Friday, August 26, 2016

Serikali yasema haitofuta mfumo wa stakabadhi ghalani kwa wakulima wa Korosho.

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba, akihutubia katika mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho nchini katika ukumbi wa chuo cha sanaa-Bagamoyo. Mkutano ambao unafanyika kwa siku mbili huku ukiwakutanisha wadau wa zao la korosho wa mikoa yote inayolima zao hilo nchini.


Dkt. Charles Tizeba


Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania-CBT, Anna Abdallah, akiongea na wadau wa korosho katika mkutano unaowakutanisha wadau wa zao hilo kutoka mikoa yote inayolima korosho nchini.

Makamu mwenyekiti wa bodi ya korosho Tanzania-CBT, Mudhihiri Mudhihiri akiteta jambo na mbunge wa Mtwara vijijini Hawa Ghasia katika mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho Tanzania-Bagamoyo.


Wajumbe wa mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho


Mbunge wa Ndnda, Cecil Mwambe akisalimiana na Mstahiki Meya wa manispaa ya Mtwara Mikindani, Geofrey Mwanichisye, katika ukumbi wa chuo cha sanaa-Bagamoyo ambako mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho unaendelea.


Mudhihiri na Katani Ahmad, wakiteta jambo ndani ya ukumbi wa chuo cha sanaa, Bagamoyo unapofanyika mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho Tanzania.


Wabunge wa Tandahimba, Katani Ahmad na Cecil Mwambe wa Ndanda wakiwa katika mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho Tanzania unaondelea katika ukumbi wa chuo cha sanaa-Bagamoyo mkoani Pwani


Mbunge wa Tandahimba, Katani Ahmad akiteta jambo na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Geofrey Mwanichisye katika ukumbi wa Mikutano wa chuo cha sanaa-Bagamoyo.



Juma Mohamed, Bagamoyo

Licha ya wakulima wa baadhi ya wilaya katika mkoa wa Ruvuma kukataa kuuza korosho zao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani, serikali imesema mfumo huo utaendelea kutumika na maeneo yote nchini yanayolima zao hilo yanapaswa kutekeleza mfumo huo.
Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho nchini uliofanyika katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, waiziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dokta Charles Tizeba, amesema bila mfumo huo wakulima wataendelea kutonufaika na zao hilo.

Dkt. Charles Tizeba


Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania-CBT, Anna Abdallah, akiongea na wadau wa korosho katika mkutano unaowakutanisha wadau wa zao hilo kutoka mikoa yote inayolima korosho nchini.


Baadhi ya wabunge kutoka mkoani Mtwara wameunga mkono agizo hilo la serikali licha kuendelea kusisitiza usimamizi bora, huku wakulima kutoka wilayani Tunduru wakiahidi kuanza kuuza mazo yao kupitia mfumo huo katika msimu ujao wa korosho ambao unatarajiwa kuzinduliwa katika mkutano huo.
Mkutano huo uliowakutanisha wadau wa tasnia ya korosho nchini, pamoja na mambo mengine unatarajia kupanga bei dira ya zao hilo kwa msimu mpya wa 2016/2017.

 

 

No comments: