Na Juma
Mohamed, Mtwara.
WAUMINI wa
dini nchini na Watanzania kwa ujumla wametakiwa kuliombea Taifa la Zanzibar ili
liendelee kuwa la amani na utulivu kutokana na kukabiliwa na mvutano wa kisiasa
baada ya Tume ya Uchaguzi visiwani humo kufuta matokeo ya Uchaguzi na kuamuru
uchaguzi huo urudiwe baada ya siku 90.
Wito huo
ulitolewa jana mkoani hapa na Askofu mkuu wa kanisa Katoliki Jimbo la Mwanza
Mwasham Tadeus Rwaichi, katika sherehe za kumsimika Askofu mkuu wa jimbo
katoliki la Mtwara, Mwasham Titus Mdowe, zilizofanyika katika ukumbi wa Kanisa
Katoliki mjini hapa na kuhudhuriwa na waumini wa kikristo kutoka sehemu
mbalimbali hapa nchini.
“Mnaweza
mkasema bara tumeshafanya uchaguzi wa Rais na ameshapatikana na maisha
yanaendelea, lakini haiwezi kuwepo ndoa ambapo mmoja wa wanandowa ni mgonjwa
mkasema kwamba sisi tuko sawa, hatuko sawa kama Watanzania, ningependa
kuwaalika Watanzania wote tuiombee nchi yetu tudumishe umoja, upendo na amani ya
Taifa hili kama familia ya Mungu.” Alisema na kuongeza:
“Nawaomba na
kuwaasa wote wenye uwezo wachangie kupatia ufumbuzi wa kufaa swala
linalorindima kule Zanzibar, tusifurahie wenzetu kuendelea kuvutana,
tusifurahie wenzetu kuendelea kutishiana kuuwana, hilo sio jema Zanzibar
pakiwaka na Bara hapatokuwa shwari..” aliongeza.
Kwa upande
wake, Waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana,
Mhe. Jenister Mhagama, aliwataka waumini wa dini kuzidi kuliombea dua taifa la
Tanzania chini ya serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John
Pombe Magufuli ili liendelee kuwa la amani na utulivu kama ilivyokuwa katika
kipindi cha uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka 2015.
Alisema,
suala la kulinda na kudumisha amani ya nchi ni la kila mmoja na kwamba viongozi
wa dini watumie nguvu waliyonayo ya ushawishi kuubili amani na upendo ili kuzdi
kuijengea heshima nchi.
“Tumetoka
kumaliza uchaguzi mkuu, na kwa mara ya kwanza uchaguzi huo na hasa kwa upande
wa Tanzania Bara umefanyika kwa amani haijapata kutokea, na uchaguzi huo
umeweza kufikia hatua hii ni kwasababu ya waumini wa dini mbalimbali kupiga
magoti na kumuomba Mungu kuliokoa Taifa letu..na uchaguzi huo ukamuweka
madarakani Dkt. John Pombe Magufuli kupata nafasi ya kuongoza kwa miaka Mitano.”
Alisema,
Alisema,
Dkt. Magufuli amejipanga na amedhamiria kuleta mapinduzi ya kimaendeleo na
zaidi ikiwa ni kupambana na mafisadi na wavunjaji wengine wa maadili kwa
vitendo, hivyo anahitaji sana msaada was ala kutoka kwa waumini wa dini ili
kufanikisha hadhma yake hiyo ambayo sio kazi rahisi kuweza kuifanikisha.
Kwa upande
wake, Askofu Titus Mdowe, akizungumza mwishoni baada ya kusimikwa, aliwashukuru
waumini wote waliohudhuria na kufanikisha kwa sherehe hizo na kuahidi kufanya
kazi kwa juhudi zote na kwamba yeye ni kiongozi wa wote hivyo atafanya kazi na
kila mtu.
Alisema,
atahakikisha anakiendeleza vyema kijiti alichokipokea kutoka kwa Askofu mstaafu
wa jimbo katoliki la Mtwara, Gabriel Mmole ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa
kipindi cha miaka 31.
No comments:
Post a Comment