
Na Juma Mohamed, Mtwara.
Wadau wa
soka na wananchi wa mkoa wa Mtwara kwa ujumla wametakiwa kuisaidia timu ya
Ndanda Fc inayokabiliwa hali ngumu ya kiuchumi ili kuinusuru na madeni
inayodaiwa kwa sasa.
Wito huo
umetolewa hii leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Hawa A. Ghasia wakati alipotembelea kambi ya
timu hiyo na kukabidhi posho ya wiki tatu kwa wachezaji.
![]() |
| Hawa A. Ghasia, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi posho kwa timu ya Ndanda |
![]() |
| Athumani Kambi na Mhe. Waziri |
Huo ni
utaratibu wa Waziri huyo ambae aliahidi kuisaidia timu hiyo inayoshiriki ligi
kuu ya Tanzania Bara, kuwa atakuwa anatoa posho kwa wachezaji kila wiki kiasi
cha sh. Milioni 1.2, mpaka ligi itakapomalizika mwezi mei mwaka huu.
“Kwanza mimi nimesoma Ndanda sekondari, kidato
cha kwanza mpaka cha sita..kwahiyo naweza nikasema kwamba Ndanda ninapoiona
naona kama niko shuleni kwangu, kwahiyo niliamua kujitoa kama mimi kwamba
lazima nitoe kamchango kangu..sio kama nina uwezo ila najibana natafuta na
nawasaidia.” Alisema Waziri.
![]() |
| Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoani Mtwara (MTWRAEFA) Athumani Kambi, akipokea posho za wachezaji |
Alisema
amekuwa akipata malalamiko kutoka kwa viongozi wa timu hiyo kuhusu ukata
walionao kiasi cha kuchangishana pesa za kuiokoa timu kutatua baadhi ya
mahitaji kambini, na kumfanya ajisikie aibu kwa niaba ya wanamtwara wote.
![]() |
| Nahodha wa Ndanda, Wilbert Mweta akitoa shukrani kwa niaba ya wachezaji wenzake kwa Mhe. Waziri, kwa msaada waliopewa. |
Naye Nahodha
wa timu hiyo, Wilbert Mweta, pichani hapo juu ametoa shukrani kwa niaba ya wachezaji wenzake
kutokana na kupokea msaada huo, lakini akisisitiza kuomba kusaidiwa zaidi
kutokana na madeni yanayoikabili kambi ya timu ambayo inakadiriwa sio chini ya
sh. Milioni 4, pamoja na hali ngumu ya chakula.
Mweta
alimtoa hofu Waziri, ambae amekuwa ni kama mlezi wa timu kwa sasa, kwa
kumuhakikishia kwamba timu haitashuka daraja na mikakati yao ni kuhakikisha
wanapata matokeo mazuri katika michezo iliyosalia wakianza na mchezo wa kesho
dhidi ya Mbeya City na ule wa wiki ijayo dhidi ya Tanzania Prisons.
Timu hiyo inateremka
dimbani kesho Aprili 4, kuwakabili Mbeya City ya mkoani Mbeya, katika mchazo ambao ni
muhimu na mgumu kutokana na timu hizo kupishana alama moja Ndanda ikiwa na
alama 23 wakati wapinzani wao wakiwa mbele kwa alama moja.
………………………mwisho………………………………………………………………………..




No comments:
Post a Comment