Wednesday, June 15, 2016

Wabunge Wanane Jubilee na Cord Kenya kufikishwa mahakamani.


Hakimu mkuu wa mahakama ya Milimani- Nairobi, Daniel Ogembo (PICHA: MTANDAO)


Na Mack Kemoli, Nairobi.

Mahakama Nairobi imeamuru wabunge wanane waliokamatwa kwa kutoa matamshi ya uchochezi wanashikiliwa na jeshi la polisi mpaka Ijumaa juni 17 mwaka huu, wakati kesi yao itasikilizwa tena.

Hakimu mkuu wa mahakama ya Milimani- Nairobi, Daniel Ogembo alisema kwamba wabunge hao wabaki korokoroni  huku idara ya upepelezi ikikusanya ushahidi wa kutosha wa kuwashtaki.

Akikubaliana na ombi la mwendesha mashtaka, Sajenti Gilbert Kitalia , hakimu huyo aliamua washilikiwe katika vituo vya polisi vya Kilimani, Gigiri, Pangani, Kileleshwa, Muthangari na Muthaiga hadi ijumaa watakapofikishwa mahakamani.

Wabunge hao ,Moses Kuria (Gatundu South) , Ferdinand Waititu (Kabete),  Kimani Ngunjiri (Bahati) wote wa mrengo wa Jubilee unaoongozwa na wenzao, Johnstone Muthama (Machakos), Junet Mohamed (Suna East), Aisha Jumwa (Kilifi), Florence Mutua (Busia) na Timothy Bosire (Kitutu Masaba) wa mrengo wa cord( upinzani), walikuwa wamekamatwa awali na kupelekwa kwenye idara ya upelelezi ambapo mkuu wa police nchini Kenya Boinnet aliamuru wasiachiliwe.

Kisa cha wabunge hao kukamatwa kilianza Jumapili ambapo vyombo vya habari vilimnukuu mbunge wa Gatundu South, Moses Kuria - anapotoka rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta akisema kwamba Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga anasumbua na kwamba anastahili apigwe risasi ili nchi iendelee.
Matamshi hayo hayakuchukuliwa vyema na wabunge wa upinzani wakiongozwa na mbunge Junnet Mohammed aliyesema kwamba hawatishwi na  serikali na kwamba hao (upinzani) wana uwezo wa kutisha hata kuua.
Wabunge zaidi waliweza kutoa vitisho kwa wenzao wa aidha upande wa serikali au upinzani.
Kisheria, endapo wabunge hao watapatikana na hatia, huenda wakafungwa kifungu kisichozidi miaka mitatu au kulipa faini ya Ksh. Million moja ( sawa na milioni 20 za Tanzania) kila mmoja.
Kamau Kuria alikuwa amedai kwamba maandamano ya kila jumatatu ya wafuasi wa Cord yalikuwa yanatatiza nchi, huku muungano wa Cord nao ukishiikilia kwamba maandamano hayo yataendelea hadi makamishama wa tume ya uchaguzi watakapoondoka ofisini.
Maandamano hayo yamesababisha uharibifu mwingi wa mali na watu sita kupoteza maisha yao.
 Aidha, Cord inadai kwamba tume hiyo ilipendelea serikali wakati wa uchaguzi mdogo wa County ya Kericho na kwamba hawana imani nayo huku uchaguzi wa uraisi ukitarajiwa kufanyika mwakani.
Mrengo wa upinzani umesema utatoa taarifa kesho alhamisi kuhusu msimamo wao dhidi ya maadnamano hayo.
Hata hivyo serikali na upinzani wamekubaliana kukaa pamoja na kutafuta suluhu, baada ya viongozi wa kidini nchini Kenya kuingilia kati mzozo huo ambao ulikuwa unaendelea kushika kasi.
Viongozi hao wametaka serikali na upinzani utoe wawakilishi saba kila upande kwa mazungumzo ya kutatua swala hilo.

No comments: