Monday, October 26, 2015

CUF waigaragaza CCM Mtwara mjini..

Mshindi wa kinyang'anyiro cha Ubunge katika jimbo la Mtwara mjini anayesubiri kuapishwa, Maftaha Nachuma wa Chama cha Wananchi CUF akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kutangazwa mshindi na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Limbakisye Shimwela.


Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo la Mtwara mjini, Limbakisye Shimwela, akitangaza matokeo ya Ubunge yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu kubwa na wananchi



Limbakisye Shimwela


Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Mtwara Mjini, Limbakisye Shimwela, akimkabidhi matokeo ya Ubunge, Mshindi wa jimbo hilo Maftaha Nachuma wa CUF


Askari wa Polisi (Field Force) wakiimarisha ulinzi katika eneo la Chuo cha Ualimu Mtwara (TTC) kutokana na wananchi kuwa na shauku ya kutaka kumjua mbunge wao kiasi cha kutaka kuvamia ukumbi wa majumuisho.


Wafuasi wa CUF waliokuwa wakisubiri matokeo ya Ubunge jimbo la Mtwara mjini







Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Mtwara mjini, Limbakisye Shimwela, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutangaza matokeo ya Ubunge.


Na Juma Mohamed

Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo la Mtwara mjini, Limbakisye Shimwela, amemtangaza mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maftaha Nachuma, kuwa ndio mshindi baada ya kuwazidi kwa idadi ya kura wagombea wenzake.

Limbakisye Shimwela

Akitangaza matokeo hayo jana jioni katika kituo cha majumuisho kilichopo katika chuo cha waalimu Mtwara (TTC), amesema Nachuma aliyekuwa akichuana na wagombea wa vyama vya ACT,NCCR,CHADEMA na CCM, ameshinda kwa kura 26,655 sawa na asilimia 47.16, akimzidi aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CCM Hasnain Murji aliyepata kura 24,176 sawa na asilimia 42.78.

Limbakisye Shimwela

Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Nachuma amesema ameyapokea kwa furaha matokeo hayo na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na watu wote bila kujali itikadi za vyama kwani yeye ni mbunge wa watu wote.

Maftaha Nachuma, akizungumza na waandishi wa habari.


Waliojiandikisha katika jimbo hilo ni 83,837 ambapo waliopiga kura halali ni 56,515 na kwamba katika kata 18, CCM wamepata kata 7, CUF kata 8 huku kata tatu zikichukuliwa na CHADEMA.

No comments: