TENGA: YONDAN HAJA 'DOUBLE SIGN'
Tenga leo |
RAIS wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga amesema kwamba katika sakata la beki wa
kimataifa wa Tanzania, Kelvin Patrick Yondan kudaiwa kusaini mara mbili, lazima
kuna klabu moja imefanya uhuni, maana yake anamtetea beki huyo kwamba hajasaini
mara mbili.
Akijibu swali aliloulizwa
kwenye Mkutano wake na Waandishi wa Habari mchana wa leo, ofisi za TFF, Ilala
mjini Dar es Salaam, Tenga alisema kwamba kulingana na mfumo wa sasa wa usajili
kupitia mtandao, shirikisho lake halihusiki kabisa na usajili na kwamba hilo ni
suala la mchezaji na klabu.
Tenga alisema anaamini klabu
hizo zitamalizana zenyewe kuhusu mchezaji huyo na akasema suala la Yondan
kudaiwa kutoroshwa kambini, Taifa Stars ili akasaini Yanga halina mantiki kwa
sababu mchezaji huyo ni mtu mzima ana akili zake timamu, ila kinachoendelea kwa
sasa ni kelele za kinazi.
Wiki iliyopita, beki Yondan
aliibuka anasaini Yanga, kabla ya klabu yake, Simba aliyoichezea tangu mwaka
2006 kudai bado ina mkataba naye na wapinzani wao hao wa jadi, wamefanya uhuni
kuzungumza naye na kumsajili wakijua hajamaliza mkataba na klabu
yake.
Lakini Yondan mwenyewe alikana
kusaini Simba na kusistiza amesaini Yanga tu, waliompa Sh. Milioni 30 kwa
mkataba wa miaka miwili.
JULIO AKIPIGA KAZI NA JUA LA ADHUHURI
TENGA ASEMA KIM POULSEN NI MTU WA KAZI, AKITOKA NYUMBANI NI SOKONI, HAJUI KUJIRUSHA
Rais wa TFF, Leodegar Chillah Tenga kulia, akizungumza na Waandishi wa Habari leo ofisi za shirikisho hilo, Ilala, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wake, Angetile Osiah akiandika hadidu za rejea. |
RAIS wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga amemwagia sifa kocha wa sasa wa timu ya
soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mdenmark Kim Polulsen kwamba ni mtu wa
kazi na hajui anasa.
Akizungumza na Waandishi wa
Habari katika ofisi za TFF, Ilala, Dar es Salaam mchana wa leo, Tenga alisema
kwamba Kim akitoka nyumbani kwake amekwenda sokoni au kazini na hajui baa wala
sehemu za starehe.
Tenga amesema wana matumaini
makubwa sana na Poulsen kwamba ataifikisha mbali soka ya Tanzania, kwa sababu
hata timu yake ya sasa inaundwa na asilimia kubwa ya vijana walio na wastani wa
umri wa miaka 23 na kwamba hata wakubwa wachache, rika la akina Juma Kaseja na
Haruna Moshi ‘Boban’ wana miaka isiyozidi 27.
Tenga amempongeza Kim na
vijana wake kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Gambia, Jumapili katika mchezo wa
kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil na
ameomba timu hiyo iungwe mkono zaidi ili ifike mbali.
“Tumefika hapa baada ya
jitihada kubwa, ikiwemo kubadilisha kocha. Kupambana na nidhamu, tulimuambia
mwalimu, tafadhali, hakikisha nidhamu, utendaji na jitihada za mazoezi, usiogope
mchezaji, ita mchezaji, nampongeza sana na hakuna jambo la ajabu kwa sababu
tunamjua Kim, ni mtu wa kazi, mwaka mzima”alisema Tenga.
