Monday, January 18, 2016

Dangote waomba radhi kufuatia wafanyakazi wao wakigeni kukosa vibali.


Mwakilishi Mkazi wa kampuni ya Dangote nchini Tanzania, Esther Baruti, akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya suala la kukamatwa kwa meneja wa kiwanda hicho na maofisa wa Idara ya Uhamiaji na kuzuiliwa kwa raia wa kigeni wanaofanya kazi kiwandani hapo bila kuwa na vibali

Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mtwara (MTPC), Juma Mohamed (Katikati) akizungumza jambo katika kikao kifupi cha Mkurugenzi wa Sekta Binafsi Nchini (TPSF) Godfrey Simbeye (kushoto) na Mwakili Mkazi wa kampuni ya Dangote nchini Tanzania Esther Baruti (kulia) juu ya suala la hatima ya wafanyakazi raia wa kigeni wa kiwanda hicho waliozuiliwa kufanya kazi na Idara ya uhamiaji kwa kukosa vibali.





Mkurugenzi wa Sekta Binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye,  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya tukio la kuzuiliwa kwa raia wa kigeni wanaofanya kazi katika kiwanda cha Saruji cha Dangote bila kuwa na vibali vya kuwaruhusu kufanya kazi.



Na Juma Mohamed, Mtwara.

MWAKILISHI mkaazi wa kampuni ya Dangote nchini Tanzania, Esther Baruti, ameomba radhi kwaniaba ya kampuni hiyo kufuatia taarifa zilizoandikwa kwenye vyombo vya habari wiki moja iliyopita juu ya kubainika kwa raia wakigeni kiwandani hapo wanaofanya kazi bila kuwa na vibali.
Akizngumza na waandishi wa habari mkoani hapa mbele ya mkurugenzi wa sekta binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye, alisema majukumu aliyonayo ni kuhakikisha kampuni hiyo inatekeleza wajibu wake na kufuata taratibu zote za nchi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa na vibali.

Rais Kikwete akitembezwa na Alhaj Dangote kujionea maeneo mbalimbali ya kiwanda cha saruji cha Dangote Cement Obajan Plant (PICHA-MTANDAO)

Alisema, amekuwa kiungo wa kuunganisha kampuni hiyo na serikali ili kuhakikisha sheria zinafuatwa na kwamba amekuwa akishirikiana vyema na waandishi wa habari wa mkoani hapa kwa kipindi kirefu toka kilipoanza kiwanda hicho mpka kipindi hiki kinapoelekea katika shughuli za uzalishaji ingawa kuna baadhi ya watu ambao wanachangia kuibuka kwa changamoto kadhaa.
“Mimi toka tumeanza kiwanda nimepata ushirikiano mkubwa na waandishi wa Mtwara, hapa katikati tu kuna wengine wanakuja wanavuruga lakini bado mimi niko na Wana-Mtwara..kwasababu sasa hivi tunatoka kwenye ‘project’ tunakwenda kwenye ‘operations’ ndio maana kunakuwa na watu mbalimbali wanaoingilia taratibu wanafanya hivii, unajua kuna mtu mwingine anaweza akaja akakuambia usifanye hivyo mimi namjua Fulani..sasa inafika mahali wewe mwenye jukumu la kushauri hiki kiwe hivi unakuwa husikilizwi..” alisema.

Mwakilishi Mkazi wa kampuni ya Dangote nchini Tanzania, Esther Baruti, akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya suala la kukamatwa kwa meneja wa kiwanda hicho na maofisa wa Idara ya Uhamiaji na kuzuiliwa kwa raia wa kigeni wanaofanya kazi kiwandani hapo bila kuwa na vibali


Alisema, vibali wameshaomba katika idara husika na hata huko nyuma walikuwa wanaomba vibali kwa utaratibu ambao unafahamika baina yao na Idara ya Uhamiaji isipokuwa hili ambalo lilitokea ni kutokana na meneja mkuu wa kiwanda hicho Vidya Sagar Dixit kutotoa ushirikiano kwa maafisa wa Idara hiyo.
“Na mimi kwaniaba ya Dangote na Watanzania wenzangu tunaomba msamaha kwa yote yaliyotokea turuhusu wafanyakazi na serikali nayo ifanye kazi yake ili kiwanda kiendelee tuendelee kupata mipango yote na serikali ambayo imejipanga ili kumsaidia Dangote kwasababu wote, serikali na sekta binafsi tunashirikiana..” aliongeza.
Alitoa wito kwa serikali na watu binafsi kufanya kazi kulingana na mipaka yao na kutokuwa na tabia ya kuingilia majukumu ya mtu mwingine, na kwamba kama sehemu kuna tatizo basi mtu aelekezwe vizuri namna ya kutatua.

Godfrey Simbeye

Kwa upande wake, mkurugenzi wa sekta binafsi nchini, Godfrey Simbeye, alisema alipata nafasi ya kukutana na meneja huyo na alieleza masikitiko yake juu ya kushikiliwa na Idara hiyo huku akiamini kuwa serikali inalishughulikia suala hilo ili shughuli za kiwandani hapo ziendelee kama kawaida.
Alisema, kuhusu wafanyakazi raia wakigeni waliosimamishwa kuendelea na kazi kiwandani hapo kutokana na kukosa vibali, bado wapo nchini na kwamba serikali inalishughulikia suala lao ili kuhakikisha wale wanaokidhi vigezo vya kuendelea kufanya kazi warudi kazini.
“Serikali sasa hivi inachofanya inatathimini ili kuona kwamba wale ambao wanakidhi haja ya kuwa na ‘permit’ ya kuishi Tanzania wanapewa ‘special pass’ ambayo mwakilishi wa Dangote tayari ameshaambiwa alipie ada yake ili vitolewe vibali kwa watu wote ambao wapo Dangote waendelee na kazi huku serikali ikijipanga kutoa vibali vya muda mrefu..” alisema.

Rais Kikwete akikata utepe katika sherehe za uzinduzi wa kiwanda cha kutengeneza Saruji cha Dangote eneo la Msijute mkoani Mtwara (PICHA-MTANDAO)





No comments: