![]() |
Mashabiki wakifurahi na kupiga picha na Atupele Green, baada ya kufunga magoli Matatu (PICHA: MOSES MPUNGA) |
Na Juma
Mohamed, Mtwara.
BAADA ya
kuivurumisha bila huruma Mbeya City Jumatano iliyopita katika michuano ya ligi
kuu ya Tanzania Bara kwa jumla ya magoli 4-1, timu ya soka ya Ndanda Fc ya
mkoani hapo jana iliendeleza wimbi la ushindi baada ya kuigaragaza Mshikamano
ya jijini Dar es Salaam kwa magoli 5-0 katika mchezo wa mzunguko wa Tatu wa
kombe la shirikisho la Azam Sports Federation Cup (FA) uliopigwa uwanja wa
Nangwanda Sijaona.
Wenyeji
walionekana kuutawala mchezo kama ilivyokuwa katika mchezo uliopita, ambapo jana
safu ya ushambuliaji ya Ndanda ilionekana kuwa hatari zaidi langoni mwa
Mshikamano, ambapo mpachika mabao wao aliyesajiliwa msimu huu kutokea Kagera
Sugar, Atupele Green aliendelea kuwadhihirishia Wanakuchele kuwa hawakufanya
kosa kumsajili baada ya kurudi nyavuni mara Tatu huku William Lucian na nahodha
Kigi Makasy wakihitimisha idadi hiyo ya 5-0.
Ushindi wa
jana kwa Ndanda unaipa nafasi ya kusonga mbele katika mzunguko wa Nne wa
michuano hiyo ambayo bingwa wake ndio atakayewakilisha nchi katika michuano ya
kombe la Shirikisho Barani Afrika, ambapo hapo awali mshindi wa pili wa ligi
kuu ndiyo alikuwa akishiriki.
![]() |
Kocha wa Ndanda Fc, Amimu Mawazo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo. (PICHA: MOSES MPUNGA) |
Kiwango cha
Ndanda kimeonekana kuimarika kuanzia katika mchezo wao wa ligi kuu walipokutana
na Yanga ambapo hata hivyo walipoteza kwa goli 1-0 kabla ya kuduwaza Mbeya City 4-1 huku hapo
jana wakiichakaza bila huruma Mshikamano kwa 5-0 hivyo kuifanya iweke rekodi
mpya ya ushindi mkubwa zaidi tangu ipande Ligi kuu msimu uliopita.
Kabla ya
ushindi huo, ushindi mkubwa kwa ‘Wanakuchele’ ulikuwa ni wa magoli 4-1 ambapo
waliupata msimu uliopita katika mechi yao ya kwanza ya ligi kuu katika uwanja
wa Kambarage Shinyanga baada ya kuifunga Stand United, hivyo kupata tena
ushindi kama huo msimu huu katika uwanja wa nyumbani dhidi ya Mbeya City.
![]() |
Mashabiki wakifurahi na kupiga picha na Atupele Green, baada ya kufunga magoli Matatu (PICHA: MOSES MPUNGA) |
Vilevile
ushindi wa 5-0 unaifanya Ndanda kuivunja rekodi yake yenyewe ya ushindi wa 4-1
waliyoiweka Jumatano iliyopita dhidi ya Mbeya City katika uwanja wa Nangwanda
Sijaona. Ikumbukwe kuwa kabla ya hapo Ndanda walikuwa hawajawahi kupata ushindi
mkubwa kama huo katika uwanja wa Nyumbani.
Timu hiyo
sasa imefikisha idadi ya magoli tisa katika michezo miwili huku yenyewe
ikiruhusu goli moja pekee.
No comments:
Post a Comment