”
Alisema Bayi.
Aidha,
alisema mafunzo waliyoyatoa kwa muda wa siku nne yatakuwa na msaada mkubwa sana
kwa walimu na viongozi wa michezo wa wilaya na mkoa kwasababu wao ndio
wameshika mpini wa michezo katika mkoa.
Alisema moja
ya mambo waliofundishwa ni namna ya kutengeneza mikataba ya vyama vyao ambalo
ni jambo muhimu sana kwa chama chochote cha michezo, kwa lengo la kuepuka
kuendesha chama kiholela na kuyumbisha kanuni za mchezo husika.
Kwa upande
wake, Idefonce Amlima, ambaye ni mmoja kati ya waliohudhuria kozi hiyo alisema
imemsaidia kumpanua kimawazo na kumjenga katika kazi yake ya uwalimu wa mpira
wa miguu, ambapo anatarajia kuwafikishia wanafunzi wake kile alichokipata
kutoka kwa wakufunzi wa kozi hiyo kutoka TOC.
…………………MWISHO…………………
No comments:
Post a Comment