Tenga amesema kwamba tangu
amewasili Kim Tanzania mwaka jana alianzisha programu nzuri ya vijana ambao
amekuwa akiwakusanya kila mwezi na kuwanoa- jambo ambalo limesababisha hivi sasa
awe na timu nzuri ya taifa, baada ya kupandishwa kutoka kocha wa timu za vijana,
hadi ya wakubwa, akirithi mikoba ya Mdenmark mwenzake, Jan Poulsen.
“Wale vijana Sure Boy (Salum
Abubakar) na Damayo (Frank) wamecheza pamoja karibu mwaka mzima timu ya vijana
chini ya Kim na wanaelewana sana. Sasa tumekwishaanza kuandaa utaratibu wa
kuwapatia vijana wataalamu wa saikolojia, ili wawafundishe mambo, namna ya
kuzungumza na Waandishi wa Habari, kuweza kujiami na kadhalika.
“Na
tumeboresha maslahi yao, wakishinda mechi wanapata asilimia 15 ya mapato,
wakitoa sare asilimia tano, ila wakifungwa hawapati kitu. Tutawakatia bima pia,
mambo yatakuwa mazuri,”alisema Tenga.
Taifa Stars hivi sasa inashika
nafasi ya pili katika Kundi C, kwa pointi zake tatu, mabao mawili ya kufunga na
matatu ya kufungwa, nyuma Ivory Coast inayoongoza kwa pointi zake nne, mabao
manne ya kufunga na mawili ya kufungwa, wakati Morocco inashika nafasi ya tatu
kwa pointi zake mbili, mabao matatu ya kufunga na matatu ya kufungwa na Gambia
yenye pointi moja, mabao mawili ya kufunga na matatu ya kufungwa inashika mkia.
Stars Jumapili itahamishia
mawindo yake katika kinyang’anyiro cha tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la
Mataifa ya Afrika mwakani Afrika Kusini kwa kumenyana na Msumbiji mjini Maputo
na inatarajiwa kuondoka nchini Ijumaa. Katika mchezo wa kwanza, timu hizo
zilitoka sare ya 1-1 Dar es Salaam na Stars inatakiwa lazima kushinda ugenini
ili kuitoa Mambas na kusonga mbele.
TOTOZ ZA MISS DAR INTER COLLEGE KATIKA TOUR KI-SURE
Baadhi
ya Warembo wa Miss Dar InterCollege wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya
kutembelea duka la Shear Illusions lililopo Mlimani City jijini Dar es
Salaam.
Picha
ya pamoja kwa warembo.
Mmoja
ya wafanyakazi wa duka la Shear Illusions la Mlimani City jijini Dar akitoa
maelezo kwa warembo wa Miss Dar InterCollege.
Warembo
wakiwa katika nyuso za furaha.
Mfanyakazi
wa dula la Shear Illusions akiwapa maelezo ya namna ya kutumia vipodozi mbali
mbali.
Warembo
wa Miss Dar InterCollege wakiangalia bidhaa mbali mbali zinazopatikana kwenye
duka hilo.
Mrembo
wa Miss Dar InterCollege akivalishwa saa.
Warembo
wa Miss Dar InterCollege wakigawiwa zawadi na mwalimu wao Marlydia Boniface (wa
kwanza kulia) ambazo walipewa mara baada ya kutembelea duka la Shear Illusions
ambao ni wadhamini wa shindano hilo. Picha/www.kajunason.blogspot.com
TENGA AWAPA 'GWALA' TAIFA STARS KUUA NGE
UKUTA WA STARS LAGOS 1980
Monday, June 11, 2012
PSG YATAKA KUIPOKONYA TONGE MDOMONI MAN UNITED, ARSHAVIN ANARUDI ZENIT
Tetesi za Jumanne magazeti Ulaya
ARSHAVIN ANARUDI ZENIT
KLABU ya Zenit St Petersburg
imeanza mazungumzo na Arsenal juu ya kumsajili tena Andrey Arshavin, mwenye umri
wa miaka 31, baada ya kiungo huyo kufanya 'mavituuz' kwenye Euro
2012.
KLABU
ya Paris Saint-Germain nayo imejitosa kwenye mbio za kuwania saini ya nyota wa
Tottenham, kiungo Luka Modric, ikitoa ofa ya dau la pauni Milioni 30 kwa Spurs
kumnasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, raia wa Croatia. Man United nayo
imeonyesha dhamira ya kumsajili nyota huyo.
KIUNGO
'baab kiubwa' wa Everton, Marouane Fellaini, mwenye umri wa miaka 24, anaweza
kutimkia Goodison Park baada ya kusema: "Nataka kucheza Ligi ya Mabinhwa au
Europa League. Msimu uliopita tulimaliza nafasi ya saba nikiwa na Everton, na
hatukufuzu kwenye michuano ya Ulaya, ambayo ilikuwa ni aibu."
KLABU
ya Liverpool inajiandaa kupambana na klabu ya Ligi Kuu ya Ujerumani, Bundesliga,
Schalke katika kumuwania mchesaji huru, Salomon Kalou, mwenye umri wa miaka 26,
ambaye ametemwa Chelsea mwishoni mwa msimu.
KLABU
za Tottenham na QPR inapigania saini ya kipa wa Birmingham, Ben Foster, lakini
mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 31 tayari anatarajiwa kuhamia moja kwa
moja West Brom kwa pauni Milioni 3, ambako alicheza kwa mkopo msimu
uliopita.
KOCHA
wa Sunderland, Martin O'Neill amepania kumbakisha katika klabu hiyo, Stephane
Sessegnon licha ya tetesi zilizozagaa kwamba mustakabali wa kijana huyo wa Benin
mwenye umri wa miaka 26 si mzuri katika klabu hiyo.
WILSHERE HAENDI OLIMPIKI
KOCHA
wa timu ya Olimpiki ya England, Stuart Pearce ameamua kutomjumuisha kiungo wa
Arsenal, Jack Wilshere mwenye umri wa miaka 20 katika kikosi chake cha mwisho,
baada ya kocha wa Washika Bunduki hao wa London, Arsene Wenger kushindwa
kuidhinisha uteuzi huo.
WADI
ya majeruhi yas timu ya soka ya taifa England inayoshiriki Euro 2012 imezidi
kuongezeka idadi ya wagonjwa, baada ya kocha wa makipa Ray Clemence, mwenye umri
wa miaka 63 aliyeichezea Three Lions mechi 61, kutolewa uwanjani jana baada ya
kuumia katika mazoezi ya kujiandaa na mechi Ufaransa, iliyoisha kwa sare ya
1-1.
ZANZIBAR WAREJEA NA SHABA, WAUA 7-2 MECHI YA MWISHO
Wachezaji wa Zanzibar Heroes |
TIMU ya soka ya taifa ya
Zanzibar, Zanzibar Heroes imerejea nchini jana ikitokea Uzbekistan ilikokuwa
ikishiriki michuano ya Kombe la Dunia ya VIVA, inayohusisha nchi ambazo si
wanachama wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na kuambulia Medali ya
Shaba.
Zanzibar ilishinda Medali
hiyo, baada ya Jumapili kuifunga Province ya Ufaransa mabao 7-2 katika mchezo wa
kutafuta mshindi wa tatu.
Awali, katika mchezo wa Nusu
Fainali, Zanzibar ilifungwa mabao 2-0 na Cyprus na Kaskazini, hivyo kukosa
tiketi ya kucheza Fainali.
Katika mechi za Kundi lake A,
Zanzibar ilifanikiwa kutinga Nusu Fainali baada ya kuzifunga Ratia 6-0 na Elaam
3-0.
Wachezaji wa Zanzibar sasa
watarejea kwenye klabu zao, kabla ya kuitwa tena baadaye kwa ajili ya michuano
ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Challenge, ambayo hufanyika
kila mwishoni mwa mwaka.
TRESURE KANU MBIYAVANGA, INJINI MPYA SIMBA SC BALAA
Tresure Kanu Mbiyavanga |
SIMBA imekamilisha malengo waliyokusudia muda mrefu mara tu baada ya kumnasa kiungo wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Tresure Kanu Mbiyavanga kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara na michuano ya kimataifa.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu walikuwa na lengo hilo tangu msimu wa mwaka jana baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho, Moses Basena raia wa Uganda kuvutiwa naye katika mechi Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Motema Pembe.
Simba ilicheza mchezo huo baada ya kutolewa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya 16 bora na Wydad Casablanca ya Morocco na Basena kumtamkia Mbiyavanga anataka kumsajili, ahadi ambayo sasa imekamilishwa, licha ya kutokuwepo kwa kocha huyo ambaye alitimuliwa mapema msimu uliopita.
Katika mchezo huo, Mbiyavanga ambaye ana umbo la wastani, lakini limejengeka kwa mazoezi, alicheza kiungo safi na kuisumbua ngome ya Simba kwa kutoa pasi safi na mipira ya mashuti. Anakumbukwa kwa utambulisho wa nywele zake alizokuwa amepaka rangi nyeupe.
Kutokana na hilo, Mwanaspoti ilifanya naye mahojiano ya kina kufahamu malengo yake na Simba pamoja na historia yake kwa ujumla.
Sababu ya kujiunga na Simba Mbiyavanga anasema amejiunga na Simba baada ya kugundua mipango yao ya soka ni mizuri, lakini pia maslahi yamechangia.
"Nimejiunga Simba kwa sababu ya mipango yao, mimi ni mchezaji naangalia panaponifaa katika mafanikio yangu,"anasema Mbiyavanga ambaye anaishabikia klabu ya Chelsea ya England.
"Viongozi wa Simba na mimi tumekubaliana mambo mengi na ndiyo sababu ya kuondoka Motema Pembe na kuja Tanzania kucheza mpira,"anaeleza Mbiyavanga ambaye pia anawafagilia viungo; Mikel Obi na Michael Essien na anataka kufuata nyayo zao.
"Mimi ni mchezaji na mpira ndiyo kazi yangu niliangalia maslahi, Simba tumekubalina pesa nyigi zaidi ya nilizokuwa napata Motema Pembe.
"Lakini pia wana mpango mzuri katika maendeleo ya soka lao, nimeona katika michuano ya kimataifa na mimi ndiyo ninapenda."
Malengo yake Mbiyavanga ambaye tayari ameshacheza soka la ushindani katika nchi tofauti kama Congo, Afrika Kusini, Rwanda, Gabon na Angola amesema, malengo yake ni kuipa mafanikio Simba kupitia uzoefu wake.
"Malengo ni kuhakikisha naipa mafanikio Simba ili ifanye vizuri katika michuano ya kimataifa na Ligi Kuu Bara," anasema Mbiyavanga aliyeungana na Emmanuel Okwi raia wa Uganda, Felix Sunzu na Mussa Mudde.
Anasema soka yake kwa mashabiki wa Tanzania si mgeni kwao kwa sababu walimshuhudia alipokuwa na Motema Pembe: "Naamini mimi si mgeni kwa mashabiki wa hapa, sina cha kuongea sana wao wasubiri kazi yangu uwanjani nami ninawaahidi sitawaangusha.
Ameongeza kuwa, furaha yake itakamilika pale Simba itakapofanikiwa kutwaa Ubingwa wa Kombe la Kagame msimu huu na yeye akichangia mafanikio hayo.
Alicheza na Mafisango kikosi kimoja Mbiyavanga aliumia alipokuwa akimhadithia, marehemu Patrick Mafisango ambaye ni Mcongo mwenzake aliyekuwa akiichezea Simba, lakini alifariki kwa ajali ya gari mwezi uliopita.
"Sipendi kumzungumzia Patrick kwa sasa, lakini ndiyo imetokea mipango ya Mungu,"anaeleza kwa masikitiko. "Namfahamu Patrick tangu tukiwa wadogo nikicheza naye kikosi kimoja katika timu za vijana, tulikuwa wote viungo na tulisaidiana sana, ninapocheza mbele namba nane na yeye anacheza nyuma namba sita tunapishana.
Sijui ingekuwaje kama tungekutana tena hapa Simba, lakini ni kama nilivyosema ni mipango ya Mungu, tuyaache kama yalivyo,"anaeleza.
Majina yake Mbiyavanga amefafanua ukweli halisi wa majina yake kuwa ni Tresure Kanu Mbiyavanga, licha ya kuwa anatambulika kama Patrick Kanu Mbiyavanga katika wasifu wake kwenye mitandao na watu wanavyomjua hivyo.
"Majina yangu ni Tresure Kanu Mbiyavanga ndiyo sahihi, hilo la Patrick ni kutokana na mashabiki, walinipa nikiwa mdogo wakifananisha na Patrick Viera (mchezaji wa zamani wa Arsenal ya Uingereza sasa yupo benchi la Manchester City),"anaeleza Mbiyavanga.
Nje ya soka Mbiyavanga anasema akiwa nje ya soka anapomaliza majukumu ya mechi, anapenda kutulia nyumbani na familia yake.
"Ninapomaliza mechi au kipindi cha mapumziko, napenda kutulia nyumbani na kucheza na familia yangu huku tukiangalia filamu na kusikiliza muziki,"anasema Mbiyavanga.
Amesema yeye ni mtu wa sala, hutumia pia muda huo wa pamoja kufanya maombi.
Historia yake Mbiyavanga ni wa kwanza katika familia yake yenye watoto nane, wadogo zake ni pamoja na Ilee, Erick, Milet, Shimen, Meryvey, Ritha na Atara.
Yeye ni baba wa watoto wawili, wa kike ni Dayana (4) na wa kiume ni Tirsiana (1) aliowapata kwa mke wake mpendwa aliyemtaja kwa jina la Mam Kanu.
Familia yake; mke na dada yake, Shimen pamoja na watoto wote wanaishi jijini Dar es Salaam.
TRESURE KANU MBIYAVANGA Kuzaliwa: Machi 15, 1989,
Mahali : Kinshasa, Congo.
Klabu: Inter Luanda Club 2006-2008,
APR 2008-2009,
Mangasport 2009-2011
Motema Pembe 2011-2012
Simba 2012-
Taifa: DR Congo
SOURCE: GAZETI LA MWANASPOTI
DROGBA: SAMATTA ANAWEZA KURITHI JEZI YANGU CHELSEA
Mbwana Ally Samatta wa TP Mazembe, akimshughulisha Kolo Habib Toure wa Manchester City |
DIDIER Drogba, akiwa na urefu wa futi sita na mng�ao wa pesa anajitokeza katika korido za vyumba vya kubadilishia nguo katika Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny. Nyuma yake kuna rundo la wachezaji wenzake mastaa.
Nabaki nimeduwaa.Mtu ambaye wiki chache zilizopita alikuwa mbele ya televisheni yangu akiifanyia maajabu Chelsea.
Anatazama jezi yangu iliyoandikwa jina �Tanzania� kifuani. Anatabasamu ananipa mkono ananisalimia kisha ananiambia �karibu Ivory Coast�.Sipati muda wa kuongea naye taratibu anaanza kuondoka nyuma yake kuna Cheikh Tiote, Kader Keita, Yaya Toure, Kolo Toure, Emmanuel Eboue na wengineo.
Wakati anakaribia kuchomoza katika sehemu ya uwanjani, anasita, anageuka nyuma, anatabasamu.Anajisikia aibu kwa sababu anajua uwanja mzima unamsubiri yeye.
Eboue anamsukuma kwa utani.
