Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya kudumisha hali ya amani na utulivu kuelekea katika uchaguzi mkuu. |
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego. |
KUFUATIA kutoelewana
kati yaTume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na baadhi ya vyama vya siasa juu ya
suala la kusimama umbali wa mita 200 kutoka eneo la kupigia kura, baadhi ya
wananchi wa manispaa ya Mtwara Mikindani wameanza kushikwa na hofu juu ya
usalama wao kiasi cha kulazimika kukimbia mji.
Kwa mujibu
wa mashuhuda waliopo katika kituo kikuu cha mabasi mkoani hapa, wamesema
kuanzia juzi asubuhi kumekuwa na idadi kubwa ya wasafiri wanaotoka mjini Mtwara
kuelekea sehemu mbalimbali hasa wilayani, kuliko wanaingia mjini.
Wakizungumza
na Nipashe jana kwa nyakati tofauti, wananchi hao wakiwamo madereva wa mabasi
ya wilayani walisema, kati ya wasafiri idadi kubwa imeonekana ni kina mama.
“Hata hizi
gari za Newala leo nimeona zimeondoka na abiria ni wengi mno kupita maelezo,
kwahiyo kwangu mimi naweza nikasema sijui wanachoenda kufanya huko waendako
lakini naweza nikasema hili sio swala la kawaida kwasababu sio siku zote inakua
hivi ni siku hizi mbuli tatu tu kuelekea uchaguzi..na wengi wanaoondoka ni kina
mama pamoja na watoto wadogo..” alisema Ali Njaru, ambaye ni dereva wa mabasi
yanayotoka Mtwara kwenda Kirambo, mpakani mwa Msumbiji na Tanzania.
Naye, Shabia
Liwowa, alikiri kushuhudia magari ya askari polisi na ya Jeshi yakipita katika
maeneo mbalimbali ya mji wa Mtwara huku mengine yakipiga ving’ola, jambo ambalo
limepelekea kuwatisha wananchi na kusababisha baadhi yao kuamua kuondoka mjini.
Mabasi yanayokwenda wilaya mbalimbali za mkoa wa Mtwara. |
“Kura hii
ipite kwa amani na kwa utulivu, ili aliyekua na motto amtunze motto wake na
aliyekua na nyumba atunze nyumba zake..tunachoomba sisi hao askari wanopita
wapiti tu kwa amani..kama wanapita wanazunguka basi watuambie kama wanapita tu
kwa amani..” alisema.
Alisema,
katika nyumba yake anayoishi, wapo baadhi ya watu walioondoka kuelekea vijijini
kutokana na woga wa kuhofia kuzuka kwa vurugu siku ya uchaguzi, ikiwa ni pamoja
na mama mmoja ambaye hakumtaja jina aliyeambatana na watoto wake.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mtwara (RPC) Henry Mwaibambe, alipotafutwa kwa simu ili aweze
kuzungumzia hilo, simu yake iliita bila kupokelewa.
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego. |
Awali
akizungumza katika kiako na waandishi wa habari juu ya kuwahamasisha wananchi
kudumisha amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, Mkuu wa
Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na
Usalama ya Mkoa, aliwataka wananchi kuondoa hofu juu ya kutokea kwa vurugu, na
kukiri kuwa na taarifa za baadhi yao wanahama mji, ambapo alisema mkoa kupitia
kamati yake ya ulinzi na usalama wamejipanga vyema kuhakikisha usalama
unakuwepo kwa wananchi wake.
Aidha,
alisema wamebaini kuwepo kwa makundi mbalimbali yaliyoandaliwa kwa ajili ya
kufanya vurugu na kuzuia watu kwenda kupiga kura, katika maeneo mbalimbali ya
mkoa wa Mtwara.
“Mfano
maeneo ya Mkanaledi, Mikindani-Mtwara, Tandahimba na Ndanda..aidha, zipo
taarifa za makundi hayo kujiandaa na silaha za jadi kushambulia vyombo vya
dola, na uchomaji moto majengo ya serikali, nawatahadharisha wale wote wenye
nia hiyo waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamevunja sheria na
mkono wa dola hautawaacha.” Alisema.
Waandishi wa habari wakiwa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego. |
Alisema,
serikaliya mkoa na wilaya zote wamejipanga vyema kuhakikisha kuwa amani na
utulivu vinatawala kwa kipindi chote cha upigaji kura hadi utoaji wa matokeo.
Aliwasisitiza
kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kupiga kura kwasababu ni haki na wajibu wa
kila mtu kumchagua kiongozi anayemtaka.
“Nategemea
wale wote waliojiandikisaha watafuata taratibu zote zilizowekwa na tume kwenda
kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria, kwenda kupiga kura kwa utulivu
mkubwa.” Aliongeza.
Aliahidi
kuhimarisha ulinzi kwa waaandishi wa habari ambao watakuwa katika maeneo
mbalimbali ya mkoa katika kutekeleza majukumu yao katika kipindi cha uchaguzi,
ambapo unaandaliwa utaratibu wa kuwapatia vitambulisho na mafulana
yatakayowatambulisha kuwa ni waandishi.
No comments:
Post a Comment