Saturday, April 14, 2012

Saturday, April 14, 2012

WALCOTT AWAKUMBUSHA KITU ARSENAL HAWAWEZI KUSAHAU MSIMU HUU

Walcott katikati ya Song kulia na Sagna kushoto
MUINGEREZA Theo Walcott amesema kwamba Arsenal ilianza ligi rasmi msimu huu baada ya kuifunga 5-3 Chelsea, Oktoba 29, mwaka jana.
Ushindi huo ulikuja baada ya Arsenal kuuanza msimu vibaya ikiwemo kutandikwa mabao 8-2 na Manchester United.
Walcott alicheza kwa kikubwa sana siku hiyo akiwa na jezi ya Arsenal kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, na akafunga bonge la bao lililodhihirisha kipaji na umahiri wake.
Dogo huyo wa umri wa miaka 23 amezungumzia mechi hiyo kama moja ya mechi ambazo hawezi kuzisahau msimu huu na ndiyo iliyowafufua.
"Mechi na Chelsea ilikuwa hatua kubwa kwa sababu tulijua tuko vizuri [wakati huo]," alisema Walcott.
"Kwenda nje ya nyumbani na kufunga mabao mengi, ilikuwa ni kila kitu. Ilikuwa babu kubwa jinsi tulivyoshirikiana, baada ya mechi (furaha yake) ilikuwa kama tumetwaa ubingwa wa Ligi Kuu.
"Huo ni moja ya wakati ambao tunataka utokee tena na bahati nzuri umetokea tena katika wiki za karibuni."
Walcott amefunga mabao manane katika timu yake hadi sasa msimu huu, mawili kati ya hayo alifunga kwenye ushindi wa 5-2 dhidi ya Spurs, Februari.

GUARDIONA AMTEMBELEA ABIDAL HOSPITALI, AKAA NAYE DAKIKA 20

Abidal
KOCHA wa Barcelona, Pep Guardiola amemtembelea beki Eric Abidal hospitali jana baada ya mchezaji huyo kufanyiwa upasuaji wa ini mapema wiki hii.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ufaransa amepigwa kisu na inasemekana anaendelea vizuri baada ya zoezi hilo gumu.
Guardiola alitumia muda wa dakika 20 akiwa na Abidal na familia yake, na amemtakia mchezaji huyo kupona haraka katika upasuaji huo wa pili juu ya tatizo hilo.
Rais wa Barcelona, Sandro Rosell alisema kwamba Mfaransa huyo anaendelea vizuri.
Kwa sasa klabu hiyo Catalans inachuana vikali na wapinzani wao, Real Madrid katika mbio za ubingwa wa La Liga na leo inacheza na Levante

MAN CITY YAUA 6-1, TEVEZ APIGA TATU

Tevez
MUARGENTINA Carlos Tevez amepiga hat-trick akiisaidia Manchester City kuitandika Norwich 6-1 na kupunguza pengo la pointi wanazozidwa na Manchester United hadi mbili katika Ligi Kuu ya England. United itacheza na Aston Villa kesho.
Tevez alifunga dakika ya 18, 73 na 80 wakati mabao mengine yalitupiwa na Aguero dakika ya 27 na 75 na Johnson dakika ya 90, wakati la wapinzani wao lilifungwa na Surman dakika ya 51.
Licha ya kocha wa City, Roberto Mancini kukata tamaa ya kuwakamata watoto wa Sir Alex Ferguson msimu huu, lakini ushindi huu bila shaka hata yeye unamfanya aone inawezekana.

LIVERPOOL WATINGA FAINALI KOMBE LA FA

LIVERPOOL  imetingia fainali ya Kombe la FA, baada ya kuwafunga wapinzani wao wa jadi, Everton mabao 2-1, mabao ya Luis Suarez dakika ya 62 na Andy Carroll dakika ya 87, wakati la wapinzani wao lilifungwa na  Jelavic dakika ya 24. Mchezo huo umemalizika hivi punde tu kwenye Uwanja wa Wembley. Hapa ni Carroll anaonekana akifunga bao la ushindi kwa kichwa

No comments: