Sunday, July 27, 2014

UINGEREZA YAIBANIA URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2018


FIFA yaikabidhi Urusi haki za kuandaa michuano ya kombe la dunia mwaka 2018.
 Na Juma Mohamed

Naibu waziri mkuu nchini Uingereza Nick Clegg ametoa wito wa Urusi kupokonywa haki za kuandaa mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 2018.

Ameliambia gazeti la Sunday Times kwamba haiwezekani kwa michuano hiyo kufanyika nchini humo kufuatia hatua ya Urusi kuwaunga mkono waasi wa Ukraine mashariki mwa taifa hilo wanaoushukiwa kwa kuitungua ndege ya abiria ya Malaysia hivi majuzi.

Amesema kuwa ulimwengu utaonekana mnyonge iwapo utaruhusu michuano hiyo kuendelea nchini Urusi.
Urusi imelaumu Ukraine kwa kuanguka kwa ndege hiyo iliowauawa takriban watu 300.

SOURCE:BBC

No comments: