|
Kaburu
akimkabidhi Ngassa jezi |
|
Ngassa
akiwasili kama unavyoona umati
unamlaki |
|
Kaburu
akizungumza, kushoto Ngassa |
|
Meneja Vifaa
wa Simba SC, Kessy Rajab akiwa nyuma ya
Ngassa |
|
Ngassa |
|
Ngassa |
|
Ngassa |
|
Waandishi,
Asha Kigundula na Dina Ismail
kulia |
|
Mwandishi
Somoe Ng'itu |
|
Ngassa
anavaa jezi |
|
Imempendezaje? |
|
M16 wa
Msimbazi |
|
TABASAMU;
Kijana anafurahia maisha
mapya |
|
KARIBU SANA;
Kaburu akipeana mikono na Ngassa baada ya
kusaini |
|
Kaburu
akimuangalia Ngassa wakati
anazungumza |
|
MISHA
POPOTE; Ngassa leo yuko
Simba |
|
AAHIDI
MATAJI; Anasema anataka kushinda mataji na
Simba |
Na Mahmoud
Zubeiry
MAKAMU Mwenyekiti wa Simba SC,
Geoffrey Iric Nyange ‘Kaburu’, majira ya saa 5:00 asubuhi ya leo, amemtambulisha
kiungo mshambuliaji mpya wa klabu hiyo, Mrisho Khalfan Ngassa ambaye alisajiliwa
rasmi jana kwa dau la jumla la Sh. Milioni 55, kutoka klabu ya Azam FC, akisaini
mkataba wa miaka miwili.
Ngassa alipokewa kwa shangwe
makao makuu ya Simba, Mtaa wa Msimbazi na mamia ya mashabiki wa klabu hiyo, na
kuingizwa kwenye ukumbi wa mikutano kutambulishwa rasmi. Tendo bila kuchelewa,
katika ukumbi uliosheheni Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya habari
nchini, ‘Mr Liverpool’, Ezekiel Kamwaga, Ofisa Habari wa Simba SC alimkaribisha
Nyange Kaburu amtambulishe Ngassa.
Pamoja na kuzungumzia Mkutano
Mkuu wa Simba, utakaofanyika Jumapili katika ukumbi wa Polisi Oysterbay, Kaburu
alimtambulisha Ngassa na kumkabidhi jezi namba 16, ambayo alikuwa anaivaa
Azam.
Ngassa alisema kwamba
anashukuru kwa mapokezi mazuri Simba SC, yamemfariji na sasa wana Simba wasubiri
kulipwa fadhila zao. “Naamini tu nitafanya vizuri katika klabu hii, kushinda
mataji na Simba ndio ndoto zangu, namshukuru Mungu. Hii ni klabu kubwa, klabu
ambayo hata baba yangu aliichezea,”alisema Ngassa.
Simba ilifanikiwa kumalizana
na Ngassa jana na kusaini naye mkataba wa miaka miwili, ambao umemfanya aondoke
na zaidi ya Sh. Milioni 35, Milioni 12 akipewa taslimu na nyingine akipewa gari
(Milioni 18), wakati mpenzi mwingine wa Simba amemuongezea Milioni
5.
Katika mkataba huo wa Simba na
Ngassa, mshambuliaji huyo atakuwa akilipwa Sh. Milioni 2 mshahara kwa mwezi,
Milioni 1 ipo kwenye fomu ya mkataba na Milioni 1 atakuwa akiongezewa na mtu.
Usajili wa mchezaji huyo,
ulikakamilishwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Hans Pop, ambaye
ndiye alitoa fedha hizo na baada ya kumsainisha na kumkabidhi haki yake, ili
kumuondolea usumbufu akambadilishia ‘chipu’ ya simu, ili akina Seif Magari
wasimpate.
Juzi Simba ilimnunua Ngassa
kutoka Azam kwa Sh. Milioni 25, lakini mchezaji huyo wa zamani wa Yanga akagoma
kwa sababu hakushirikishwa katika dili hilo.
Kwa kumuongeza ‘kifurushi’ cha
Sh. Milioni 35, ina maana Simba imemsajili Ngassa kwa Sh. Milioni 60 kwa miaka
miwili, ambalo ni dau kubwa zaidi la usajili kwa mchezaji huyo tangu aanze
kucheza soka.
Yanga ilimsaini kwa Sh.
Milioni 25 jumla kutoka Kagera Sugar mwaka 2007 pamoja na uhamisho wake akasaini
mkataba wa miaka mitatu, wakati miaka miwili iliyopita, Azam ilimsajili kwa Sh.
Milioni 55 pamoja na uhamisho wake (Sh. Milioni 30) ikimsainisha mkataba wa
miaka mitatu, ambao ulitarajiwa kumalizika mwakani.
Azam ilifikia uamuzi wa
kumuuza Ngassa, baada ya mchezaji huyo iliyemsajili kutoka Yanga miaka miwili
iliyopita, kubusu jezi ya Yanga baada ya kufunga bao la pili katika Nusu Fainali
ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, dhidi ya AS Vita ya
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Na uamuzi huo, ni wa mzee Said
Salim Bakhresa mwenyewe, ambaye alikerwa na kitendo hicho akawaagiza wanawe,
Wakurugenzi wa bodi ya timu wamuuze mchezaji huyo popote, haraka
iwezekanavyo.
No comments:
Post a Comment