Basi la Azam Fc, likitoka ndani ya uwanja wa Nangwanda Sijaona baada ya kumaliza mazoezi ya jioni |
Na Juma Mohamed
Timu za soka
za Ndanda Sc na Azam Fc, kila moja imetamba kuibuka na ushindi katika mchezo wa
ligi kuu ya Tanzania bara unaotarajiwa kuchezwa kesho, katika dimba la
Nangwanda Sijaona, mkoani Mtwara.
Msemaji wa Azam Fc, Jaffer Idd, akizungumza na NEWS ROOM juu ya maandalizi ya timu hiyo kwa ajili ya mchezo wa kesho dhidi ya Ndanda Sc. |
Akizungumza leo
na NEWS ROOM, msemaji wa Azam Fc ya jijini Dar es Salaam, Jaffer Idd Maganga,
amesema wanafahamu ugumu wa mchezo huo kutokana na timu zote kuhitaji alama
tatu ambazo walizikosa katika michezo yao iliyopita, lakini kikosi chao kipo imara
kwa ajili ya kuondoka na ushindi.
Alisema, licha ya upana wa kikosi chao kilichosheheni wachezaji mchanganyiko wa ndani na nje ya nchi, bado wanawaheshimu Ndanda kutokana na upinzani wanaoupata pindi wanapokuta.
Aidha, aliwataja wachezaji watatu ambao watakosekana katika mchezo huo muhimu ambao wanahitaji alama tatu kuweza kuendelea kuwakaba koo Yanga walio kileleni, kuwa ni Abuubakar Salum 'Sure Boy' mwenye kadi tatu za njano, Marick Farid na Mudathir Yahaya ambao ni majeruhi.
Kwa upande
wake, kocha wa Ndanda Sc, Amimu Mawazo, amesema pamoja na mapungufu yaliyopo
katika kikosi chao hasa katika eneo la kiungo, lakini amewaandaa vizuri vijana
wake na kuahidi kuendeleza ubabe wao mbele ya wanalambalamba hao katika uwanja
wa nyumbani.
Aidha,
mashabiki wa Ndanda wamesema bado wanaimani na timu yao kuwa itaibuka na
ushindi hapo kesho, licha ya kutopata matokeo mazuri katika michezo yao
iliyopita hasa ya ugenini.
No comments:
Post a Comment