Matokeo ya uchaguzi kisiwani Zanzibar yamefutiliwa mbali.Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kisiwani humo Jecha Salum Jecha amesema kuwa uchaguzi huo haukuwa wa haki na kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa sheria za uchaguzi.
Kwa mujibu wa BBC SWAHILI, mwenyekiti huyo alitangaza hatua hiyo kupitia chombo cha habari cha mamlaka ya eneo hilo ZBC.
Jecha amesema kuwa uchaguzi huo haukuwa wa haki na kwamba kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria za uchaguzi.
SOURCE: BBC SWAHILI
No comments:
Post a Comment