|
Daktari bingwa wa upasuaji kutoka MOI, Mwanahabasi Suwed. |
Na Juma Mohamed, Mtwara.
Baadhi ya
wazazi wenye watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi katika
mikoa ya Lindi na Mtwara wameshauriwa kuacha tabia ya kuwafungia ndani watoto
wao na baadala yake wawapeleke hospitalini kwa matibabu wanaposikia ujio wa
madaktari bingwa wakutibu magonjwa hayo.
Wakizungumza
katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mtwara, Ligula, baadhi ya kina mama wenye
watoto hao waliobahatika kupata huduma za madaktari bingwa kutoka hospitali ya
Taifa Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI), walisema awali ugonjwa huo
uliwakatisha tamaa na kudhani hauwezi kutibika.
“Baada ya
kukaa ndani mtoto yule ndio kuna siku nikaona kichwa kinazidi kuongezeka tu na
kinaendelea tu..tukawa tumekaa ila juzi ndio tukasikia kuna watu hao wametoka
huko Dar (Dar es Salaam) wamekuja Mtwara, ndio tukasema twende tukajaribu huko mamaangu
akakubali tukaja nae hadi hapa wametupokea vizuri na hivi ninavyosema mtoto
wangu anaendelea vizuri..” alisema Salma Ally, mkazi wa Lindi.
Salma Ally, mkazi wa Lindi ambaye mtoto wake amepatiwa matibabu ya tatizo la kuwa na kichwa kikubwa. |
Naye, Zenat
Ally mkazi wa Mtwara, alisema aliamua kufika hospitalini hapo baada ya kusikia
matangazo juu ya kuwepo kwa madaktari bingwa wanaotoa matibabu hayo, ndipo
akaona amuwahishe mwanae apate matibabu.
Daktari
bingwa wa upasuaji wa vichwa, migongo na mishipa ya fahamu kutoka MOI,
Mwanahabasi Suwed, alitoa ushauri kwa wanawake walio katika umri wa kushika
ujauzito namna ya kujikinga ili kuhepuka na kujifungua watoto wenye matatizo
hayo.
“Mara nyingi
hili tatizo linasababishwa na ukosefu wa madini yanaitwa Phoric Acid ambayo
tunayapata kwenye mboga za majani za kijani na matunda, kwahiyo tunashauriwa
wanawake wote ambao wapo kwenye umri wa kuweza kushika mimba kuweza kupata hivi
vidonge ambavyo nadhani kidonge kimoja vinauzwa sh. 50 kuwa unakunywa kila siku
pamoja na kula mboga za majani na matunda..” alisema.
Afisa habari
wa GSM Foundation ambao ndio wafadhili wa mpango wa kutoa huduma hizo Khalfan
Kiwamba alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kupata matibabu hayo.
Hata hivyo,
muitikio kwa wakazi wa Mtwara katika kujitokeza kupeleka watoto kupata matibabu
hayo umetajwa kuwa ni mdogo tofauti na matarajio ambapo ni watoto sita pekee
ndio waliopata matibabu hayo kwa muda siku Nne huku matarajio yakiwa ni watoto
40.
No comments:
Post a Comment