Friday, July 13, 2012

TASLIMA AZUIA UCHAGUZI YANGA, KIJANA WAKE CHUPUCHUPU WATU WAMGAWANE

Jamaa mmoja mida hii chupuchupu agombewe na wanachama wa Yanga, baada ya kufika makao makuu ya klabu, Jangwani akiwa na barua ya wakili ya kushauri uchaguzi wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika Jumapili uahirishwe. Kilichomponza ni kwamba, alipofika mlango wa kuingia klabuni, akasema anataka kumuona Katibu Mkuu, ana barua ya Mahakama ya kuzuia uchaguzi. Watu kusikia hivyo wakamvaa, kwanza wakampora begi lake wakachukua barua wakaisoma. Wakagundua ni ya wakili tu na haina nguvu, ndipo wakamrudishia barua yake na kumfukuza, tena wakimuonya asionekane kabisa katika viunga hivyo. Soma barua yenyewe….


Jamaa mwenyewe ndio huyu

 

YANGA FANS FACEBOOK WAMWAGA MAJI KLABUNI

Beki wa Yanga, Ladislaus Mbogo kulia, akipokea msaasa huo

Mwesigwa alikuwa anaendelea na mambo yake

Na Princess Asia
Wanachama na mashabiki wa Yanga wa kundi cha Young Africans SC Fans katika facebook, leo wamekabidhi msaada wa maji ya kunywa kwa ajili ya wachezaji wa klabu hiyo, wenye thamani ya Sh. 80,000 ofisini kwa Katibu Mkuu wa Yanga, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam.
Akikabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa kikundi hicho, Innocent Mwingira alisema kwamba wameamua kutoa msaada huo ili pamoja na kudhihirisha mapenzi yao kwa klabu yao, lakini pia kufungua milango kwa watu wengine wenye uwezo wa kutoa misaada midogomidogo ya aina hiyo, wajitokeze.
“Tunaamini tulichotoa kitasaidia klabu, japo kwa siku mbili, Yanga ina mamilioni ya wapenzi, kama wakijitokeza wengine na wengine, tuna hakika klabu yetu haitakuwa na matatizo madogo madogo, hivyo sisi tunawaomba na wengine pia waige mfano huu,”alisema.
Akipokea msaada huo, beki wa Yanga Ladislaus Mbogo alisema kwamba kwa niaba ya wachezaji wenzake anashukuru kwa msaada huo kwani hiyo ni ishara kwamba wapenzi hao wapo nyuma ya wachezaji.
Katibu wa Yanga, Selestine Mwesigwa aliwashukuru wapenzi hao na kusema huo ni mfano wa kuigwa na akafungua milango kwa wapenzi wengine wowote wa Yanga, kujitokeza wakati wowote kutoa chochote walichonacho.
Kwa upande wake, Katibu Msaidizi wa kikundi hicho, Fadhila Lemba alisema kwamba msaada huo kwao ni mwanzo tu na watakuwa wakijikusanya na kutoa zaidi.

MWANZA YATINGA FAINALI COPA COCA COLA


Na Princess Asia
MWANZA imejipatia tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola 2012 baada ya leo asubuhi (Julai 13 mwaka huu) kuilaza Temeke mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Hadi dakika 90 za kawaida zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1. Mwanza walitangulia kufunga dakika ya tatu kupitia kwa Jamal Mtegeta kabla ya Temeke kusawazisha kwa penalti dakika ya 56 iliyowekwa wavuni na Baraka Ntalukundo.
Mabao mengine ya Mwanza yaliyoipatia tiketi ya kucheza fainali keshokutwa (Jumapili) yalifunga katika dakika 30 za nyongeza. Mtegeta alitikisa wazu dakika ya 94 kabla ya Dickson Ambundo kukwamisha la tatu dakika ya 108.
Nusu fainali ya pili itachezwa leo jioni ikikutanisha timu za Morogoro ambayo kwenye robo fainali iliibamiza Mara mabao 4-0 na Tanga iliyopata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Dodoma.

NYIGU WATOTO WAJA KUIVAA NGORONGORO


Frank Damayo, mmoja wa
nyota wa Ngorongoro
Na Prince Akbar
TIMU ya taifa ya Rwanda ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 inatarajia kuwasili Dar es Salaam leo mchana (Julai 13 mwaka huu) kwa ndege ya RwandAir kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki dhidi ya Ngorongoro Heroes.
Rwanda yenye msafara wa watu 27 wakiwemo wachezaji 20 itafikia hoteli ya Sapphire. Mechi hizo zitachezwa Julai 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Chamazi na Julai 16 mwaka huu Uwanja wa Taifa.
Ngorongoro Heroes tayari iko kambini chini ya Kocha Jakob Michelsen na msaidizi wake Adolf Rishard kujiwinda kwa mechi hizo ambazo ni sehemu ya maandalizi ya kuivaa Nigeria.
Mechi dhidi ya Nigeria ambayo ni ya kwanza ya raundi ya pili kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Algeria itachezwa Julai 29 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

TUSKER WATUA LEO KUKAMILISHA IDADI TIMU ZA KAGAME 2012


Kikosin cha Tusker FC

Na Prince Akbar
MABINGWA wa zamani Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Tusker ya Kenya na Ports ya Djibouti zinawasili leo jioni kukamilisha idadi ya timu 11 zinazoshiriki mashindano ya Kombe la Kagame yanayoanza kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi za kesho ni APR ya Rwanda dhidi ya El Salam Wau ya Sudan Kusini itakayoanza saa 8 kamili mchana na kufuatiwa na ya saa 10 kamili jioni kati ya mabingwa watetezi Yanga na Atletico ya Burundi.
Timu zote kutoka nje ya mazoezi zimeshapangiwa viwanja vya mazoezi ambapo zitavitumia kwa mujibu wa ratiba ambayo imepangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Makazi ya timu hizo na viwanja vya mazoezi ni kama ifuatavyo;


Timu: Uwanja wa mazoezi: Accommodation:
APR (Rwanda) Mabibo Hostel - Marriott Hotel (Mabibo External)
AS Vita (Congo) University of Dar es Salaam - Chichi Hotel (Kinondoni)
Atletico (Burundi) Mabibo Hostel - Lunch Time Hotel (Mabibo Hostel)
Azam (Tanzania) Azam Complex - Azam Complex (Chamazi)
El Salam Wau (S. Sudan) Zanaki Sekondari - Rungwe Hotel (Kariakoo)
Mafunzo (Z’bar) Kinesi - Rombo Green View Hotel (Sinza)
Ports (Djibouti) Kinesi - Rombo Green View Hotel (Sinza)
Simba (Tanzania) ……………………. – Vina Hotel (Mabibo Makutano)
Tusker (Kenya) Zanaki Sekondari - Rungwe Hotel (Kariakoo)
URA (Uganda) Loyola - Valentino Royal Hotel (Kariakoo)
Yanga (Tanzania) …………………. – ……………………….
 

SAFU YA UONGOZI YANGA HII HAPA, KASWAHILI AIPIGA ZENGWE

Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili ameonya juu ya kampeni chafu kuelekea uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo, uliopangwa kufanyika Jumapili, ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Akizungumza makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kaswahili amesema hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa, ikiwemo watu kufutiwa uanachama. Miongoni mwa aliyokemea ni vipeperushi vinavyoonyesha safu kamili ya watu wa kuwachagua kwenye uchaguzi huo. Pichani Kaswahili akionyesha kipeperushi chenye safu ya uongozi iliyopangwa.

Safu ya uongozi iliyokemewa na Kaswahili, lakini si inafaa kabisa hii jamani?

No comments: