Mkazi wa kata ya Chikongola manispaa ya Mtwara Mikindani, Jema Hamisi, akipandishwa kwenye gari la Tanesco kwa ajili ya kuelekea kituo cha Polisi akiwa chini ya ulinzi wa askari baada ya nyumba anayoishi kubainika kuwa inatumia umeme wa wizi
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
SHIRIKA la
Umeme Tanzinia (Tanesco) mkoani hapa limefanikiwa kumkamata Jema Khamisi, mkazi
wa kata ya Chikongola manispaa ya Mtwara kutokana na kubaini kuwa anatumia
umeme wa wizi kwa muda ambao haukuweza kubainika haraka.
Hatua hiyo
imetokana na shirika hilo kupitia maofisa wake kuendesha oparesheni ya kufanya
ukaguzi wa kushtukiza kwa wateja wake, wakiambatana na Mhandisi wa shirika hilo
mkoa wa Mtwara Daniel Kyando, iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya Manispaa
ya Mtwara Mikindani.
Akizungumza
nyumbani kwa mteja huyo baada ya kubaini tukio hilo, Athuman Saidi ambaye ni
fundi wa shirika hilo, alisema walibaini kuwa kuna wizi unafanyika katika
nyumba hiyo baada ya kuona mita ya Luku imefunguliwa ambapo walipochunguza
wakaona waya mmoja umetolewa katika sehemu yake na kufungwa katika sehemu
nyingine.
Fundi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Mtwara, akikata umeme katika nyumba ya Hamisi Namwelenu, mkazi wa kata ya Chikongola, manispaa ya Mtwara Mikindani, baada ya kubaini kuwa inatumia umeme wa wizi. |
Alisema,
kitendo hicho kinapelekea umeme kuingia kwenye nyumba moja kwa moja ambapo hata
mita ikiwa imeishiwa salio la Luku bado umeme utapatikana pasipo malipo yoyote.
“Tulivyoiangalia
ile mita yenyewe umeme iliisha lakini bado mteja ndani umeme anapata, hizi mita
zetu za Luku umeme ukiisha zinajiandika ‘No Credit’ ikishajiandika hivyo
inamaana Yule mteja hawezi kupata umeme mpaka aweke salio ndio umeme utawaka
ndani..ila kwasababu yeye amechukua kabla ya mita ndio maana umeme bado
unaendelea kuwaka.” Alisema.
Alisema,
aina ya wizi uliofanywa katika nyumba hiyo inaonyesha umefanywa na mtu ambaye
ana ujuzi wa masuala ya umeme kwasababu siku hizi kuna vyuo vingi ambavyo
vinafundisha ufundi wa umeme na kupelekea mitaani kuwepo watu wenye taaluma
hiyo.
Akitoa
utetezi wake baada ya kukamatwa, Jema, ambaye katika nyumba hiyo anaishi na
mume wake ambaye hata hivyo hakuweza kupatikana kwa madai kuwa alikuwa kwenye
majukumu yake ya kila siku, alisema hajui lolote kwani toka wamefunga mita ya
Luku hakuwahi kuingiza umeme na baadala yake jukumu hilo linatekelezwa na mume
wake.
“Kwangu mimi
jambo hili limenisikitisha na kunihuzunisha kwasababu mimi ni motto wa kike na
sielewi lolote katika mchakato huu, yani kuelewa kwangu ni baada ya hao mafundi
kufungua hapo na kunielekeza ndio hili suala nalijua liko hivi kwahiyo sielewi
chochote na mimi..” alisema.
Hata hivyo
juhudi za kumpata mume wake aliyemtaja kuwa ni Khamisi Namwelenu, hazikuweza
kufanikiwa mara moja baada ya simu yake kuto patikana ndipo askari polisi
waliombatana na maofisa wa Tanesco kuamua kumkamata mama huyo aliyekutwa na
mototo mdogo na kumfikisha kituoni.
Mhandisi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoa wa Mtwara, Daniel Kyando, akimhoji mkazi wa kata ya Chikongola Jema Hamisi, ambaye nyumba anayoishi inayomilikiwa na Hamisi Namwelenu ilibainika kuwa inatumia umeme wa wizi. |
Kwa upande
wake, Mhandisi wa mkoa, Daniel Kyando, alisema kwamujibu wa sheria za nchi,
kitendo hichi ni kosa kisheria na kwamba kwa taratibu za Tanesco muhusika
anapaswa kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.
“Na taratibu
zetu, tutakukatia umeme na taratibu zingine za kisheria zitafuata ikiwa ni
pamoja na kukufikisha mahakamani..na ndio maana leo tuko na vyombo vya habari
hapa waone kinachoendelea pamoja na askari ambao watatusaidia wewe kukufikisha
mahakamani, na hili liwe fundisho kwa watu wengine katika mkoa wa Mtwara
kufanya hivi..” alisema Kyando.
Katika hatua
nyingine, Tanesco ilibaini tabia ya kujiunganishia umeme kinyume na taratibu
iliyofanywa na Fatuma Athuman, mkazi wa kata ya Magomeni ambaye aliunganisha umeme
katika maeneo mawili tofauti ambayo moja lilikua la biashara na lingine la
makazi huku akitumia mita moja.
Maafisa wa
shirika hilo waliamua kumkatia umeme katika maeneo yote na kumtaka alipe faini
ambayo hata hivyo haikuelezwa moja kwa moja ni kiasi gani alichotakiwa kulipa.
No comments:
Post a Comment