Wednesday, June 15, 2016

Vyombo vya usalama Mtwara vyatakiwa kukomesha uhalifu mitandaoni.





Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, akifungua semina ya kutoa elimu kwa umma juu ya ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)

Wadau wa huduma za mawasiliano wakifuatilia somo




Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego akifuatilia somo juu ya elimu kwa umma kuhusu ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Kulia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Henry Mwaibambe na kushoto ni mkuu wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally.


Mwanasheria wa Tume ya Ushindani wa Haki (FCC) Khadija Ngasongwa, akionesha aina ya simu bandia katika semina ya kutoa elimu kwa umma juu ya ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)



Maboksi ya simu bandia


Picha ya pamoja, mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, mkuu wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally na kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Henry Mwaibambe na wadau wa mawasiliano mkoani Mtwara.


Na Juma Mohamed, Mtwara.
Wasimamiaji wa sheria za mawasilino mkoani Mtwara wametakiwa kuwachukulia hatua haraka watu watakaobainika kwenda kinyume na kuvunja sheria za matumizi sahihi ya mawasiliano, ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya simu za kiganjani.
Akizungumza katika ufunguzi wa semina ya siku moja ya kutoa elimu kwa umma juu ya ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, alisema hakuna sababu ya vyombo vya usalama kuwa na kigugumizi katika kuwachukulia hatua watakaobainika kuvunja sheria za matumizi ya mawasiliano.

Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego



“Lengo la kusajili simu ni kutaka kutambuana, kudhibiti matukio mabaya na ya kihalifu pamoja na kuhimarisha hali ya usalama..tunatumia mawasiliano kupotosha habari na kuleta hali ya mtafaruku kwa wananchi kitu ambacho ni kibaya..” alisema na kuongeza;
“wasimamiaji wa sheria, kusiwe tena na kigugumizi tunapoanza kutambuana..jeshi la polisi lisimame katika kutenda haki ili kudumisha usalama..” aliongeza.

Wdau wa huduma za mawasiliano mkoa wa Mtwara wakiwa katika semina ya kutoa elimu kwa umma juu ya ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)



Aidha, alisema wizi wa simu sasa utakua mwisho kwasababu mtu akiiba haitamsaidia kwani mwisho wake atakamatwa, huku akiamini baada ya semina hiyo kila mtu ataelimika juu ya matumizi ya simu.
Akiwasilisha mada ya kwanza katika semina hiyo, Mhandisi wa mfumo rajisi wa namba za utambulisho wa simu kutoka TCRA, Imelda Salum, alisema kila simu ya kiganjani ina namba pekee ya utambulisho ambayo inatambulika kama International Mobile Equipment Identity ( IMEI) ambayo haifanani na nyingine duniani kote.

Mwanasheria wa Tume ya Ushindani wa Haki (FCC) Khadija Ngasongwa, akionesha aina ya simu bandia katika semina ya kutoa elimu kwa umma juu ya ufahamu wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyoendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)



Alisema, namba hiyo inamsaidia mwenye simu katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na usalama wa kifaa chake, kutambulika kwa mamlaka husika na vyombo vya usalama.
Alisema kupitia namba hizo, inamsaidia mmliki kuweza kutambua kama simu yake ni bandia au laa iwapo atahakiki kwa kunakili namba hizo ambazo atazipata kwa kuangalia ndani simu baada ya kuiondoa betri au kwa kubonyeza alama ya *#06# kisha zitajitokeza tarakimu 15 alafu atazituma kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) kwenda namba 15090.

No comments: