Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amechukizwa na kitendo cha kuchomwa moto ofisi za chama cha CUF katika jimbo la Dimani visiwani Zanzibar.
Akizungumza mara
baada ya kujionea ofisi hizo zilizoteketea kabisa kwa moto, tukio
lilifanywa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana Malim Seif
alisema hali hiyo inasikitisha na ina lengo la kuchafua hali ya amani na
utulivu iliyopo visiwani Zanzibar kwa sasa.
Aliongeza kwa kulitaka jeshi la Polisi visiwani Zanzibar, kufanya uchunguzi wa kina ili kuwajua watu walio husika kuchoma moto ofisi za chama hicho katika jimbo la Dimani wilaya ya Magharibi Unguja.
Katika tukio hilo inadaiwa watu wasio fahamika walifika katika ofisi hizo usiku majira ya saa nane wakiwa kwenye gari ambapo walitoa matairi na kuyaingiza ndani ya ofisi na kisha kuilipua ofisi hiyo.
Kufuatia jengo hilo kuungua limesababisha hasara ya takribani milioni 135.
Katibu
Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad,
akitembelea Ofisi ya (CUF) jimbo la Dimani kuangalia uharibifu
uliofanywa baada ya ofisi hiyo kuchomwa moto na watu wasiojulikana hivi
karibuni. Picha na Salmin Said, OMKR
SOURCE: TIMES FM
Aliongeza kwa kulitaka jeshi la Polisi visiwani Zanzibar, kufanya uchunguzi wa kina ili kuwajua watu walio husika kuchoma moto ofisi za chama hicho katika jimbo la Dimani wilaya ya Magharibi Unguja.
Katika tukio hilo inadaiwa watu wasio fahamika walifika katika ofisi hizo usiku majira ya saa nane wakiwa kwenye gari ambapo walitoa matairi na kuyaingiza ndani ya ofisi na kisha kuilipua ofisi hiyo.
Kufuatia jengo hilo kuungua limesababisha hasara ya takribani milioni 135.
Katibu
Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad,
akitembelea Ofisi ya (CUF) jimbo la Dimani kuangalia uharibifu
uliofanywa baada ya ofisi hiyo kuchomwa moto na watu wasiojulikana hivi
karibuni. Picha na Salmin Said, OMKRSOURCE: TIMES FM
No comments:
Post a Comment