Ghafla anajitokeza uwanjani huku wenzake wakimfuat anyuma. Uwanja mzima unapagawa, mashabiki wanapiga kelele za kuchanganyikiwa kwa kumuona kwake. Ni kama vile limefungwa bao la fainali katika uwanja wa nyumbani. Na mimi nachanganyikiwa.
Anageuka upande wa kulia anapunga mkono hewani, anageuka upande wa kushoto anapunga mkono hewani.
Mashabiki wanapagawa.Uwanja mzima unachanganyikiwa kumuona mfalme huyu.
Wachezaji wenzake hawana habari.Kila mmoja yuko na mwenzake anapiga stori.
Lakini Drogba anageuzwa kuwa tukio maalumu katika uwanja wa Felix Houphouet-Boigny.
Hatimaye anatembea taratibu kwa maringo kwenda upande wa kulia kuwasalimia mashabiki.
Upande ule wa kulia watu wanachanganyikiwa, wanakanyagana kwa ajili ya kusogea mbele kumuona kwa karibu. Kundi kubwa la askaril inafanya juhudi kubwa kumzunguka. Na mlinzi wake binafsi anasimama nyuma yake.
Kisha anageuza, anavuka uwanja na kwenda upande wa kushoto ambako kama ilivyo kwa Uwanja wa Taifa, kuna televisheni kubwa. Kule nako watu wanapagawa, akili zinawaruka, wanakanyagana kusogea mbele kumuona kwa karibu. Mwishowe anarudi zake kuungana na wenzake.
Si Toure wala Tiote wanaofanya hivyo.Ni yeye peke yake. Ana kitu cha ziada katika ubongo wa watu wa hapa.
Anatimka zake kwenda vyumbani na wenzake, lakini ghafla anakutana na waamuzi wa mechi ambaoni Waraabu.
Anamsalimia mmoja mmoja kwa heshima kubwa na watu wanashangilia. Unajiuliza, wanashangilia nini hasa? Lakini katika akili yangu nafahamu kuwa anacheza mchezo wa akili kwa kuwavuta waamuzi upande wake ili wampe heshima maalumu uwanjani.
Dakika kadhaa baadaye, Mfalme Drogba anafanya jambo la kipuuzi kidogo.Yeye ni nahodha, na amesimama mbele karibu na waamuzi kando ya nahodha wetu, JumaKaseja.
Lakini wakati mwamuzi akiamrisha timu zianze kuelekea uwanjani, Drogba anainama chini na kuanza kufunga taratibu kamba zake za viatu pamoja na plasta ya nje ya soksi.Inachukua dakika tano.
Anafanya hivi taratibu na wachezaji wa timu zote mbili ambao wako tayari kutoka kuelekea uwanjani wanalazimika kumsubiri.
Kaseja kasimama kando na anashangaa jinsi nahodha mwenzake anavyojifanyia mambo yake kwa namna anavyotaka. Timu zinachelewa kutoka uwanjani.
Baada ya kuingia uwanjani, ndani ya dakika tano mpira unaanza.Uwanja mzima unamtazama mtu huyu anayekaribia kulipwa pauni 250,000 kwa wiki pale China.
Haonekani kuwa makini sana kama tunavyomuona darajani. Anacheza huku anatembea.
Muda mchache baadaye anapokea mpira na Aggrey Morris anamkwatua kidogo tu kwa nyuma.
Drogba anajirusha kama amechotwa na katapila. Morris anapewa kadi ya njano.Hapo hapo nakumbuka jinsi Drogba alivyo wasalimia kwa bashasha waamuzi wakati wanaenda kupasha misuli moto.
Muda mchache baadaye inakuwa zamu ya Shaaban Nditi.Anamuingia kwa nguvu nyuma na Drogba anajirusha kama Bruce Lee.
Bahati kwa Nditi hapewi kadi ya njano lakini faulo inapigwa kuelekea lango la Stars. Anapiga mwenyewe,anapaisha, anacheka.Uwanja unapiga makofi.
Kwa dakika zote tisini, Drogba haonekani kuwa makini uwanjani. Na kila akijaribu kuwa makini Kelvin Yondani na Morris wanamdhibiti vilivyo.
Hapumui.Kitu kizuri ni kwamba hana dharau. Anaongea vizuri na akina Yondani uwanjani wakati mech iinaendelea.
Baadaye anafunga kwa kichwa kwa staili ileile ya usiku wa Allianz Arena. Uwanja mzima unazizima.Bao la Kalou lilikuwa zuri kuliko la Drogba, lakini hili linashangiliwa sana kwa sababu limefungwa na Mfalme.
Mpira unakwisha, wachezaji wa Stars wanahaha kupiga naye picha na wala haonyeshi maringo.
Hata mimi najisogeza na kupiga naye picha.Natafuta nafasi ya kuonge naye naikosa, kila mtu anamzunguka yeye, wapiga picha wote wanamzunguka yeye.
Ghafla akachomoka kwenda katika mashabiki wa jukwaa la kushoto ambao wakati ule aliwafanya watu wa mwisho katika salamu zake. Kabla hajafika, kijana mmoja anapenya na kuingia uwanjani kwa kasi akielekea kumkumbatia Drogba.
Maaskari wanamzunguka na kuanza kumchapa.
Drogba anawahi katika tukio na kuamrisha askari wasimpige. Anamkumbatia na askari wanatulia kama vile wamepewa amri ya kijeshi.
Anakimbia na kijana huyo kwenda kumpandisha ngazi za jukwaani na kifupi ni kwamba anaokoa maisha yake kutoka kwa askari wenye hasira ambao majuzi tu walikuwa wakishiriki vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Baada ya hapo uwanja mzima unamshangilia.Anateka kila kitu uwanjani.Hakuna anayejishughulisha naTiote, Gervinho wala Toure ambaye wiki chache tu zilizopita kawapa ubingwa Manchester City.
Katika mkutano na waandishi wa habari simuoni Drogba. Nilitazamia angekuwepo, lakini anakuja Solomoni Kalou na kocha wake,Sabri Lamouchi.
Wanaongea lakini na mimi akili yangu imetekwa na Drogba.
Bahati nzuri ukumbi wa waandishi wa habari uko upande ule ule ambao kuna vyumba vya wachezaji wa Ivory Coast.
Namsikiliza Kalou haraka haraka kisha kocha wake. Wote wanaisifia Tanzania, wote wanamsifia Mbwana Samatta.Napata kitu cha kuandika kisha naondoka kumnyemelea Drogba.
Ghafla wachezaji wa Ivory Coast wanaanza kujitokeza kwenda nje kupanda basi. Wanapita wote akina Eboue najifanya siwaoni, ghafla anatokeza mfalme.
Hii ndio fursa pekee ya kupata neno kutoka kwake.Namuwahi fasta kabla waandishi wengine hawajanusa.
Namuuliza ameionaje Stars, anasema imecheza bonge la mechi na hakutegemea hivyo. Namuuliza nan iamekuvutia,anajibu �yule aliyevaa jezi namba 10�.
Anamwagia sifa Samatta na mwishowe anatania kwa kusema �anawezakwenda Stamford Bridge kuvaa jezi yangu, mimi naondoka, mwambie aende�. Moyo wangu unafarijika.Nataka kumuuliza kitu, kumbe kundi la waandishi limeshatuzunguka.Mmoja ananiwahi na kumuuliza Kifaransa, mwingine tena anauliza hapo hapo.
Tulikuwa wawili, lakini ghafla tukajikuta tuko 40.Najichomoa kundini.
Walinzi wanamzuia asijibuma swali.Anaondolewa kwa nguvu. Nageuka kumtazama anavyotokomea, natabasamu.Hapo hapo nakumbuka ile penalti yake ya mwisho pale Allianz Arena. Mfalme anatoweka machoni kwangu!
No comments:
Post a Comment