KIFAA KINGINE SIMBA SC KUSAINI KESHO YANGA
KIFAA kingine cha Simba
kimeomba kusajiliwa Yanga kikidai hakina mkataba na klabu yake ya sasa, kwani
kilisaini mkataba wa mwaka mmoja, ambao umemalizika.
Lakini Abdallah Bin Kleb, Mgombea Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga katika uchaguzi wa Julai 15, mwaka huu amemuambia mchezaji huyo kwamba awape ushahidi wa kutosha, ili wajiridhishe na watamsaini kwa sababu wanaheshimu soka yake.
Kesho, mchezaji huyo fundi, aliye kambini timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars- ameahidi kupeleka ushahidi ili naye ajichotee noti zenye alama ya mnyama tembo kama alizokusanya Yondan usiku huu.
Lakini Abdallah Bin Kleb, Mgombea Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga katika uchaguzi wa Julai 15, mwaka huu amemuambia mchezaji huyo kwamba awape ushahidi wa kutosha, ili wajiridhishe na watamsaini kwa sababu wanaheshimu soka yake.
Kesho, mchezaji huyo fundi, aliye kambini timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars- ameahidi kupeleka ushahidi ili naye ajichotee noti zenye alama ya mnyama tembo kama alizokusanya Yondan usiku huu.
BREAKING NEWS;YONDAN AKAMILISHA USAJILI YANGA NA KUKANA KUSAINI SIMBA
Yondan akikamilisha usajili wake Yanga, mbele ya Seif Magari kulia leo usiku, Kushoto ni mtu wa Simba, ambaye alimpeleka mchezaji huyo kumaliza usajili naye akapewa posho yake. |
Akizungumza na BIN ZUBEIRY usiku huu, Yondan amesema Simba wanampakazia kusaini mkataba mpya na anataka wapenzi wote wa soka Tanzania watambue kwamba kuanzia sasa yeye ni mchezaji halali wa Yanga.
"Kesho tutaongea vizuri, nimechoka,"alisema Yondan baada ya kukamilisha usajili wake, mbele ya mgombea Ujumbe wa kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb na swahiba wake Seif Ahmad 'Magari' usiku huu.
"Alikuwa amesaini kila kitu, kuna sehemu alikuwa hajamaliza kujaza leo, ndio amemalizia na ametuhakikishia hana mkataba na Simba, hivyo huyu ni mchezaji ambaye mimi na Seif tunamsajili kwa ajili ya klabu yetu kipenzi, Yanga,"alisema Bin Kleb.
Habari ambazo BIN ZUBEIRY imezipata ni kwamba, Yondan aliikana Yanga awali kwa sababu walimsainisha fomu bila kumpa fedha, lakini leo amepewa Milioni 30 zake taslimu na amemaliza kila kitu.
ROONEY AHAMASISHA WENZAKE ENGLAND
- Don't get your hopes up! Southgate warns fans as England fly out to Krakow
- England head into Euros as world's sixth-best team (well, according to FIFA...)
Wayne Rooney amewataka
wachezaji wenzake wa timu ya taifa ya England, kusahau matokeo mabaya ya nyuma
na kujituma katika michuano ya Euro 2012.
Mshambuliaji huyo yumo kwenye
kikosi cha kocha Roy Hodgson cha Euro 2012, lakini alikuwa mchezaji muhimu
kwenye timu ya England kilichochza fainali mbili za Kombe la Dunia na kukosa
tiketi ya Euro 2008.
MANJI 'AJILIPUA' YANGA, VIGOGO SERIKALINI WAINGIA MITINI
Manji; Mwenyekiti mpya mtarajiwa Yanga |
YUSSUF Mehboob Manji ni
miongoni mwa wanachama 29 wa Yanga waliorudisha fomu leo kwa ajili ya kuwania
nafasi mbalimbali za uongozi katika klabu hiyo, katika uchaguzi uliopangwa
kufanyika Julai 15, mwaka huu, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Kamati ya
Uchaguzi ya Yanga, Francis Kaswahili amesema jioni hii katika Mkutano na
Waandishi wa Habari kwamba, Manji ni miongoni mwa wanachama wanne waliorudisha
fomu kwa nafasi ya Mwenyekiti, wengine wakiwa ni John Jambele, Edgar Chibura na
Sarah Ramadhani.
