Monday, February 6, 2017

Mashindano ya Golf Quarter 6 Dar yatamatishwa chini ya Vodacom

Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania, kanda ya Kawe jijini Dar es Salaam,Straton Mchau(kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu  mshindi wa jumla wa mashindano ya Golf  Quarter  6 ,2016, Hatibu Kisenkoro wakati  hafla fupi  iliyofanyika kwenye viwanja vya Golf Lugalo jijini Dar es Salaam,Iliyoandaliwa na Lugalo Breakfast Community Group  na kudhaminiwa na  Vodacom Tanzania.Katikati ni kaimu  Kapteni,Mada Margwe.


Mshindi wa Tatu wa mashindano ya  Golf  Quarter 6 2016, Godfrey Kilenga akikabidhiwa simu na  Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania,Kanda ya Kawe jijini Dar es Salaam, Straton Mchau (kushoto)wakati wa hafla fupi  iliyoandaliwa na Lugalo Breakfast Community Group  na kufanyika katika  viwanja vya Golf Lugalo jijini Dar es Salaam chini ya Udhamini wa Vodacom Tanzania.Katikati anayeshuhudia ni  Kaimu Kapteni, Mada Margwe.


Mshindi wa kwanza wa mashindano ya Golf  Quarter 6 2016, yaliyoandaliwa na Lugalo Breakfast Community ,Profesa Mahebu Nyirabu(kulia) akikabidhiwa simu na  Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania,Kanda ya Kawe jijini Dar es salaam Straton Mchau (kushoto) wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya Golf Lugalo jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.Katikati  ni  Kaimu Kapteni, Mada Margwe.


Mshindi wa jumla wa mashindano ya Golf  Quarter  6 ,2016,Hatibu Kisenkoro (kulia) akikabidhiwa  kikombe cha Ushindi na Ofisa Uendeshaji wa Klabu hiyo,Captain  Amanzi Mandengule (kushoto) wakati  hafla fupi  iliyofanyika kwenye viwanja vya Golf Lugalo jijini Dar es Salaam,Iliyoandaliwa na Lugalo Breakfast Community Group  na kudhaminiwa na  Vodacom Tanzania,Katikati ni  Kaimu Kapteni,Mada Margwe.


Zawadi mbalimbali


No comments: