Thursday, April 28, 2016

Halmashauri Mtwara zapitisha mpango wa pamoja wa matumizi ya ardhi.


Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kikao cha kujadili na kupitisha mpango kabambe wa matumizi ya ardhi kwa halmashauri za wilaya ya Mtwara na manispaa ya Mtwara Mikindani.


Fatma Ally


Na Juma Mohamed, Mtwara.

HALMASHAURI ya wilaya ya Mtwara pamoja na manispaa ya Mtwara Mikindani zimepitisha mpango wa matumizi ya ardhi utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka 20, ambapo yametengwa maeneo maalumu kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa kikao cha kupitisha mpango huo, kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Rashidi Mtima, alisema mpango huo ndio utakuwa nguzo ya kisheria katika matumizi ya ardhi katika halmashauri hizo huku ukilenga kuhakikisha kuwa Mtwara inahudumia shughuli za gesi.
Alisema, mpango huo umetenga maeneo matano kutoka katika halmashauri hizo kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo na kwamba miongoni mwa hayo ni pamoja na eneo la Ziwani litakalokuwa maalumu kwa ajili ya kuhudumia masuala ya gesi na mafuta.
“Tumezungumza pale kwamba vision ya Mtwara iwe mji bora katika kanda hii ya bahari ya Hindi, mji bora na kama tunavyojua tunatarajia vilevile Mtwara tutoe huduma za gesi..sehemu ya kudumu ya visima vya gesi kule baharini iwe ni Mtwara, kwahiyo master plan imelenga hilo ndio maana ikaweka eneo lile la Ziwani kuwa kama logistic park..” alisema.
Mkurugenzi wa halmashauri ya

Kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Mtwara Mikindani, Rashidi Mtima, akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili na kupitisha mpango kabambe wa matumizi ya ardhi kwa halmashauri mbili za manispaa ya Mtwara na halmashauri ya wilaya ya Mtwara.

 wilaya ya Mtwara, Zacharia Nachoa, alisema katika uendelezaji wa mpango huo, kila halmashauri itakuwa na wajibu wa kuona yale yaliopo katika mpango yanatekelezwa, jambo ambalo litasaidia kuondoa ujenzi holela.
“Mwenzako hawezi kujenga kiwanda hapa na wewe unaweka hospitali pale, lazima pawe na namna moja ya upangaji wa matumizi ya ardhi ambayo yanaelekeza kwamba vitu fulani vitafanyika hapa, mambo ya utalii yatafanyika hapa, afya na nini yatakuwa huku..” alisema.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Fatma Ally, aliwahamasisha wananchi kuutambua na kuupokea mradi huo ambao anaamini utawanufaisha kupitia ardhi zao iwapo watazitunza vizuri na kuacha kuwauzia watu kwa ghara za chini ambazo hazitakuwa na tija kwao.

Fatma Ally


Alisema kama wananchi hawna elimu ya kutosha juu ya mpango huo, ni vyema wakawauliza madiwani wao ambao wanauwezo wa kuwaelimisha zaidi huku wakijua kuwa ardhi zao ni thamani kubwa.
“Kwahiyo nawahamasisha wananchi watunze ardhi yao na wasidanganyike wala wasihadaike, kwasababu sasa hivi kuna madalali wengi wanakuja kununua ardhi ili wao wakaiuze kwa wahusika kama wawekezaji..na wale wanunuzi pia nawaambia wasije wakanunua ardhi kienyeji, kwasababu wanaweza kununua ardhi kumbe ni eneo ambalo limetengwa kwa makaburi..” alisema.
Maeneo mengine yaliyotengwa kupitia mpango huo ni eneo la Naumbu lililotengwa kwa ajili ya Viwanda, Mjimwema ambako huko ni kwa ajili ya elimu ya juu, Nanguruwe kumetengwa kwa ajili ya shughuli za kilimo na makazi pamoja na eneo la Mtwara mjini lililotengwa kwa ajili ya shughuli za kibiashara.




No comments: