Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mtwara Mikindani wakiwa katika foleni ya kusubiri kupiga kura kuwachagua wagombea wa Ubunge, Udiwani na Rais katika kituo cha Ligula C-2 |
Na Juma
Mohamed.
WAKATI zoezi
la upigaji kura likiwa linaendelea katika vituo mbalimbali hapa manispaa ya
Mtwara Mikindani, baadhi ya vyama vimekumbwa na changamoto ya kukosa mawakala
katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.
Wkizungumza na
Nipashe kwa nyakati tofauti, wagombea Ubunge wa vyama vitatu ambavyo ni Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ACT-Wazalendo na NCCR-Mageuzi wamekiri
kukumbwa na changamoto hiyo kwa sababu zinazotofautiana.
Akizungumza baada
ya kupiga kura katika kituo cha shule ya msingi Kambarage, mgombea Ubunge wa
jimbo la Mtwara mjini kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Bakari Mchira, alisema
vipo baadhi ya vituo ambavyo wamekosa kuwa na mawakala ikiwa ni pamoja na kituo
ambacho amepigia kura.
S/M Kambarage |
Alisema,
hali hiyo imesababishwa na kukosa kuapishwa kwa mawakala wao kutokana na wahusika
wa suala hilo kuwa kwenye semina ya siku mbili juu ya uchaguzi, jambo ambalo
liliwafanya wakose barua za kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi za kuwatambua
kama mawakala.
“Havizidi
vituo vitano ambavyo mawakala hawajaapishwa, tatizo limekuwa ni kuapishwa..na
sio uzembe kwasababu walikwenda ila watendaji walikosekana, unajua wakati wa
kuapa watendaji wa kata ndio wanahusika, sasa siku za mwanzo kulikuwa na watu
wengi maana ni kama inavyokuwa siku za kupiga kura, mtu anakuja anaona kuna
watu wengi anaamua kurudi kwa kujua atakuja siku inayofuata..” alisema
Alisema ili
kutatua changamoto hiyo, wanashirikiana na vyama vingine vya upinzani ambavyo
pia vimekosa mawakala ili kusaidiana majukumu ya kulinda kura.
Naye,
mgombea Ubunge wa chama cha NCCR-Mageuzi, Uledi Hassan Abdallah, alisema,
wanashirikia kwa karibu na Chadema katika kusaidia kuweka mawakala, kwahiyo
pale ambapo hakuna wakala wa NCCR, wakala wa Chadema anahusika kulinda kura zao
na hivyo hivyo kwa Chadema.
Kwa upande
wao, Chadema, kupitia mgombea wao wa Ubunge, Joel Nanauka, alikanusha kuwa na
ushirikiano wa vyama vingine katika kuweka mawakala na kusema kuwa mawakala wao
wanatekeleza majukumu kwa upande wa Chadema pekee.
Ligula C-2 |
Aidha,
walilalamikia kitendo kilichojitokeza katika baadhi ya vituo kuwa na mawakala
wa Chadema ambao hawatambuliki na mgombea huyo ambao walipewa barua na uongozi
wa chama wilaya.
“Kuna
mawakala ambao wanaonekana kuwa na barua za Chadema, lakini mimi kama mgombea na
hata msimamizi mkuu wa mawakala hatuwafahamu, lakini wamejitambulisha na
wameruhusiwa kuingia kwenye vituo lakini nafikiri ni jambo la kisheria zaidi, na
najaribu kulitatua..” alisema Joeli.
Alikiri kuwa
na mgogoro wa kiuongozi ndani ya chama lakini hakutaka kuuzungumzia kiundani
kwasababu ni swala la kiuongozi, huku akidai kuwa na watu ambao waliwapeleka
mawakala kinyume na taratibu na kuwapatia barua za utambulisho.
“Kwahiyo
tuliwakuta kwenye vituo na wale ambao waliwapokea walishindwa kuwatofautisha
kuwa yupi ni yupi halisi, kwahiyo tumekumbwa na changamoto hiyo na ni maeneo
mengi na mimi nawafahamu mawakala wangu, lakini nikienda nakuta wakwangu
wamezuiwa wale wengine wameruhusiwa na wanabarua za utambulisho..” aliongeza.
Mkuu wa
mawakala wa chama hicho, ambaye pia ni mwanasheria wa mgombea huyo, Raymond
Edward, alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo moja ya eneo linalikubwa na changamoto
hiyo ni kituo cha Mingano, na kwamba wakala wake alionyesha barua aliyopewa na
Chadema mkoa.
“Lakini
kitaratibu, kiongozi wa mkoa hawezi kutoa barua ya wakala kwenye kata Fulani,
isipokuwa wilaya husika ndio wanatoa..nilitafuta hekima kwa baadhi ya watu
akiwemo afisa uchaguzi (Msaidizi) anaitwa Kambili, tulipowasiliana naye alikiri
kuuona huo mkanganyiko mapema, lakini walichoamua ni kumpokea Yule wakwanza
kupeleka barua kutoka wialayani au mkoani na anyechelewa hawapokei.” alisema
Alisema,
kwasasa wanajaribu kuwasiliana na uongozi wa chama wa ngazi za juu ili
kuwaeleza hali ilivyo, huku wakijaribu kuwapaelekezo mawakala wale waliopo ili
kujua namna ya kufanya na mambo mengine ya kisheria.
Msimamizi wa
uchaguzi wa jimbo la Mtwara mjini, Limbakisye Shimwela, alikiri kutambua utata
huo huku akihusisha na mgogoro wa ndani ya chama kati ya uongozi wa wilaya na
mkoa, ambao manispaa haiwezi kuingilia.
“Sisi
hatukumuapisha mtu ambaye hakuletwa na chama, barua ililetwa ambaye ilisainiwa
na katibu wao wa chama wa wilaya, kwahiyo kama kuna maeneo mengine wanasema sio
mawakala wao, labda sio kwasababu ya makundi yao ndani ya chama ambayo sisi
hatuwezi kuyaingilia.” Alisema.
Aidha,
alisema hali ya uchaguzi inaendelea vizuri katika jimbo hilo ambapo katika
baadhi ya vituo ambavyo ametembelea amekuta hari ya utulivu huku sehemu
nyingine zikiwa na watu wachache na nyingine kuwa na idadi kubwa ya watu.
No comments:
Post a Comment