Katika nafasi ya Makamu
Mwenyekiti, Kaswahili aliyekuwa akizungumza mbele ya mwakilishi wa kamati ya
Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Hassan Chabanga Dyamwale alisema
wamerudisha wanachama watano ambao ni Ally Mayay, Ayoub Nyenzi, Yono Kevela na
Clement Sanga.
Katika nafasi za Ujumbe
waliorudisha ni Lameck Nyambaya, Ramadhani Mzimba ‘Kampira’, Mohamed Mbaraka,
Ramadhani Said, Edgar Fongo, Beda Simba, Ahmad Gao, Mussa Katabaro, George
Manyama, Aaron Nyanda, Abdallah Bin Kleb, Omary Ndula, Shaaban Katwila, Jumanne
Mohamed Mwammenywa, Abdallah Mbaraka, Peter Haule, Justin Baruti na Abdallah
Sharia.
Kaswahili alisema Mkuu wa
Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, Mfanyabiashara Muzamil Katunzi na Katibu
Mkuu wa Wizara ya Madini, Eliakhim Masu hawakurudisha fomu, wakati Isaac Chanzi
pia hakurudisha fomu ya Makamu Mwenyekiti.
Mzee Dyamwale kulia akifafanua jambo kwa Waandishi kumsaidia Kaswahili, kushoto |
Manji alimchukulia fomu Bin
Kleb, ambaye naye leo amemrejeshea fomu Yussuf, akisindikizwa na Seif Ahmad
‘Magari’.
GAMBIA YAWASILI LEO DAR, PROGRAMU YA MAZOEZI STARS HII HAPA
Wachezaji wa Stars |
TIMU ya
taifa ya Gambia, The Scorpion inatarajia kuwasili nchini wakati wowote kuanzia
leo (Juni 6 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa
Stars.
Kamati ya
Maridhiano inayoendesha Chama cha Soka Gambia (GFA) hadi leo mchana ilikuwa
haijatuma taarifa rasmi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) juu ya
ujio wake.
Lakini
vyombo vya habari vya Gambia vimeripoti kuwa timu hiyo ikiwa na wachezaji 23 na
viongozi tisa ilitarajiwa kuondoka huko leo kuja Dar es Salaam tayari kwa ajili
ya mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na washabiki wengi nchini.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa GFA aliyekaririwa na
vyombo vya habari vya nchi hiyo, Bakary Balder, msafara wa timu hiyo utaongozwa
na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Michezo, Malang Jassey. .
Mbali ya
Jassey, viongozi wengine katika msafara huo ni Ofisa Utawala wa timu Modou Sowe,
Kocha Luciano Machini, makocha wasaidizi Peter Bonu Johnson na Lamin Sambou,
Kocha wa makipa Alhagie Marong, mtaalamu wa tiba mbadala (physiotherapist) Pa
Matarr Ndow, Mtunza vifaa Sanna Bojang na Daktari wa timu Kalifa
Manneh.
Wachezaji
ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh,
Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba
Savage, Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan
Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut
Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
Wakati huo
huo: Tanzania
imepanda kwa nafasi sita kwenye orodha ya viwango ya Shirikisho la Kimataifa la
Mpira wa Miguu (FIFA) iliyotolewa leo (Juni 6 mwaka huu) na shirikisho
hilo.
Kwa viwango
vya Mei mwaka huu, Tanzania ambayo timu yake ya Taifa (Taifa Stars) inadhaminiwa
na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa namba 145 hivi sasa imefika nafasi ya 139
ikiwa na pointi 214.
Mei 26
mwaka huu Taifa Stars ilicheza mechi ya kirafiki na Malawi na kutoka suluhu.
Malawi yenye pointi 324 imeporomoka kwa nafasi tano kutoka ya 102 hadi
107.
Ivory Coast
ambayo katika mechi yake ya mwisho Juni 2 mwaka huu iliifunga Taifa Stars mabao
2-0 imeporomoka kwa nafasi moja kutoka ya 15 hadi 16 ikiwa na pointi 943. Hata
hivyo ndiyo inayoongoza kwa upande wan chi za Afrika katika viwango
hivyo.
Aidha, Kiingilio
cha chini ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na
Gambia (The Scorpions) itakayochezwa Jumapili (Juni 10 mwaka huu) Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam ni sh. 3,000.
Watazamaji
watakaolipa kiingilio hicho ni watakaokaa kwenye viti vya rangi ya bluu na
kijani ambavyo ni 36,693 kati ya jumla ya viti 57,558 vilivyopo katika uwanja
huo wa kisasa. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ni sh.
5,000.
Kwa upande
wa VIP C watalipa sh. 10,000 wakati VIP B ni sh. 20,000. Kiingilio kwa jukwaa la
VIP A ambalo linachukua watazamaji 748 tu ni sh. 30,000 kwa mechi hiyo
itakayoanza saa 10 kamili jioni.
Tiketi
zitaanza kuuzwa Jumamosi (Juni 9 mwaka huu) kuanzia saa 2 asubuhi kwenye vituo
vya Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin
Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo na Uwanja wa Taifa. Siku ya mechi pia mauzo
yatafanyika katika vituo hivyo na baadaye kuhamia Uwanja wa Taifa.
PROGRAMU YA TAIFA STARS KWA
MECHI YA GAMBIA
JUMATANO JUNI
6
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja
wa Karume
10.00 jioni Mazoezi-
Uwanja wa Taifa
ALHAMISI JUNI
7
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja
wa Taifa
IJUMAA JUNI
8
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja
wa Taifa
JUMAMOSI JUNI
9
04.00 asubuhi Mkutano na
Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
11.00 jioni Mazoezi- Uwanja
wa Taifa.
BIN KLEB ARUDISHA FOMU YAKE NA MANJI JANGWANI
Anaondoka |
KABURU: TUNAWASHITAKI YANGA
MAKAMU Mwenyekiti wa Simba SC,
Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba wataishitaki Yanga kwa kitendo cha
kuzungumza na beki wao, Kelvin Patrick Yondan kinyume cha kanuni za
usajili.
Akizungumza na BIN
ZUBEIRY dakika chache zilizopita, Kaburu (pichani kushoto) alisema
kwamba kanuni za usajili haziruhusu klabu kuzungumza na mchezaji wa klabu
nyingine bila kupewa ruhusa na klabu yake.
“Kwa mujibu wa fomu tuliyoiona
ambayo Yondan amesaini Yanga, wakati anasaini Yanga alikuwa ana mkataba wa miezi
sita na Simba, kisheria ni makosa na sisi tutawashitaki kwa kukiuka kanuni za
usajili,”alisema.
Inadaiwa Yondan alisaini
Yanga, Novemba mwaka jana- wakati ambao wenyewe (Yanga) wanadai alikuwa hana
mkataba na Simba SC.
Yondan mwenyewe
amekwishakaririwa akikana kusaini Yanga, ingawa fomu ya mkataba imemuumbua leo.
Mapema mwezi uliopita Simba ilisema ilikwishongeza mkataba na
Yondan.
YONDAN HAJATIMIZA MIAKA 18, ANASAINI VIPI MIKATABA?
Yondan kulia akimdhibiti Drogba mjini Abidjan Jumamosi iliyopita, Taifa Stars ilipomenyana na Ivory Coast. |
DROO YA VUMBUA HAZINA YA SBL YAZIDI KUNEEMESHA
BREAKING NEWS; KELVIN YONDAN ATUA YANGA KWA MILIONI 30
Eneo la malipo ya Yondan katika fomu hiyo |
Sehemu ya mkataba wa Yondan na Yanga |
SBL KUMCHAFUA KWA 'DOLARI' MWANAMICHEZO BORA TASWA
MWANAMICHEZO Bora wa Tanzania
kwa mwaka 2011 anatarajiwa kupewa dola za Marekani 8,000 (Zaidi ya sh. Milioni
12 za Tanzania) imetangazwa leo.
Akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam leo, Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti
(SBL), Imani Lwinga alisema uamuzi wa kutoa fedha una lengo la kumpa uhuru
mshindi aweze kufanya mambo anayoyapenda kutokana na zawadi hiyo.
“Nia
ya kutoa zawadi ni kumfanya mshindi aone ana kitu fulani amepata, hivyo safari
hii tumeona tutoe kiasi hicho cha fedha ambacho tunaamini kitakuwa changamoto
kubwa kwa mshindi,” alisema Lwinga.
Alieleza kuwa walipokea ombi
kutoka Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), ambacho ndiyo
kinaandaa tuzo hiyo, kwamba safari hii kuwe na mabadiliko kwa mshindi akabidhiwe
fedha badala ya zawadi ya gari kama ilivyokuwa mwaka jana. Pia mshindi huyo wa
jumla atapewa cheti na kombe.
Lwinga alisema pia Serengti
itatoa zawadi ya Sh. Milioni moja kwa kila mshindi wa michezo mbalimbali ambayo
itazawadiwa katika sherehe hizo zitakazofanyika Juni 14 mwaka huu ukumbi wa
Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Akizungumzia hilo, Katibu Mkuu
wa TASWA, Amir Mhando alisema wanatarajia wanamichezo mbalimbali watapewa tuzo
siku hiyo na kutaja michezo ambayo itapewa tuzo
kuwa ni riadha, wavu,netiboli,kuogelea, tenisi, judo, kikapu, soka, ngumi za
kulipwa, ngumi za ridhaa, gofu wa ridhaa, gofu wa kulipwa, baiskeli, kriketi.
Mingine ni mpira wa mikono, olimpiki maalum, Mchezaji Bora wa Nje
anayecheza Tanzania, Mchezaji Bora Chipukizi, Mchezaji Bora wa Tanzania
anayecheza Nje, Karate, Mwanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2011 na Tuzo ya
Heshima.
Mhando ambaye pia ni Katibu wa
Kamati ya Tuzo alisema Ijumaa watatangaza majina ya wanamichezo wote
watakaowania tuzo hiyo na kuipongeza Serengeti kwa udhamini wao wa kila
mwaka.
Kwa mujibu wa Mhando mwaka
2006 Mwanamichezo Bora wa Tanzania alikuwa Samson Ramadhan aliyezawadiwa sh.
500,000, wakati mwaka uliofuata mshindi ambaye alikuwa Martine Sulle alizawadiwa
Sh.500,000, huku mwaka 2008 mshindi akiwa Mary Naali alizawadiwa sh.750,000.
Wote hao ni wanariadha.
Mshindi wa mwaka 2009 alikuwa mchezaji netiboli
Mwanaid Hassan aliyezawadiwa sh. Milioni moja na mwaka 2010 pia alikuwa Mwanaid
aliyezawadiwa gari aina ya Toyota Cresta GX 100 .
Akizungumza kwenye mkutano
huo, Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto aliwashukuru Serengeti na kusema kuwa ana
matumaini zawadi hizo itakuwa kichocheo cha wanamichezo kufanya vizuri
zaidi.
