UJERUMANI YAIBWAGA UHOLANZI
MABAO mawili ya
Mario Gomez yameipa Ujerumani ushindi wa 2-1 dhidi ya Uholanzi katika Euro 2012
usiku huu
MABAO mawili ya
Mario Gomez yameipa Ujerumani ushindi wa 2-1 dhidi ya Uholanzi katika Euro 2012
usiku huu
URENO YAIPIGA 3-2 DENMARK KWA MBINDE
RASMI; DAMAYO AANGUKA MIAKA MIWILI JANGWANI JION HII
HATIMAYE klabu Yanga ya Dar es
Salaam, leo imefanikiwa kumsainisha mkataba wa miaka miwili, kiungo mkabaji wa
JKT Ruvu ya Pwani, Frank Damayo (pichani kushoto) anayechezea timu
ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
Yanga imezipiga bao Simba na Azam FC, ambazo pia zilikuwa zinawania saini ya chipukizi huyo. Zoezi hilo limefanikishwa jioni ya leo kwa jitihada za pamoja za Seif Ahmad 'Magari' na Abdallah Ahmad Bin Kleb jioni hii.
"Tumemalizana na Damayo, tumesaini naye mkataba wa miaka miwili jioni hii,"alisema Seif kuiambia BIN ZUBEIRY. Jana kutwa nzima Yanga walikuwa wanakwenda mbio kusaka saini ya mchezaji huyo na haimaye wamefanikiwa leo. Seif amesema kabla ya kuzungumza na mchezaji huyo, walianza kwanza kuzungumza na klabu yake, ikawaruhusu kufanya naye mazungumzo.
Damayo alicheza soka ya maana katika mechi ya Jumapili ya Taifa Stars na Gambia, Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil. Katika mechi hiyo, ambayo Stars ilishinda 2-1, Damayo alicheza kwa maelewano makubwa na beki Kelvin Yondan wa Simba, ambaye pia amesaini Yanga- ingawa na klabu yake inasistiza ina mkataba naye.
Yanga imezipiga bao Simba na Azam FC, ambazo pia zilikuwa zinawania saini ya chipukizi huyo. Zoezi hilo limefanikishwa jioni ya leo kwa jitihada za pamoja za Seif Ahmad 'Magari' na Abdallah Ahmad Bin Kleb jioni hii.
"Tumemalizana na Damayo, tumesaini naye mkataba wa miaka miwili jioni hii,"alisema Seif kuiambia BIN ZUBEIRY. Jana kutwa nzima Yanga walikuwa wanakwenda mbio kusaka saini ya mchezaji huyo na haimaye wamefanikiwa leo. Seif amesema kabla ya kuzungumza na mchezaji huyo, walianza kwanza kuzungumza na klabu yake, ikawaruhusu kufanya naye mazungumzo.
Damayo alicheza soka ya maana katika mechi ya Jumapili ya Taifa Stars na Gambia, Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil. Katika mechi hiyo, ambayo Stars ilishinda 2-1, Damayo alicheza kwa maelewano makubwa na beki Kelvin Yondan wa Simba, ambaye pia amesaini Yanga- ingawa na klabu yake inasistiza ina mkataba naye.
BREAKING NEWS; AZAM WAJENGA MPYA WA KISASA KAMA TAIFA
Uwanja wa sasa wa Azam |
KLABU ya Azam FC, imeanza
ujenzi wa Uwanja mpya mkubwa na wa kisasa wenye hadhi sawa na Uwanja mpya wa
Taifa wa Dar es Salaam, ambao ndio utakuwa ukitumika kwa mechi mbalimbali za
timu hiyo, wakati Uwanja wa sasa utakuwa kwa ajili ya mazoezi tu.
Habari za ndani kutoka Azam
(siyo kwa Patrick Kahamele), ambazo BIN ZUBEIRY imezipata zimesema
kwamba tayari hatua za awali za ujenzi zimeanza katika eneo lile lile la
Chamazi.
“Tunajenga Uwanja mwingine
mkubwa, huo utakuwa kama Uwanja wa Taifa. Utakuwa unatumika kwa mechi zetu zote
za kitaifa na kimataifa, huu Uwanja wa sasa utakuwa kwa ajili ya mazoezi tu na
mechi za timu za vijana,”kilisema chanzo chetu kutoka Azam.
Azam FC wanaelekea kupiga
hatua nyingine kubwa na kuzidi kuzipiga bao, timu kongwe nchini Simba na Yanga-
kwani hadi sasa tayari hiyo ndio klabu pekee nchini yenye Uwanja wake wenye
kukidhi vigezo.
Simba iliyoanzishwa zaidi ya
miaka 70 iliyopita, bado haina Uwanja hata wa wachezaji wake japo kupigia
danadana, wakati wapinzani wao wa jadi, timu kongwe zaidi nchini kwa sasa, Yanga
ina Uwanja wa Kaunda, ambao umetelekezwa na upo katika hali
isiyotazamika.
Ingawa historia inasema Yanga
ilizaliwa mwaka 1935 na Simba mwaka 1936, lakini ukizama ndani utagundua kwamba,
huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa utani na upinzani wa jadi, baina ya miamba hiyo ya
soka nchini.
Kulikuwa kuna timu inaitwa New
Youngs, ambayo mwaka 1938 ilisambaratika na baadhi ya wachezaji wake wakaenda
kuunda timu iliyokuwa ikiitwa Sunderland, ambayo hivi sasa inajulikana kama
Simba.
Kabla ya kutokea vurugu
zilizoisambaratisha New Youngs, vijana wa Dar es Salaam walikuwa wana desturi ya
kukutana viwanja vya Jangwani kufanya mazoezi na baada ya muda wakaamua kuunda
timu yao, waliyoipachika jina Jangwani.
Ndani ya kipindi kifupi tu,
timu hiyo iliteka hisia za wengi, waliojitokeza kujiandikisha uanachama wa klabu
hiyo. Miongoni mwa waliovutika na uanachama wa klabu hiyo ni Tarbu Mangara (sasa
marehemu) na ilipofika mwaka 1926, walifanya mkutano wa kwanza katika eneo
ambalo hivi kuna shule ya sekondari ya Tambaza.
Miongoni mwa yaliyojadiliwa
kwenye mkutano huo ni kuiboresha timu hiyo, ambayo wachezaji wake wengi walikuwa
wafanyakazi wa Bandarini na mashabiki wake wengi walikuwa wabeba mizigo wa
bandarini.
Baada ya mkutano huo, timu
hiyo ilibadilishwa jina na kuwa Navigation, iliyotokea kuwa moto wa kuotea mbali
katika timu za Waafrika enzi hizo, kabla ya uhuru wa Tanganyika. Timu kama
Kisutu, Kitumbini, Gerezani na Mtendeni zilikuwa hazifui dafu kwa wana Jangwani
hao.
Ikiwa inatamba kwa jina la
Navigation, wanachama wa timu hiyo walikuwa wakitembea kifua mbele na kuwatambia
wapinzani, kwamba wao ndiyo zaidi. Kwa sababu katika kipindi hicho, Italia
ilikuwa inatamba kwenye ulimwengu wa soka, wanachama wa timu hiyo nao waliamua
kuibadilisha jina timu yao na kuiita Taliana.
Taliana ilipata mafanikio ya
haraka na haikushangaza ilipopanda hadi Ligi Daraja la Pili Kanda ya Dar es
Salaam, mwanzoni mwa miaka ya 1930. jina la Taliana waliamua kuachana nalo
mapema, kabla ya kuingia kwenye ligi hiyo, hivyo wakaanza kujiita New
Youngs.
Lakini kila ilipokuwa
ikibadilisha jina, ilikuwa ikifanya vitu pia, kwani wakiwa na jina la New
Youngs, waliweza kutwaa Kombe la Kassum, lililoshirikisha timu mbalimbali za Dar
es Salaam.
Hatimaye ukawadia mwaka mbaya
kwa New Youngs, 1938 wakati baadhi ya wachezaji walipojitoa na kwenda kuanzisha
Sunderland. Kwa sababu hiyo, waliobaki wakaamua kubadili jina na kuwa Young
Africans, jina ambalo mashabiki wake wengi walishindwa kulitamka vizuri hivyo
kujikuta wakisema Yanga.
Azam FC, ilianzishwa mwaka
2004 tu na kikundi cha wafanyakazi wa kampuni ya Mzizima Flour Mill, kampuni
tanzu ya Bakhresa, makao yake makuu yakiwa Barabara ya Nyerere, Dar es
Salaam.
Lengo la wafanyakazi hao wa
kampuni inayomilikiwa na Said Salim Bakhresa, awali ilikuwa ni kucheza kwa ajili
ya kujiburudisha, baada ya kazi.
Lakini baada ya kuona wana
timu nzuri, Oktoba 16, mwaka 2004, waliisajili rasmi kwa ajili ya kushiriki Ligi
Daraja la Nne, wakitumia jina la Mzizima FC.
Baadaye Mkurugenzi Mkuu wa
makampuni ya Bakhresa, Abubakar Bakhresa, aliona ni vyema timu hiyo ihusishe
wafanyakazi wa kampuni zote za Bakhresa, na kutumia jina la moja ya bidhaa zao
kubwa, Azam.
Kampuni nyingine za Bakhresa
ni Food Products Ltd, Azam Bakeries Ltd, Omar Packaging Industries Ltd na
kadhalika. Wazo lake lilikubaliwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo, ndipo timu
hiyo ikaanza kuitwa Azam SC, badala ya Mzizima. Lakini baadaye Juni 11, mwaka
2007, ilibadilishwa jina tena na kuwa Azam FC.
Azam ilikwenda kwa kasi nzuri
kuanzia Daraja la Nne na hadi mwaka 2008, ilifanikiwa kucheza Ligi Kuu, na msimu
uliopita pamoja na kutwaa Kombe la Mapinduzi mbele ya vigogo wa soka nchini
Simba na Yanga, pia ilikaribia kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu- baada ya kuzidiwa na
Simba waliobuka mabingwa, huku wao wakishika nafasi ya pili mbele ya waliokuwa
mabingwa watetezi, Yanga.
Kwa
mara ya kwanza, Azam mwakani itapeperusha bendera ya Tanzania kwenye michuano ya
Afrika, ikicheza Kombe la Shirikisho.
No comments:
Post a Comment