Na Juma
Mohamed, Mtwara.
WAZIRI wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Mhe. Willium Lukuvi amesisitiza juu ya kulipwa fidia kwa
wananchi wanaotoa ardhi zao na kusema kuwa hayupo tayari kuona serikali ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiadhibiwa na wananchi ambao hawalipwi fidia zao
stahiki baada ya kuchukuliwa maeneo yao wanayomiliki kihalali.
Aliyasema hayo wiki iliyopita mkoani hapa na kuongeza kuwa
hayupo tayari kuona taasisi yoyote au kiongozi yoyote anagombanisha wananchi na
serikali, na atakaefanya hivyo hatakama itakuwa ni Taasisi ya Upimaji Viwanja
(UTT) ambae ipo chini ya serikali, ataipinga na kutumia madaraka yake kuifuta
kabisa katika shughuli ya biashara ya ardhi.
“Kwahiyo
nimetoa waraka wangu unaosisitiza juu ya wajibu wa mtu yoyoyte anaechukua ardhi
ya mtu kulipa fidia kabla ardhi ile haijachukuliwa..na fidia yenyewe imfanye
huyu mwenye ardhi yake anaondoka huku anacheka, kama ni ardhi yake halali maana
yake analipwa ardhi na vile vilivyopo ndani ya eneo lake..hii habari ya
kunyang’anya watu kwanguvu halafu watu wananung’unika hawana pakusema, adhabu
inakuja kwa serikali, na kwenye uchaguzi tena CCM inaadhibiwa huko, mimi hiyo
sikubali..” aliongeza.
Aidha, alisema kuanzia Julai 1 mwaka huu gharama za upimaji viwanja kwa wananchi
zitapungua kutoka shilingi laki nane kwa hekari moja mpaka kufikia laki tatu,
kwa lengo la kuongeza kasi ya wananchi kumiliki hati kihalali na kuongeza kuwa kodi watakayolipa
kwa mwaka itapungua kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 400.
Alisema wananchi
wakimiliki ardhi kihalali kwa kuwa na hati, itasaidia kupunguza migogoro baina
yao na serikali kwasababu ulinzi wa maeneo yao itakuwa ni majukumu yao wenyewe.
“Hali hii ya
kuwa na ardhi na mashamba kiholela, bado serikali haitupi faida kwasababu hata
sisi serikali haitupi mapato, mapato yetu yanatokana na wale tu ambao
tumewamilikisha kihalali..kwahiyo kasi ya umilikishaji wa hati kwa viwanja na
mashamba ni ndogo sana, ningeuliza hapa kwa mwaka mzima manispaa na halmashauri
mumemilikisha mashamba mangapi kwa wananchi wa Mtwara mtaniambia hakuna..”
alisema Lukuvi.
Alisema njia
pekee ya kuwawezesha wananchi wa vijijini na kuwafanya waweze hata kwenda benki
kuchukua mikopo ni kuwamilikisha hati za mashamba na viwanja ambazo ndio
zitakuwa dhamana kwao.
…………………mwisho………………………………………….
No comments:
Post a Comment