Tuesday, June 5, 2012
NYOTA SIMBA WAKIJIFUA GYM ASUBUHI YA LEO
Mshambuliaji mpya wa Simba SC, Abdallah Juma akijifua katika gym ya Kelken , Chang'ombe, Dar es Salaam asubuhi ya leo. |
Kocha wa makipa, James Kisaka naye akijifua |
Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu'akizungumza na mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Abdallah Juma akiendelea na mazoezi |
Patrick Mbiyavanga kutoka DRC |
Meneja Vifaa vya Michezo wa Simba, Kessy Rajab naye akijifua |
Mbiyavanga akijifua |
Mbiyavanga |
Amri Kiemba akijifua |
Salum Machaku naye alikuwepo |
AZAM FC KAMBINI IJUMAA SHAMBA
Wachezaji wa Azam |
BAADA ya mapumziko ya
takribani mwezi mmoja tangu kumalizika kwa msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, wachezaji wa Azam FC wameanza kuwasili mjini Dar es Salaam kwa
ajili ya maandalizi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, CECAFA
Kagame.
Meneja wa Azam FC, Patrick
Kahemele ameiambia BIN ZUBEIRY asubuhi hii
kwamba,
kulingana na programu ya
maandalizi, Azam FC wataanza mazoezi Ijumaa wiki hii, Uwanja wa Azam Complex,
Chamazi maalum kwa mashindano hayo yatakayofanyika mwezi ujao mjini Dar es
Salaam.
Kahemele amesema wachezaji
kutoka nje ya Tanzania watawasili mapema wiki hii kwa maandalizi ya makazi kabla
ya kuanza kwa mazoezi hayo yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Azam,
Chamazi.
Alisema usajili kwa wachezaji
ulikwishamalizika kabla ya wachezaji kwenda likizo, hivyo wachezaji wote
waliosajiliwa wataanza mazoezi isipokuwa wale walioko kwenye timu zao za taifa,
Tanzania, Uganda na Zanzibar, ambazo zipo kwenye mashindano mbalimbali ya
kimataifa wikiendi hii.
Alisema programu ya maandalizi
ya Kombe la Kagame, itamalizika siku moja kabla ya kuanza mashindano hayo na
yatakapomalizika, wachezaji watapewa mapumziko ya siku chache kabla ya kuanza
maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.
Kahemele amesema maandalizi
kwa ajili ya VPL yatahusisha pia ziara ya nje ya nchi ya kujiandaa na msimu
mpya, ingawa amesema nchi hiyo itatajwa baadaye.
Kahemele alisema wachezaji
wapya kiikosini Azam msimu huu ni kiungo Mkenya George ‘Blackberry’ Odhiambo na
kipa Deogratius Munishi kutoka Mtibwa Sugar, wakati Aishi Salum, Jackson Wandwi,
Dizana, Ibrahim Rajab Jeba na Joseph Kimwaga, wamepandishwa kutoka akademi ya
Azam.
Kikosi kamili cha Azam FC
kinaundwa; na makipa, Mwadini Ally, Deo Munishi ‘Dida’ Aishi Salum na Jackson
Wandwi, mabeki wa Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samir Haji Nuhu,
Luckson Kakolaki, Said Mourad, Joseph Owino na Aggrey
Morris.
Viongo ni Kipre Bolou,
Abdulhalim Humud, Himid Mao, Salum Abubakar, Abdi Kassim Sadalla, Ramadhani
Suleiman Chombo, Abdulghani Ghullam, Ibrahim Rajab Jeba, Jabir Aziz Stima,
Ibrahim Joel Mwaipopo, Kipre Tchetche, Mrisho Ngassa, Zahoro Pazi, Khamis Mcha
na George Odhiambo ‘Blackberry’ wakati washambuliaji ni Gaudence Mwaikimba, John
Bocco ‘Adebayor’.
Hii
ni mara ya kwanza kwa Azam FC kucheza Kombe la Kagame, baada ya kushika nafasi
ya pili katika msimu uliopita wa Ligi Kuu. Katika Kombe la Kagame mwaka huu,
wenyeji Bara wataingiza timu tatu, Yanga ambao ni mabingwa watetezi, wakati
Simba na Azam wanaingia kwa nafasi za uwakilishi.
Wakati huo huo: Kahemele
amesema kwamba, Azam FC imepanga kuifikisha klabu ya Simba kwenye Kamati ya
Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), iliyo chini ya Mwenyekiti, Kamanda
Mstaafu wa Polisi, kanda maalum Dar es Salaam, Alfred Tibaigana iwapo itaendelea
na mpango wa kumuiba mchezaji wao, Jeba.
