Friday, October 14, 2016

Wakulima kuuza Korosho hadi Sh. 3670


Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa wadau wa tasnia ya korosho Tanzania.



Na Juma Mohamed, Mtwara

Kampuni ya Golden Agriculture imeibuka kinara katika ununuzi wa zao la korosho, baada ya kuwashinda washindani wenzake katika mnada wakwanza wa chama kikuu cha ushirika cha Tandahimba, Newala Co-operative Union TANECU uliofanyika leo wilayani Newala.
Mwanasheria wa Bodi ya Korosho Tanzania CBT mkoani Mtwara, Ugumba Kilasa, ameiambia Juma News kwa simu kuwa, kampuni hiyo imeshinda kwa bei ya Sh. 3,670 na kuwa kampuni ilioongoza kwa ununuzi wa bei ya juu katika minada ya leo.

Makamu mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania CBT-Mudhihiri Mudhihiri


Katika mnada uliofanyika wilayani Masasi chini ya chama kikuu cha ushirika cha Mtwara, Masasi Co-operative Union MAMCU, kampuni ya Maviga East Africa imeibuka kinara kwa kufikia bei ya sh. 3,650 na kuwaacha washindani wake kampuni za Machinga, Duliva na CDJKL LTD.

No comments: