Sunday, December 18, 2016

Simba Sc yarejea kileleni baada ya kuifunga Ndanda Fc Mtwara.





Kiungo wa Ndanda FC Salum Telela akijaribu kumtoka mlinzi wa Simba SC Mohamed Huseinkatika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliochezwa katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Simba ilishinda bao 2-0

Mshambuliaji wa Ndanda FC Omary Mponda akimtoka mlinzi wa Simba, Mohamed Husein katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliochezwa katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Simba ilishinda bao 2-0



Mshambuliaji kinda wa Ndanda FC Riphati Khamisi, akipokea mfano wa hundi ya tuzo yenye thamani ya Shilingi Milioni 1 ya mchezaji bora wa mwezi Novemba wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kutoka kwa mkurugenzi wa kanda ya Mashariki ya kati wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom, Bi Harieth Koka.


Riphati Khamisi akiwa na tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Novemba wa VPL




Juma Mohamed, Mtwara

Wekundu wa Msimbazi Simba Sc leo wamefanikiwa kurejea kileleni mwa ligi kuu ya Tanzania Bara na kuwashusha Yanga waliokaa kwa saa kadhaa, baada ya kuwasambaratisha Ndanda FC ya Mtwara kwa jumla ya mabao 2-0 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Simba wanaonolewa na Joseph Omog, walicharuka zaidi kipindi cha pili cha mchezo huo baada ya kushindwa kuliona lango katika dakika 45 za kipindi cha kwanza, ambacho Ndanda walishuhudiwa wakifika langoni mwa Simba mara kadhaa bila mafanikio.

Mlinzi wa Simba SC Mohamed Husein, akichuana na mshambuliaji wa Ndanda FC Omary Mponda, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliochezwa katika uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara. Simba ilishinda bao 2-0.



Alikua ni Mzamiru Yasin alieanza kupeleka kilio kwa wanakuchele katika dakika ya 63, baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Mohamed Ibrahim, ambaye baadaye dakika ya 81 alishindilia msumari wa mwisho langoni mwa Ndanda.
Kabla ya kuanza kwa mchezo huo, kampuni ya mawasiliano ya Vodacom ambao ndio wadhamini wakuu wa ligi hiyo, walimkabidhi mshambuliaji kinda wa Ndanda FC Riphati Khamisi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 1 ikiwa ni tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Novemba wa VPL.
Simba sasa inafikisha alama 38 baada ya kucheza michezo 16 na kuongoza ligi kwa alama mbili nyuma ya Yanga, huku Ndanda wakisalia na alama zao 19.
 

No comments: