Wednesday, July 4, 2012

MJINI MAGHARIBI YATINGA 16 BORA COPA COCA COLA


 

Na Princess Asia
MJINI Magharibi imetinga hatua ya 16 bora ya michuano ya Copa Coca-Cola baada ya leo (Julai 4 mwaka huu) kuilaza Tanga bao 1-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Bao la washindi katika mechi hiyo ya kundi B lilifungwa dakika ya 68 na Juma Ally. Kwa matokeo hayo Mjini Magharibi ambayo imemaliza mechi zake imefikisha pointi 13 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine katika kundi hilo.
Mbeya imejipatia ushindi wa pili mfululizo katika kundi lake la C baada ya leo kuifunga Mara bao 1-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Tanganyika Packers ulioko Kawe, Dar es Salaam. Mshambuliaji John Jerome alifunga bao hilo pekee dakika ya 43.
Licha ya ushindi huo Mbeya wameshindwa kukata tiketi ya 16 bora kwani wamemaliza mechi zao wakiwa na pointi sita tu. Timu za Dodoma yenye pointi 12 na Kinondoni ambayo imefikisha pointi 10 na mechi moja mkononi ndizo zilizofuzu kucheza 16 bora kutoka kundi hilo.
Pwani imepata ushindi wake wa kwanza katika kundi lake la D baada ya leo kuichapa Kagera mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Nyumbu mkoani Pwani. Mabao ya washindi yalifungwa na Cotiveno Ngaga dakika ya 19, Abdallah Juma dakika ya 30 na Salum Ame dakika ya 68.
Kagera ambayo imebakiza mechi moja dhidi ya Shinyanga ikiwa na pointi sita ilipata bao dakika ya 42 kupitia kwa Athuman Kassim. Nazo Ruvuma na Arusha zimetoka suluhu katika mechi ya kundi A iliyochezwa Uwanja wa Tamco.

‘LULU’ YA SIMBA ‘TAKATAKA TU’ COASTAL UNION


Shiboli

Na Princess Asia
MSHAMBULIAJI aliyewahi kugombewa na klabu za Simba na Yanga, kabla ya hajaangukia kwa Wekundu wa Msimbazi, mwaka juzi- Ahmad Ally ‘Shiboli’ ni miongoni mwa wachezaji 11 waliomaliza mikataba yao ya kuichezea timu ya Coastal Union ya Tanga inayoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, na sasa wako huru kujiunga na klabu yoyote.
Kwa mujibu wa Coastal Union, wachezaji wengine ni Ben Mwalala, Samwel Temu, Francis Busungu, Lawrence Mugia, Daudi Chengula, Godfrey Mmasa, Mwinyi Abdulrahman, Sabri Ramadhan China, Soud Abdallah na Ramadhan Wasso.
Uhamisho wa wachezaji kwa msimu huu ulianza Juni 15 mwaka huu na utamalizika Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuanza wachezaji (kwa wasio wa Ligi Kuu) ni kati ya Juni 15 na 30 mwaka huu.
Kwa klabu za Ligi Kuu kutangaza wachezaji watakaositishiwa mikataba yao ni kuanzia Juni 15-30 mwaka huu na usajili wa wachezaji unafanyika kuanzia Juni 15 hadi Agosti 10 mwaka huu.
 

STARS YAKWEA MATAWI YA JUU FIFA


PONGEZI KWAKO; Kocha mpya Taifa Stars, Kim Poulsen kazi ya mwezi uliopita imezaa matunda

Na Prince Akbar
TANZANIA imependa kwa nafasi 12 kwenye orodha ya viwango vya ubora ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) iliyotolewa leo (Julai 4 mwaka huu) na shirikisho hilo.
Kwa viwango vya Juni mwaka huu, timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, ilikuwa namba 139 hivi sasa imefika nafasi ya 127 ikiwa na pointi 253 kulinganisha na 214 za Juni mwaka huu.
Ivory Coast inayoshika nafasi ya 16 duniani bado inaongoza kwa upande wa Afrika ikiwa na pointi 939. Timu hiyo ilikuwa katika nafasi hiyo hiyo kwa viwango vilivyotolewa Juni 6 mwaka huu. Hispania ambao ni mabingwa wa Ulaya na Dunia ndiyo wanaoendelea kuongoza kwa kukamata nafasi ya kwanza wakiwa na pointi 1,691.

BREAKING NEWS: YANGA WAFUKUZWA ZANZIBAR


Na Prince Akbar
CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA) kimewafukuza Yanga katika mashindano ya Urafiki, kwa kitendo cha kupeleka kikosi cha vijana (Yanga B) badala ya kikosi cha wakubwa kwenye michuano hiyo kama walivyokubaliana.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya ZFA, kimeiambia BIN ZUBEIRY jioni hii, kwamba ZFA na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ujumla wamekerwa na kitendo kilichofanywa na uongozi wa Yanga na wamekichukulia kama ni dharau, kupeleka timu B badala ya timu A.
“Mashindano haya kuendesha ni gharama, jana Yanga wamecheza, watu wamekuja wanaona timu B, wametukana sana, wamesema ni utapeli, dhahiri mechi ijayo watu hawatakuja uwanjani. Sasa tutawahudhumia Yanga kwa gharama kubwa, wakati watu hawaendi uwanjani kuwaona watoto wao wa B.
Kwa sababu hiyo, ZFA baada ya kushauriana pia na baadhi ya viongozi wa serikali (ya Mapinduzi), tumeamua kuwarudisha watoto wa Yanga Dar es Salaam, wameondoka na boti ya saa 10:00 na watafika Dar es Salaam saa 12, kawapokeeni,”kilisema chanzo chetu kutoka ZFA.
Chanzo hicho kilisema mashindano hayo, yalikuwa yana lengo zuri tu la kuzipa matayarisho timu zote zinazocheza michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame, inayoanza Julai 14, Dar es Salaam- ambazo ni Mafunzo kwa upande wa Zanzibar na Simba, Azam na Yanga kwa upande wa Bara.
“Lakini ajabu Simba na Azam wameleta timu zao za kwanza, ila wao Yanga wanaleta watoto, sasa hii ni dharau kwetu kama ZFA na kinyume cha makubaliano yetu na wao. Ni dharau kwa falimia yote ya wapenda soka wa Zanzibar, ni dharau kwa wapenzi wa Yanga wa huku,”kilisema hicho.
Yanga pamoja na kupeleka timu B, lakini jana kilicheza soka ya uhakika dhidi ya mabingwa wa zamani wa Tanzania, Jamhuri ya Pemba na kufungwa kwa taabu mabao 3-2.

KOCHA MBELGIJI YANGA TAYARI AMEWASILI DAR, TAZAMA ALIVYOPOKEWA KIFALME

Kocha mpya wa Yanga, Mbelgiji Thom Saintfiet amewasili mida hii Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kulakiwa na mamia ya wapenzi wa klabu hiyo. Tazama mapokezi yake tangu anatokea ndani ya Uwanja wa Ndege, hadi akiwa ndani ya gari tayari kwa safari ya Jangwani.












 

TBL YAKABIDHI 'MPUNGA' WA UCHAGUZI YANGA

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steven Kilindo (kulia) akimkabidhi mfano wa Hundi ya Sh. Milioni 20, Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesigwa (kushoto) katika hafla fupi ya kukabidhi hundi hiyo iliyofanyika makao makuu ya TBL, Ilala Dar es Salaam asubuhi ya leo.
TBL imetoa fedha hizo kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo, uliopangwa kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, Julai 15, mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya mkataba wa udhamini baina ya Yanga na Kilimanjro Premium Lager Beer, inayozalishwa na TB L.
Wengine nyuma yao, kutoka kulia ni Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili, Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah, Meneja wa Bia ya Safari Lager aliyemuwakilisha George Kavishe, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro aliye safarini na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Jaji John Mkwawa.

Angetile akielezea jambo, kulia kwake ni Kaswahili

Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu katikati akiwa na 'vimwana' Dina Ismail kulia na Elizabeth Mayemba kushoto

Mwesigwa akiondoka TBL na begi lake dogo likiwa na 'mahela', kulia ni Clara Alphonce wa Mwananchi

Mkurugenzi wa Executive Solutions, Aggrey Marealle aliyekuwa mwongoza shughuli hiyo


Oscar Shelukindo katikati akimuwakilisha George Kavishe. Kulia ni Kilindo na kushoto Mwesigwa

Jaji Mkwawa akitafakri jambo

Mwesigwa akizungumza

Sehemu ya Waandishi walioalikwa

Michael Momburi wa Mwanaspoti kulia, akiwa Dina Ismail wa Tanzania Daima

Unaweza kuwaona magwiji hapo, Clara, Eliza, Grace Hoka na |Somoe Ng'itu na kwa mbele kulia ni jembe la Channel 10, Said Makalla

Ofisa wa Executive Solutions, Ibrahim Kyaruzi kulia akiwa Ofisa wa TBL kwenye hafla hiyo

No comments: