KIBARUA CHA SOLSKJAER KINAELEKEA KUOTA NYASI
|
Ole Gunnar Solskjaer
|
Na Juma Mohamed
Meneja wa Cardiff City Ole Gunnar Solskjaer anatarajiwa kuiacha klabu hiyo baada ya kuwa kwenye usukani miezi tisa.
Solskjaer, 41, alifanya mashauriano na mwenyekiti Mehmet Dalman Jumatano.
Tangazo kuhusu mustakabali wa raia huyo wa Norway linatarajiwa
kutolewa Alhamisi, huku maelezo kuhusu kuondoka kwake yakiendelea
kukamilishwa.
Klabu hiyo, ijulikanayo kwa utani kama Bluebirds (Ndege wa Bluu),
imo katika nafasi ya 17 katika ligi ya daraja la pili baada ya kushindwa
mechi mbili kati ya saba walizocheza, ikiwa ni pamoja na kushindwa kwao
nyumbani 1-0 na Middlesbrough Jumanne na pia kucharazwa 4-2 na Norwich.
SOURCE: SUPER SPORT
No comments:
Post a Comment