Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mkuu wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally, leo katika Tarafa ya Mpapura halmashauri ya wilaya ya Mtwara. |
Na Juma Mohamed, Mtwara.
Katika kuunga
mkono juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John
Magufuli za kupiga vita matumizi na biashara ya madawa ya kulevya nchini, mkoa
wa Mtwara umefanikiwa kuwakusanya vijana 156 waathirika wa madawa hayo na kati
ya hao, vijana 104 tayari wameunganishwa katika mpango wa matibabu katika
hospitali ya rufaa ya mkoa huo, Ligula.
Hayo
yameelezwa mkoani hapa jana na mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, baada ya
kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru na mkuu wa mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi, katika
Tarafa ya Mpapura, halmashauri ya wilaya ya Mtwara, kabla ya kumkabidhi mkuu wa
wilaya ya Mtwara Fatma Ally.
“Mkoa wetu
nao ni mwathirika wa madawa ya kulevya, tumeendelea kubanana, kupambana na
kuchukua hatua dhidi ya wale wote wanaoleta madawa kusambaza na watumiaji, mpaka
leo nimesimama hapa kuna kesi 38 ziko kwenye mahakama mbalimbali lakini kuna
vijana 156, na kati yahoo waathirika 104 tumewaunganisha katika mpango wa matibabu
katika hospitali yetu ya mkoa ya Ligula..” alisema Dendego.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego akikumbatiana na mkuu wa wilaya ya Mtwara Fatma Ally baada ya kumkabidhi Mwenge wa Uhuru. |
Aidha,
alisema ukiwa mkoani Mtwara, Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuzindua jumla ya miradi
40 katika halmashauri zote tisa na wilaya tano za mkoani humo yenye thamani ya
sh. Bilioni 49.8 huku mchango wa wananchi ukiwa ni sh. Bilioni 1.8 katika fedha
hizo.
Awali
akizungumza kabla ya kukabidhi mwenge huo kwa mkuu wa mkoa wa Mtwara, mkuu wa
mkoa wa Lindi Godfrey Zambi, alisema Mwenge huo ukiwa mkoani mwake uliweza kuzindua
jumla ya miradi 48 yenye thamani ya sh. Bilioni 11.6, na kwamba kati ya fedha
hizo, ruzuku kutoka serikalini zilikuwa ni sh. Bilioni 8.9 huku michango ya
wananchi ikiwa ni sh. Bilioni 1.5.
“Wahisani
walituchangia sh. Milioni 911.4 halmashauri zilichangia sh. Milioni 305.7..Mhe.
mkuu wa mkoa wa Mtwara, mbio za Mwenge wa Uhuru za mwaka 2016 zimebeba ujmbe
usemao ‘Vijana ni Nguvu Kazi ya Taifa, Washirikishwe na Wawezeshwe, mkoa wa
Lindi kwa kutambua umuhimu wa vijana unaendelea kwa kuwashirikisha katika
shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kuwapatia mikopo yenye ria nafuu, kutenga
maeneo rasmi ya uzalishaji, kukuza masoko ya bidhaa zao na kuwapatia kazi
mbalimbali..” alisema.
Naye, mkuu
wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally akizungumza baada ya kukabidhiwa Mwenge huo na
mkuu wa mkoa wa Mtwara, alisema katika wilaya yake Mwenge utakimbizwa kwa siku
mbili huku miradi 12 yenye thamani ya sh. Milioni 12 ikitarajiwa kuzinduliwa.
No comments:
Post a Comment