Mkuu wa wilaya ya Tandahimba, Emmanuel Luhahula. |
Fundi akiendelea na ujenzi wa jengo la maabara, sekondari ya Tandahimba |
Juma Mohamed, Mtwara.
Ikiwa
zimebaki wiki mbili kabla ya kufikia mwisho wa muda uliotelewa na serikali kwa
halmashauri zote nchini juu ya utatuzi wa uhaba wa madawati kwa shule za msingi
na sekondari, halmashauri ya wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara imekamilisha
agizo hilo kwa asilimia 100 kwa shule za msingi.
Mkuu wa wilaya
hiyo, Emmanuel Luhahula alisema awali halmashauri hiyo ilikuwa ikikabiliwa na
uhaba wa madawati 7,453 kwa shule zote za msingi na sekondari ambapo tayari ya
shule za msingi yamekamilika huku wakibawa na zoezi la kukamilisha madawati
zaidi ya 500 kwa shule za sekondari.
“Mpaka hapa
sasa hivi tunapoongea madawati kwa shule za msingi tulishakamilisha yote,
hakuna dawati hata moja ambalo tunadaiwa kilichobaki ni kuanza kuyasambaza kwa
shule husika..kwa sekondari bado madawati sina takwimu sahihi hapa lakini ni
kama Miatano na kitu au miasaba hivi..” alisema.
Alisema,
madawati yaliyobaki kwa sekondari yapo katika hatua za mwsho ili yakamilike ambapo
licha kukabiliwa na uhaba wa mbao lakini aliahidi kukamilisha kabla ya June 30
mwaka huu.
Sambamba na
utatuzi wa changamoto ya madawati, halmashauri hiyo inaendelea na utekelezaji
wa agizo la Rais wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete, la ujenzi wa Maabara ya
Sayansi kwa shule za sekondari ambapo wanafunzi walielezea adha wanayoipata kwa
kukosa Maabara.
“Masomo yapo
matatu, na yote yanahitaji ‘practical’ (Mafunzo kwa vitendo) kwahiyo wanafunzi
wanapoingia Maabara kufanya ‘practical’ vipindi vinagongana kwahiyo inawapa
tabu sana walimu kwasababu mwalimu wa Physics anataka kufanya ‘prctical’ katika
‘laboratory’ hiyohiyo na mwalimu wa Kemia anataka afanye hivyo hivyo kwahiyo inatupa
changamoto sana wanafunzi pale tunaposoma..” alisema Mwanahawa Hussein,
mwanafunzi wa Sekondari ya Tandahimba.
Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Tandahimba, Mwanahawa Hussein. |
Kwa upande
wake, mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Mzega Twalib, alisema ujenzi wa Maabara
unaendelea katika halmashauri yake ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali ya
awamu ya Nne huku akiahidi kukamilisha ifikapo mwezi Septemba mwaka huu.
“Vikao vya
halmashauri vilitenga fedha sh. Milioni 300 kwa ajili ya kupeleka kwenye
Maabara kwahiyo tulipeleka kwenye shule zote 28 ili kufanya ‘finishing’ ya
angalau chumba kimoja ili viweze kutumika kwahiyo ndio ujenzi ambao unaendelea..lakini
pia halmashauri inampango wa kupeleka fedha nyingine takribani sh. Milioni 600
katika mwaka huu wa fedha unaoanzia Julai ili kwa vyovyote itakavyokuwa ifikapo
mwezi Septemba tuwe tumekamilisha zoezi la ukamilishaji wa ujenzi wa Maabara..”
alisema.
Halmashauri
hiyo inatarajia kutumia kiasi cha sh. Bilioni 2.1 ili kukamilisha ujenzi huo
kwa maabara zote katika shule zote 28 za sekondari.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Tandahimba, Mzega Twalib |
No comments:
Post a Comment