Simba na Azam zinamgombea
mchezaji huyo chipukizi, ambaye msimu uliopita alichezea Villa Squad Ligi Kuu
kwa mkopo akitokea kwa wana Lamba Lamba, lakini Wekundu wa msimbazi wanasema
kinda huyo hana mkataba na Azam.
BABU FERGUSON ACHARUKA, AAMUA KUBOMOA BENKI SASA
Tetesi za J'tano magazeti ya
Ulaya
FERGUSON AAMUA KUBOMOA BEKI
KOCHA Sir Alex Ferguson
amemtia kwenye orodha ya wachezaji anaowataka beki wa kushoto wa Everton na
England, Leighton Baines na kiungo wa Tottenham, Luka Modric baada ya kumsajili
kiungo Mjapan, Shinji Kagawa kwa dau la
pauni Milioni 12.
KLABU
ya Napoli ya Italia, pia inamtolea macho Leighton Baines, mwenye umri wa miaka
27, ambaye anauzwa kwa kiasi cha pauni Milioni Milioni 20.
KOCHA
wa West Ham, Sam Allardyce anataka kumsajili winga machachari wa klabu ya
Wolves, Michael Kightly, ambaye ana umri wa miaka 26.
KLABU
za QPR na Sunderland zinamtolea macho kiungo mwenye umri wa miaka 26, aliyewahi
kuzichezea Everton na Portsmouth, Manuel Fernandes, ambaye kwa sasa ni mchezaji
huru.
KLABU
ya Sunderland inatumai kocha wa Aston Villa, Paul Lambert anamtolea macho
mshambuliaji wa Norwich, Grant Holt na hiyo itasaidia mpango wa kumng'ao
mshambuliaji Gabriel Agbonlahor Villa Park kutua Stadium Of
Light.
KIUNGO
wa Swansea, Gylfi Sigurdsson hatarajii kubaki katika klabu hiyo msimu ujao na
amesemaq anataka kumfuata kocha Brendan Rodgers Liverpool.
MCHEZAJI
anayetakiwa na Newcastle, Douglas amesema kwamba The Magpies wanamtaka kwa dhati
- lakini mzaliwa huyo wa Brazil, anayechezea FC Twente pia amesema klabu kubwa
Ulaya nazo zinataka huduma yake.
KIUNGO
Joe Cole atarejea Liverpool baada ya kumaliza muda wake wa kucheza kwa mkopo
Ufaransa, kwa mujibu wa kocha wa Lille, Rudi Garcia.
RONALDO MILELE BERNABEU
MSHAMBULIAJI
wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesema hana mpango wa kurejea Ligi Kuu
England na anataka kucheza hadi mwisho wa maisha yake ya soka katika klabu ya
Bernabeu.
KIUNGO
wa Manchester City, David Silva amewaambia Real Madrid hana mpango na kuhamia
klanu hiyo ya nchini mwake, kwani anafurahia maisha Uwanja wa Ethiad.
KOCHA
wa Tottenham, Harry Redknapp amemtaka Mwenyekiti wa klabu hiyo, Daniel Levy
kufanya haraka kumpa mkataba mpya kama wanathamini yeye kama
kocha.
KOCHA
wa Stoke, Tony Pulis anafikiri mshambuliaji, Peter Crouch atarejea 'mtamu' zaidi
na zaidi msimu ujao, kufuatia kutemwa katika kikosi cha England cha Euro
2012.
KLABU
ya Norwich inatumai kumtambulisha Chris Hughton kama kocha wao mpya - na itatuma
maombi rasmi kwa kocha huyo wa Birmingham katika saa 48 zijazo.
MWENYEKITI
wa Swansea, Huw Jenkins amesema kwamba ipo karibu kumtaja kocha wao mpya, na
amekwishazungumza na Ian Holloway juu ya nafasi hiyo
No comments:
Post a Comment