MANDZUKIC KUIKOSA JUVE OCTOBA 1
|
Mario Mandzukic
|
Na Juma Mohamed
Straika wa Atletico Madrid Mario Mandzukic atafanyiwa upasuaji kwenye
pua lake ambalo lilijeruhiwa wakati wa kichapo cha mabingwa hao wa La
Liga cha 3-2 Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mikononi mwa Olympiakos ya
Ugiriki Jumanne.
Raia huyo wa Croatia mwenye umri wa miaka 28 aliachwa akivuja damu
kwenye pua lake baada ya kugongana na Patjim Kasami dakika ya tatu
lakini alimaliza dakika zote 90 na hata alifunga bao lake la tatu katika
mechi sita tangu ajiunge nao kutoka Bayern Munich Julai.
Mandzukic bila shaka atakosa mechi ya La Liga dhidi ya Celta Vigo
Jumamosi na huenda akakaa nje wiki mbili, na hivyo kutilia shaka
uwezekano wake wa kucheza mechi muhimu ya Atletico ya Ligi ya Klabu Bingwa
Ulaya nyumbani dhidi ya Juventus ya Italia Oktoba 1.
SOURCE: SUPER SPORT
No comments:
Post a Comment