Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego |
Picha ya pamoja kati ya mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, aliyekaa katikati, na wadau wa habari wa mkoa wa Mtwara. |
Na Juma Mohamed.
WAANDISHI wa
habari mkoani hapa wametakiwa kufanya kazi zao kwa kujiamini na kwa kufuata
maadili yao, wakati wa kuandika habari katika kipindi cha uchaguzi.
Akizungumza
jana katika ufunguzi wa mkutano wa wadau ulioandaliwa na Chama cha Waaandishi
wa Habari Mkoa wa Mtwara (MTPC), mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego,
alisema mkoa unatambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari, hivyo
umejipanga kuhakikisha usalama unakuwa wakutosha kwao.
Alisema,
toka amewasili mkoani hapa miezi kadhaa iliyopita, amekuwa akishirikiana vema
na wanahabari, jambo ambalo linamfanya aamini kuwa ni wadau muhimu kwake na kwa
mkoa kwa ujumla.
Aidha,
alitumia fursa ya kuzungumza katika mkutano huo kuwataka wananchi zaidi ya
700,000 wa mkoa wa Mtwara waliojiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga
kura, kwenda kupiga kura siku ya Jumapili ya Oktoba 25, kwani wajibu wao.
“Tumepita
katika kipindi cha kampeni, na sasa tunaelekea katika uchaguzi..nawaomba
wajitokeze wale wote waliojiandikisha waende wakatendee haki nafsi zao, wakachague
viongozi ambao wanaamini watawavusha katika kipindi cha miaka mitano..”
alisema.
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego |
Aliwaondoa hofu
wananchi juu ya wasi wasi uliopo kuhusu uvunjifu wa amani, na kusema kwamba
vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga vyema kuhakikisha amani inatawala
katika kipindi cha uchaguzi mpaka wakati wa kutangaza matokeo kama ilivyokuwa
katika wakati wa kampeni ambazo zinaelekea mwisho.
Kwa upande
wake, Shekh mkuu wa mkoa wa Mtwara, Shekh Nurdin Abdallah Mangochi, akizungumza
kama mdau wa habari, alisema anaimani na waandishi wa habari katika kutenda
haki na kuhakikisha amani inaendelea kutawala ndani ya mkoa.
Alisema,
waislamu kawaida yao ni kuswali swala tano kila siku na kwamba anaimani kama
ilivyo kwake, na wengine hufanya ibada kwa kumuomba mungu juu ya kutawala amani
katika uchaguzi ili zoezi hilo liweze kupita kwa amani.
Naye,
mwenyekiti wa Chama cha Wazee na Wastaafu (CHAWAMU) mkoa wa Mtwara, Robert
Maganga, alisema, uchaguzi wa mwaka huu umekuwa na msisimko mkubwa kwa wananchi
hasa vijana, lakini wanaimani kubwa juu ya mchango wa vyombo vya habari katika
kuandika habari zenye kuleta masilahi kwa taifa ambazo haziwezi kuwa na
upendeleo wa upande wowote.
Alisema,
wazee wanakuwa katika wakati mgumu ikitokea kuna hari ya uvunjifu wa amani
ktokana na wengi wao kukosa nguvu kama ilivyo kwa vijana, jambo ambalo
linapelekea kudhulika kirahisi kwa kushindwa kujiokoa.
Mwandishi wa
habari mwandamizi na mwanachama wa MTPC, Philipo Lulale, aliwaasa wanahabari
kutoonyesha upenzi wao wa kisiasa katika chama chochote ili kuhepusha
kutofautiana na wananchi.
Alisema,
uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu kutokana na ushindani uliopo hasa kwa wagombea
wawili wa nafasi ya Urais, ambao ni Mhe. John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) na Mhe. Edward Lowassa, wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
akiungwa mkono na vyama vya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
No comments:
Post a Comment